Gazeti la Dira: Kashfa ya kuhongwa - Zitto, Ole Sendeka, Sarah Msafiri na Anne Kilango watajwa

Mimi siamini kuwa Zitto kachukua chochote, isipokuwa kiherehere chake cha kujiingiza katika mgogoro kati ya wizara na tanesco ndivyo vimemponza. Lilikuwa kosa kusema Mhando arejeshwe kazini bila kujua ukweli kuwa Mhando ana ufisadi alioufanya. Ninajua kuwa laiti Zitto angejua ufisadi huo, asingekimbilia kumtetea. Sasa mdogo wangu Zitto, huna wa kumlaumu, ni wewe mwenyewe, acha kiherehere, mtu anayetaka urais huwa hasemi sana, wewe humwoni mwenzako Lowasa yuko kimya!!! ama humuoni Slaa yuko kimya!!!. Tulizana. sasa umeshanuka sana, itakugharimu sana kujijenga tena.
 
Zitto ni mnafiki mkubwa na tangu aonje asali anataka kuchonga mzinga ili kuwa rais lakini ashukuriwe Mungu kwa sababu huwa hamfichi mnafiki
 
Nahisi hiki kitanzi cha sasa kinaweza kuwa the most difficult one kuvuka - kwa pande zote. Tuombe mungu aingilie kati.

spika ameelemewa tena sana...huwezi kuamini katika list ya wabunge waliokula rushwa jina la zitto halimo lakini azimio la kikao cha jana usiku na taarifa zilizokwenda kwa spika hiyo jana zinataka zitto aingizwe na atajwe...akikubaliana na wanachotaka na yeye akafanya kama wanavyotaka basi atakuwa amejiharibia sifa ya kuwa spika...
 
Zito, mwenendo wake ulianza kutiwa shaka mapema, Sendeka na Kilango gafla waligeuka kuwa mabubu kwenye harakati za kupinga ufisadi. Shame upon them!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
kuchukua sitting allowance si kosa kwani ni haki ya kila mbunge.

Yaani ulipwe mshahara wa Mbunge na ulipwe kwa kuwa Bungeni kama sio ufisadi huo ni nini?
Nini tofauti yao na ccm..? unaposhabikia chama usiwe kipofu moja kwa moja,fikiri.
 
hii nchi! bora kusiwe na rais wala serikali, ingewezekana tukajiongoza wenyewe! naitema puuuuuu![/QUOT

nyerere aliiaribu hii nchi, tunavumiliana sana katika hii nchi, imagine andrew chenge na uchafu wote alio nao anaongoza kamati ya fedha ya bungu, Lowasa ivyo ivyo nae kamati ya bunge ya mambo ya nje.
nimesikitika sana bali natoa rai kama uchafu huu unajumuisha pia wabunge wa chadema, namuomba Dr slaa achukue hatue kali sana dhidi ya yeyote atakaebainika kwani tuko nyuma yake, hasa tukizingatia wenzetu wa CCM wamezoea wizi maana ata mh. JK alitajwa kuhusika katika richmond na mpaka leo hajawai kukanusha
 
Suala hili ni nafuu kwa CDM kwa kutokea wakati huu kwani kama itachukua hatua kali kwa wabunge wa CDM watakaobainika katika sakata ili itakuwa inajisafishia njia nzuri katika uchaguzi wa 2015 kwani itaongeza imani ya kiutendaji kwa wananchi, kwa upande wa CCM hii itakuwa ni ongezeko la kashfa nyingine zaidi ya nyingi zilizopita na uwezekano wa kujipanga na kuleta imani kwa wananchi ni ngumu sana kwani watatakiwa wawajibishwe wengi tangu enzi ya BWM ili wananchi tuweze kuwa na imani na serikali na viongozi wa CCM kwani tangu kashfa zimeanza hakuna aliyewajibishwa hata mmoja kinachofanyika ni kumuondoa au kumbadilisha mtu katika nafasi yake.
 
Gazeti la Dira leo limekuwa lulu kwa Pro-Chadema ha haa haaa tutasikia mengi kuelekea uchaguzi.

umeona eheeee, natumai umefurai sana, kwani CCM wao watu wa aina hii ulindwa kwa kila khali, si wakumbuka waliousika meremeta, kagoda, deep green nk ata mizengo pinda anawalinda
 
MVUMBUZI Usi generalize,tatizo la Zitto si la upinzani,kwani kila siku umekuwa ukisikia watu wakimnanga Zito kuwa hafai na ana UCCM fulani,aliyoyafanya kwa wachambuzi wa mambo sio ajabu
 
Last edited by a moderator:
duh..hapa lazima pachimbike..kumbe wanasiasa wote wanafiki, hakuna mkweli hata mmoja, na ole wao waje kuniomba kura..napiga risasi huko huko
 
spika ameelemewa tena sana...huwezi kuamini katika list ya wabunge waliokula rushwa jina la zitto halimo lakini azimio la kikao cha jana usiku na taarifa zilizokwenda kwa spika hiyo jana zinataka zitto aingizwe na atajwe...akikubaliana na wanachotaka na yeye akafanya kama wanavyotaka basi atakuwa amejiharibia sifa ya kuwa spika...

Kwa bahati mbaya tuna Spika dhaifu kushinda maelezo. Lazima ata-mismanage hii kitu. Hata jinsi alivyo-handle hoja ya Vita Kawawa na kuvunja kamati ya Nishati ameacha maswali mengi sana. Ndio shida ya kupeana kazi mezani. Yeye mwenyewe Spika hana intergrity ya kukalia hicho kiti.
 
Habari kuwa kuna wabunge wa upinzani wanaohusika kuihujumu TANESCO zimepokelewa kwa masikitiko makubwa sana na imewafanya wananchi wengi kukata tamaa. Kwa ufupi wananchi tulikuwa tunawaunga mkono vyama vya upinzani tukijua wana dhamira ya kuleta mabadiliko na hatimaye kuboresha maisha ya watanzania. Kinachoonekana kutokana na taarifa za Waziri Sospether Muhongo ni kwamba hakuna tofauti kati ya CCM na vyama vya upinzani kwani lengo lao ni moja tu kutumia rasilimali za watanzania kunufaisha matumbo yao na familia zao in the expense ya maumivu na matatizo ya watanzania. Hii ni dhambi kubwa. Binafsi nimebaki njia panda kuhusu kwa nani watanzania tuweke matumaini yetu kuhusu mustakabali wa maisha bora kwa kila mtanzania. Watanzania tunasalitiwa na viongozi waroho ambao kwa wananchi wanajidai kondoo kumbe ndani ni Mbwa mwitu wabaya. Kwa viongozi wa namna hii tusitarajie tena mabadiliko hata kama CCM tutaiondoa kwani tunafanya yale yale yanayotufanye tupigane usiku na mchana kukiondoa chama dhalimu CCM madarakani. Si mambo ya kufumbia macho kwa sababu ya ushabiki wa kichama bali kutumia jicho la pili kuona upande mwingine wa shilingi na kufanya maamuzi yatakayo rudisha heshima ya vyama vinavyohusika na hatimaye kurudisha matumaini kwa waTZ. Viongozi hawa watajwe hadharani na wapewe adhabu inayostahili na wasipewe tena nafasi ya kuongoza kwani wamekosa adabu na credibility. Hii haina tofauti na kuku kula vifaranga wake.
Mtaani kwangu watu wamebaki na maswali mengi kuliko majibu na yanatakiwa yapate majibu kutoka kwa viongozi hawa hawa kwani doa lililosababishwa na wahusika ni kubwa sana.
INANIWIA KUSEMA HERI mtikila agombee urais
 
Kaaaazi kweli kweli, ndo maana siku ile kamati inavunjwa Zitto alionekana mpoleee na pia zile kashfa wakati zatajwa kaonekana kuloa kinoma, mwenendo wa Zitto cdm na mihela yake zilikuwa zatia shaka, nasikia anamiliki Hummer na magari kibao ya kifahari daaaah, kweli njaa kitu kibaya.Mi nashauri cdm wamfukuze uanachama maana ni tatizo muda mwingi.

Naunga mkono hoja ikithibitika Nyepesi kala rushwa,hii haikubariki Zitto hela umepata wapi kununua hummer na vogue? Zitto unaichafua CDM,hakika dr slaa mfukuzeni huyu mtu ikithibitika otherwise hatakiua chama kwa tamaa za kijinga mwandiga tunamsubiri tumpe vidonge vyake!!
 
Hizi stori zote zinatengenezwa kuondoa upepo wa kutekwa kwa Dr ULIMBOKA na TISS kwa maagizo ya IKULU.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom