Gazeti la Freeman Mbowe latumika kumsafisha LOWASSA

Mungu atunusuru na hili na lingine lijalo. Kuna siri nzito sana inakuja

Uko sahihi Mkuu Kiranja, hili ni janga la kitaifa. Naomba ninukuu mjadala mmoja sitotaja wapi na nani alisema maneno haya, aalisema yafuatayo;

"Gazeti la Tanzania Daima lilianzishwa na Freeman Mbowe kwa jina la mkewe Dk.Lilian Mbowe, na mwandishi mwanzilishi kwa maana ya mipango na mikakati alikua Deodutus Balile akiwa na wenzake Jacton Manyerere na Mbaraka Islam na wengineo wakajiunga nao. Balile alitumia uzoefu wake wa kuanzisha gazeti la Mwananchi (kabla halijanunuliwa na Nation) na walipanga timu na mikakati yote ikiwa ni pamoja na kuita waandishi wengine kama vile Erick Anthony, Joseph Senga na wengineo kujiunga nao japo Islam aliwatosa na kwenda kushirikiana na wengine kuanzisha Thisday.

"Wakati wa kuanzishwa kwa Tanzania Daima ilikua kipindi cha mchakato kuelekea 2005 ambako aliyekuwa Rais Benjamin Mkapa, hakuwa akimtaka Jakaya Kikwete na Edward Lowassa, na hivyo JK na Lowassa walianza kufanya mazungumzo na Mbowe kuangalia uwezekano wa kujiunga na Chadema ikiwa watatoswa na CCM.(Nitajadili siku nyingine). Mazungumzo hayo yaliratibiwa vyema na Rostam Aziz na Lowassa japo Mbowe aliona Lowassa anafaa zaidi kuwa Rais kuliko JK. Kwa msingi huo upo uwezekano mkubwa kwa Tanzania Daima kupata msaada kutoka kwa kina Lowassa maana lilianzishwa kwa mtaji mkubwa na lilitumika hata wakati wa mchakato 2005. Kwa ujumla pamoja na yote, bado Mbowe binafsi ana siri nzito na Lowassa na pengine ndio maana Kibanda ana jeuri ya kufanya hayo bila kuguswa na wamiliki. Hata Balile aliondoka lakini akapokewa Mtanzania aliko hadi sasa na iko siku histroria itaanikwa. Hata suala la Fredrick Sumaye kuzungumza na Chadema lilipoibuika, JK aliambiwa hakuna dhambi maana hata yeye 2005 alizungumza na Chadema."

Naomba kuwasilisha mengine nitayaleta wakati mwafaka na baadhi ya waliotajwa ni member wa JF wataongezea nyama nyama.
 
Uko sahihi Mkuu Kiranja, hili ni janga la kitaifa. Naomba ninukuu mjadala mmoja sitotaja wapi na nani alisema maneno haya, aalisema yafuatayo;

"Gazeti la Tanzania Daima lilianzishwa na Freeman Mbowe kwa jina la mkewe Dk.Lilian Mbowe, na mwandishi mwanzilishi kwa maana ya mipango na mikakati alikua Deodutus Balile akiwa na wenzake Jacton Manyerere na Mbaraka Islam na wengineo wakajiunga nao. Balile alitumia uzoefu wake wa kuanzisha gazeti la Mwananchi (kabla halijanunuliwa na Nation) na walipanga timu na mikakati yote ikiwa ni pamoja na kuita waandishi wengine kama vile Erick Anthony, Joseph Senga na wengineo kujiunga nao japo Islam aliwatosa na kwenda kushirikiana na wengine kuanzisha Thisday.

"Wakati wa kuanzishwa kwa Tanzania Daima ilikua kipindi cha mchakato kuelekea 2005 ambako aliyekuwa Rais Benjamin Mkapa, hakuwa akimtaka Jakaya Kikwete na Edward Lowassa, na hivyo JK na Lowassa walianza kufanya mazungumzo na Mbowe kuangalia uwezekano wa kujiunga na Chadema ikiwa watatoswa na CCM.(Nitajadili siku nyingine). Mazungumzo hayo yaliratibiwa vyema na Rostam Aziz na Lowassa japo Mbowe aliona Lowassa anafaa zaidi kuwa Rais kuliko JK. Kwa msingi huo upo uwezekano mkubwa kwa Tanzania Daima kupata msaada kutoka kwa kina Lowassa maana lilianzishwa kwa mtaji mkubwa na lilitumika hata wakati wa mchakato 2005. Kwa ujumla pamoja na yote, bado Mbowe binafsi ana siri nzito na Lowassa na pengine ndio maana Kibanda ana jeuri ya kufanya hayo bila kuguswa na wamiliki. Hata Balile aliondoka lakini akapokewa Mtanzania aliko hadi sasa na iko siku histroria itaanikwa. Hata suala la Fredrick Sumaye kuzungumza na Chadema lilipoibuika, JK aliambiwa hakuna dhambi maana hata yeye 2005 alizungumza na Chadema."

Naomba kuwasilisha mengine nitayaleta wakati mwafaka na baadhi ya waliotajwa ni member wa JF wataongezea nyama nyama.

Heshima kwako Tina,

Nakubaliana na hoja zako 100%.
 
Kwani Mbowe ana usafi kiasi gani?
Mchunguzeni sana katika biashara zake kuna uchafu mwingi hata ruzuku anakula sana
 
Kwani Mbowe ana usafi kiasi gani?
Mchunguzeni sana katika biashara zake kuna uchafu mwingi hata ruzuku anakula sana

Sidhani kama uchafu ama usafi unatoa nafasi ya kuvuruga demokrasia.. Hiyo ni hulka tu ya mtu
 
Uko sahihi Mkuu Kiranja, hili ni janga la kitaifa. Naomba ninukuu mjadala mmoja sitotaja wapi na nani alisema maneno haya, aalisema yafuatayo;

"Gazeti la Tanzania Daima lilianzishwa na Freeman Mbowe kwa jina la mkewe Dk.Lilian Mbowe, na mwandishi mwanzilishi kwa maana ya mipango na mikakati alikua Deodutus Balile akiwa na wenzake Jacton Manyerere na Mbaraka Islam na wengineo wakajiunga nao. Balile alitumia uzoefu wake wa kuanzisha gazeti la Mwananchi (kabla halijanunuliwa na Nation) na walipanga timu na mikakati yote ikiwa ni pamoja na kuita waandishi wengine kama vile Erick Anthony, Joseph Senga na wengineo kujiunga nao japo Islam aliwatosa na kwenda kushirikiana na wengine kuanzisha Thisday.

"Wakati wa kuanzishwa kwa Tanzania Daima ilikua kipindi cha mchakato kuelekea 2005 ambako aliyekuwa Rais Benjamin Mkapa, hakuwa akimtaka Jakaya Kikwete na Edward Lowassa, na hivyo JK na Lowassa walianza kufanya mazungumzo na Mbowe kuangalia uwezekano wa kujiunga na Chadema ikiwa watatoswa na CCM.(Nitajadili siku nyingine). Mazungumzo hayo yaliratibiwa vyema na Rostam Aziz na Lowassa japo Mbowe aliona Lowassa anafaa zaidi kuwa Rais kuliko JK. Kwa msingi huo upo uwezekano mkubwa kwa Tanzania Daima kupata msaada kutoka kwa kina Lowassa maana lilianzishwa kwa mtaji mkubwa na lilitumika hata wakati wa mchakato 2005. Kwa ujumla pamoja na yote, bado Mbowe binafsi ana siri nzito na Lowassa na pengine ndio maana Kibanda ana jeuri ya kufanya hayo bila kuguswa na wamiliki. Hata Balile aliondoka lakini akapokewa Mtanzania aliko hadi sasa na iko siku histroria itaanikwa. Hata suala la Fredrick Sumaye kuzungumza na Chadema lilipoibuika, JK aliambiwa hakuna dhambi maana hata yeye 2005 alizungumza na Chadema."

Naomba kuwasilisha mengine nitayaleta wakati mwafaka na baadhi ya waliotajwa ni member wa JF wataongezea nyama nyama.

Hii imechakachuliwa kidogo!! lakini Tina unaonekana uko ndani ya Tanzania Daima ama ulikuwamo, tupe data zaidi
 
Huko ndie kule kusema unasoma btn the lines, unasoma na kuona hapana something is wrong somewhere! I have been doing so even kwa mwanahalisi na nikaja kugundua ni la JK, na sasa kumbe TZ daima la Lowassa! niliacha kusoma Tz daima mwaka wa nne sasa.

Kuna vitu unasoma, unatafakari/meditate na unaona havijakaa sawa, haviko vinavyotakiwa kuwa they call this 'critical thinking' unaangalia manufaa ya mwananchi kwa kusoma hiyo habari.

Kibanda tangu alipoingilia uchaguzi wa mwenyekiti wa chadema nilianza kuwa na wasiwasi naye kama huyu mwandishi wa habari kweli yuko fair, nilishangaa pia kuona hata Kubenea ana uvuruga ule uchaguzi na kusaidia kubakwa kwa demokrasia waziwazi!

asanteni kwa michango yenu, napata soda bariiidi hapa huku nikitafakari mliyoyaandika
 
Kwani kuna tofauti gani kati ya mbowe na chadema? Chadema ni mali ya mkwe wake kwahiyo ni mali yake pia na gaazeti pia ni mali yake unauliza kitu gani?
CCM ni mali ya nani?....nina wasiwasi na uwezo wako wakufiri..
 
Nimeisoma makala ya Tanzania Daima sijaona popote ambapo gazeti limejaribu kumsafisha Lowassa. Lowassa aliulizwa maoni yake juu ya baraza la mawaziri na akaitumia fursa hiyo kulalamika kuwa anapakaziwa kwamba alimshinikiza rais Kikwete amuingize kwenye baraza la mawaziri jambo ambalo amesema si kweli, pia akamtetea Frederick kuwa ripoti za gazeti moja kuwa amenunua nyumba London na anachunguzwa si za kweli. Hii kwa mwandishi habari yeyote si juhudi za kumsafisha Lowassa. Hii makala ingeweza kuandikwa pia Daily News au Raia Mwema, kwani ni mtazamo wa Lowassa. Sijaona hapo juhudi zozote za kumsafisha.
 
Jamani hivi hamfahamu urafiki wa muda mrefu kati ya lowassa na mbowe mbona wengi wanafahamu ? Fuatilieni mikutano ya mbowe yuko tayari kumpiga madongo jk lakini hata siku moja hataweza kufanya kwa lowassa.
 
Nimeisoma makala ya Tanzania Daima sijaona popote ambapo gazeti limejaribu kumsafisha Lowassa. Lowassa aliulizwa maoni yake juu ya baraza la mawaziri na akaitumia fursa hiyo kulalamika kuwa anapakaziwa kwamba alimshinikiza rais Kikwete amuingize kwenye baraza la mawaziri jambo ambalo amesema si kweli, pia akamtetea Frederick kuwa ripoti za gazeti moja kuwa amenunua nyumba London na anachunguzwa si za kweli. Hii kwa mwandishi habari yeyote si juhudi za kumsafisha Lowassa. Hii makala ingeweza kuandikwa pia Daily News au Raia Mwema, kwani ni mtazamo wa Lowassa. Sijaona hapo juhudi zozote za kumsafisha.

Jasusi, Heshima yako Mkuu. Usemayo ni sahihi kabisa lakini inahitaji ujasiri wa hali ya juu kuzungumza na Lowassa kwa wakati huu na Tanzania Daima lina ujasiri wa kutenda haki (fair) na hivyo kuweza kusimamia haki ya wale wanaokosa pa kusemea kwa kwa sasa Lowassa ni mnyonge kwa kuwa amekosa pa kusemea kwa waandishi kumuona mchafu kama ambavyo Fred Sumaye alikua akikimbiwa na magazeti kuelekea 2005. Lakini pamoja na kutenda haki huko, kama gazeti makini, lilipaswa kuangalia baadhi ya mambo ya msingi hasa uzito wa habari husika (zilizokanushwa) na uzito wa majibu yaliyotolewa. Mjadala wake ni mpana lakini Tanzania Daima pia wanapaswa kupongezwa lakini wanapaswa kuwa makini sana. Kuna mjadala mpana ambao unaendelea kuhusu mauaji ya 'watu wenye hasira kali', na polisi kuua majambazi. Kwa ujumla Tanzania Daima wamejitahidi sana kuwa makini na kutenda haki
 
Nimeisoma makala ya Tanzania Daima sijaona popote ambapo gazeti limejaribu kumsafisha Lowassa. Lowassa aliulizwa maoni yake juu ya baraza la mawaziri na akaitumia fursa hiyo kulalamika kuwa anapakaziwa kwamba alimshinikiza rais Kikwete amuingize kwenye baraza la mawaziri jambo ambalo amesema si kweli, pia akamtetea Frederick kuwa ripoti za gazeti moja kuwa amenunua nyumba London na anachunguzwa si za kweli. Hii kwa mwandishi habari yeyote si juhudi za kumsafisha Lowassa. Hii makala ingeweza kuandikwa pia Daily News au Raia Mwema, kwani ni mtazamo wa Lowassa. Sijaona hapo juhudi zozote za kumsafisha.

Hii ndio huitwa Hekima. Nimesoma kilichopositiwa na kichwa cha uzi nikakosa mnyumbuliko.
Nikasoma maoni yote sioni wakinisaidia kuonyesha huo usafishaji. Mwandishi kupata habari ya upande wa pili imekuwa kusafisha mwe! Halafu ndio watu hapa kila siku hupiga kelele tunataka upande wa pili'
Watu wengine ndio wametoka nje ya ya kilichoandikwa na kuanza kuleta data zisizohusiana. Mbowe si Mhariri wala si mwandishi na hakuna mwenye ushahidi kuwa kabla gazeti halijachapwa anapitia na kuruhusu ni kiandikwe au kisiandikwe. Kwa ujumla hii thread ni utumbo haina kitu cha maana ndani yake.
 
Back
Top Bottom