Leo asubuhi nikiwa nasikiliza mapitio ya magazeti kwenye Radio Magi FM nimesikia kwa mara nyingine tena mtangazaji akisema kwa kujiamini "Sasa nimeshika gazeti xyz "GAZETI LA CHAMA"Kwa kuwa mimi ni wa kizazi cha enzi hizo za chama kimoja nimeelewa mtangazaji alimaanisha nini anapozungumzia juu ya "CHAMA". je aliyezaliwa baada ya kuanzishwa kwa vyama vingi hapa aeleweje? Na cha ajabu ni vyombo vingi vya habari hurudia kauli hii Gazeti la CHAMA.. Wana JF mlio karibu na hawo watangazaji jaribu kuwaelimisha.