Wadanganyika wangapi mumeamka? Na hiyo idadi yenu inatosha kumweka rais mumtakaye come 2015? Au unaendelea kudanganyika na idadi ya hapa JF? Na kama tumaini lako ni idadi ya wachangiaji wa hapa jukwaani basi huko sasa kudanganyika kubaya na ni usingizi mbaya zaidi kuliko ule tuliokuwa tumelala awali.Tuingie mitaani,twende humo vijijini kote tukawaamshe watanganyika wenzetu wengine na si kujiridhisha na michango ya wanajukwaa wenzetu hapa.Fanya wafanyavo LOWASSA hasafishiki, wadanganyika tumeamka na hatuko tayari kuedelea kudanganywa, hatuko tayari kuona watu wanachukulia advantage ya umaskini wetu kujinufaisha wao, hatuko tayari kuona MWIZI ambae huhitaji uwe na degree kumfahamu kuwa Mwizi anachukua nyumba yetu nyeupe ambayo baba yetu alituambia pale ni sehemu patakatifu.
Lowassa usipoteze pesa, nguvu na muda wako bure, amini ukiwa raisi kwa HILA nchi hii haitotwalika, tutakuwa tayari kuipigania taifa letu kwa gharama yoyote, tutalinda heshimana utu wetu