Gazeti la Mwananchi lamuangukia Waziri Membe

Katika magazeti yote Tanzania, Mwananchi ndilo gazeti pekee ninaloliamini kwa habari za uhakika za papo kwa papo. Ilikuwaje wakakosea kwa miezi zaidi ya sita iliyopita?

Mkuu Kichuguu hii habari iliandikwa 12 January 2011, hadi hii leo wanapokuja kuikanusha ni zaidi ya mwaka mmoja na miezi sita. Hata mimi ninapata wasiwasi kwamba gazeti la mwananchi linaelekea ku compromise na waziri membe ama serikali.
Kumradhi Waziri Membe

Monday, 23 July 2012

Katika gazeti hili la tarehe 12/01/2011 tulichapisha habari yenye kichwa. Membe: Polisi walikiuka Maadili (Mabalozi waibana Serikali, wahoji polisi kutumia risasi za moto).

Au ni katika harakati za waziri membe kujiweka sawa katika kinyang'anyiro cha ukazi wa magogoni! Kwani ni juzi juzi tu amelipuka kwamba kuna watu hatari 11 ambao ni maadui wake na pia ni maadui wa serikali hii dhaifu. Kwahiyo anatafuta kila namna ya kufyeka vichaka vyote vinavyomzunguka ili kujisafishia njia.
 
Last edited by a moderator:
Gazeti la Mwananchi limepoteza mwelekeo wake kwa sas... Limekuwa ni gazeti la propaganda kwa maslahi ya watu binafsi..
 
Mbona mmekawia sana kuomba radhi? Au mlikua mnashikilia uamuzi wenu mpaka mliposhindwa mahakamani? haukuna uungwana kama mmeshindwa mahakamani ndio mnaomba radhi. Mwaka na zaidi umepita nyie MWANANCHI ndio mnaomba radhi leo! Mwe!


Kwani membe aliwafungulia mashitaka mahakamani juu ya habari hii? mbona mimi sikuwahi kuisikia? SHEKHE Gorogosi unaweza kunikumbusha hii kesi ilifunguliwa katika mahakama gani?
 
Last edited by a moderator:
Mwananchi kwishney.....waliandika uongo na mhariri akapitisha habari sasa wanaomba radhi...Membe kama hujawahonga wakusafishe peleka mahakamani hili gazeti ikiwezekana lifungiwe, lakini kama umepenyeza rupia basi mimi nanyamaza maana nchi hii bana kila kitu kinawezekana. Eti wewe umeiba gari...muombe msamaha mwenye gari...halafu yanaishia hapohapo...hii mpya sijawahi sikia achilia mbali kuona
 
'A wise man changes his mind sometimes..'. Endapo Gazeti la Mwananchi kwa sababu yoyote ile iwayo, wamegundua kuwa waliandika habari ambayo haikuwa sahihi, ni uungwana kuomba radhi, hata kama kosa hilo la kibinadamu ni la muda mrefu. Big up Mwananchi..! Mmeonyesha njia, Vyombo vingine vya Habari vinapaswa kuiga mfano wenu. Kuomba radhi sio ujinga, ni uungwana tuu, hata kama kosa ni la zamani, muda haulifanyi kuwa sahihi na katika hili Muhariri wa Mwananchi ameonyesha Weledi kazini.
 
Mwananchi acheni hadaa.
Naomba ufafanuzi wa mambo yafuatayo toka kwa yeyote mwenye uelewa wa jambo hilo.
Hivi unaweza kuandika habari kwa bahati mbaya? Ina maana kuwa habari hiyo ulikuwa nayo lakini hukukusudia kuichapa kwenye toleo hilo au gazeti hilo, hivyo ni ya kweli.
Uchunguzi wao waliufanyia wapi na wahusika ni akina nani?
Ni kitu gani kiliwafanya Mwananchi kufanya uchunguzi wa habari hiyo baada ya kuitoa?
Kama walikuwa wanafanya uchunguzi wa habari hiyo, ni Kwanini hawakuujulisha Umma mapema walipo anza?
Kwa uelewa wangu, habari kama haina uhakika au haijadhibitishwa, au kama mhusika mkuu (Membe) alikanusha alopoulizwa ili ku balance habari huwa inaelezwa hivyo kwenye gazeti au chombo husika kilichotoa habari hiyo.
Je Mwananchi walifanya hivyo? Kama hawakufanya hivyo, walikuwa na uhakika wa habari hiyo au waliamua kumchafua Membe. Lakini je kulikuwa na malalamiko yoyote kuhusu habari hiyo kutoka kwa pande zilizo husika, yaani polisi,serikali au mtu yeyote?
 
Kwa kweli hili gazeti sasa limepoteza credibility, nilimshuhudia Membe akiongea na kutamka maneno hayo kwenye tv, halafu leo mhariri anakana ili kumsafisha kwa manufaa ya kisiasa ya Membe. Kwa unafiki huu wa mhariri na gazeti kwa ujumla shame on you!!! na msishangae kuona watu makini wakisusia kununua hard copy ya magazeti yao.tulikuwa tunafikiri labda gazeti la Mwananchi linasimamia ukweli kumbe ni walewale waganga njaa.

Kama kwa mtu tu kama Membe hata kama ni waziri wako wanafiki kihivyo sasa kwa lidude kama Serikali au taasisi zake za mabavu wanaweza kusimamia na kuandika ukweli!? kwa kweli wameliahibisha na kuishusha thamani sio tu gazeti lao la Mwananchi bali taasisi yao ya Mwananchi communication mbele ya watu makini.
 
Tanzania kila kitu kinawezekana.
Wanajanvi wengi walishangilia humu JF baada ya Dunstan Tido Mhando kuwa mkulugenzi wa Mwananchi hawakujua kuwa wajanja wameanza mkakati wa kujipenyeza katika chombo hicho ambacho kilikuwa kinaonekana ni tishio kwa uhai wa wajanja wanakula kuku kwa mrija.
Kubali, Kataa lakini huu ndio ukweli. TANU na CCM kuitawala nchi kwa zaidi ya miaka 50 hakujatokea by chance bali ni kwa mikakati ya hali ya juu sana.

Ninashangaa wanajanvi wengi hapa kila mara wanasema kwa kejeli maneno kama CCM (RIP IN ADVANCE) lakini ukweli ni kuwa, we have a big fight ahead for CCM to be buried forever.

Kwa Mwananchi kuanza kubadili mwelekeo kwa wanajua siasa hawawezi kushangaa kwa sababu walitegemea kama hili litatokea.

Toka mwanzo sikukubaliana na hili swala la vua gamba vaa gwanda bila ya kuwa na proper vetting mechanism.

Kwa mtaji huu, Chama kitajaa mamluki.
 
kumradhi waziri membe

monday, 23 july 2012

katika gazeti hili la tarehe 12/01/2011 tulichapisha habari yenye kichwa. Membe: Polisi walikiuka maadili (mabalozi waibana serikali, wahoji polisi kutumia risasi za moto).

Habari hiyo ambayo ilifuatia tukio la vifo vya watu watatu na majeruhi kadhaa vilivyotokea mjini arusha wakati polisi walipokabiliana na waandamanaji wa chadema, ilidai kwamba waziri membe alililaumu jeshi la polisi kwa kukiuka maadili, kuvuka mipaka yake na kusababisha mauaji hayo ambayo yalitia doa tanzania.

aidha habari hiyo iliendelea kudai kwamba mabalozi wa nchi mbalimbali walimbana wakitaka tamko la serikali juu ya tukio hilo.

Baada ya uchunguzi wa kina, gazeti hili limebaini kuwa, waziri membe hakusema maneno hayo na wala hapakuwa na mvutano wala madai yeyote ya mabalozi juu ya jambo hilo.

Kutokana na hayo, tunachukua fursa hii kumwomba radhi waziri membe, jeshi la polisi, serikali, mabalozi wote na wananchi kwa ujumla.

Aidha tunapenda kumhakikishia waziri membe na wasomaji wote kwa ujumla kwamba habari hii iliandikwa kwa bahati mbaya na kwamba gazeti hili litaendelea kufanya kazi yake kwa kufuata misingi ya taaluma ya uandishi wa habari, maadili na sheria za nchi bila kumwonea mtu au kushinikizwa na mtu yoyote kwa maslahi binafsi.

Mhariri
nidhamu ya uoga ...inamaana mpaka habari inatoka kulikuwa hakuna editng as to the authentification ya habar husika.....yaani hadi magazeti yetu nayo yameshanunuliwa.
 
Mbona mmekawia sana kuomba radhi? Au mlikua mnashikilia uamuzi wenu mpaka mliposhindwa mahakamani? haukuna uungwana kama mmeshindwa mahakamani ndio mnaomba radhi. Mwaka na zaidi umepita nyie MWANANCHI ndio mnaomba radhi leo! Mwe![/QUOTE
WAMESHAINGIZWA KWENYE PAYROLL CHEZEA RAIS MTARAJIWA...
 
Kwa kweli hili gazeti sasa limepoteza credibility, nilimshuhudia Membe akiongea na kutamka maneno hayo kwenye tv, halafu leo mhariri anakana ili kumsafisha kwa manufaa ya kisiasa ya Membe. Kwa unafiki huu wa mhariri na gazeti kwa ujumla shame on you!!! na msishangae kuona watu makini wakisusia kununua hard copy ya magazeti yao.tulikuwa tunafikiri labda gazeti la Mwananchi linasimamia ukweli kumbe ni walewale waganga njaa.

Kama kwa mtu tu kama Membe hata kama ni waziri wako wanafiki kihivyo sasa kwa lidude kama Serikali au taasisi zake za mabavu wanaweza kusimamia na kuandika ukweli!? kwa kweli wameliahibisha na kuishusha thamani sio tu gazeti lao la Mwananchi bali taasisi yao ya Mwananchi communication mbele ya watu makini.


Hili sasa limedhihirika kwamba magazeti haya ama yanatumiwa au yanakurupuka. At long last Membe has been vindicated though I am not sure whether the apology has what is takes to restore one's reputation that has been dented by reckless jounalism. Natumaini magazeti mengine ambayo kila kukicha yamegeuka kuwa karakana za kupaka matope wenzao kuwa maliwato ya kutakasa mafisadi waliochafuka na kuwachafua walio weipe kama theluji watajifunza kuwa na uandishi wenye maadili! This is what we call eating a humble pie, stupid!
 
Kwasasa habari ambazo nitakuwa na imani nazo ni live za kwenye tv tu, magazeti hayaeleweki kwa sasa, jana tena nimemsikia membe kwenye jahazi clouds fm akisema mwananchi walimnukuu vibaya kutoka itv, nassari naye kwa sasa ukisoma habari kwenye gazeti lazima uhulize kama ni kweli kwa watu waliosoma magazeti mengine au walio angaria tv.
 
Baada ya uchunguzi wa kina, gazeti hili limebaini kuwa, Waziri Membe hakusema maneno hayo na wala hapakuwa na mvutano wala madai yeyote ya Mabalozi juu ya jambo hilo.
 
Cjapata ona,sa uyo mwandishi aliepeleka vp iyo habar wakat hana vithibitisho vya kutosha czn kama ata anastahil kuendelea na kaz,yn wanashindwa hata na magazet ya udaku yanaandika habar japo hailingan na uhalica wa kichwa cha habar but at the end mhucka waliongea nae au walipiga picha sasa uyu mwandish ilikuaje ?
 
Sasa mbona hawazungumzii kumlipa fidia ya mabilioni ili uwe mtaji wake hapo baadaye!
 
Back
Top Bottom