Gavana Ndulu ahofia vijana Tanzania kuingia mitaani kama Misri!

MUONGO PINDA SIJUI ANAJISIKIAJE. Umaarufu unashuka kwa kasi. Kumbe pozi zote kwenye PM QUESTIONS kichwa linafikiri uongo
 
Uharo mtupu. Sina uhakika kama uko sawa, nadhani leo bange umezidisha kidogo.

Nyamafu!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

* Taifa lapoteza sh. trilioni 1 kwa mwezi

Si nyinyi ndio mlipinga hii mitambo ya Dowans isinunuliwe?


* Hofu yatanda maelfu ya vijana kukosa ajira

Wasiokuwa na ajira ndio watapata ajira serikali hii ikiondoka? Ajira alizoahidi ni million moja, mpaka sasa kisha towa zaidi ya hizo.

* Ukali wa maisha wawaacha Watanzania hoi

Hoi kuliko wakati wa Nyerere? Hata viwembe vya kunyolea ilikuwa havipatikani! Ukikogea Lux, harufu tuu, unaonekana wa maana? Wakati upi hoi zaidi?

* Serikali yang'ang'ania mchezo wa Dowans

Mchezo upi wa Dowans? Jee, Dowans wanakosa lipi? Na inawahusu nini siasa yenu?

Kwa nini mnaingiza matatizo ya umeme kwenye siasa? Kwani matatizo ya umeme yalianza kwa JK?

Mlianza na kutomtambuwa Rais, mkaona hapa pagumu!

Mkaja na Katiba, mkanuyamazishwa kiulaini.

Mnakuja na Dowans, kaja mwenye Dowans bado hamtaki. Na majuha wanawasikiliza.
 
Mkwere mwenyewe analielewa hilo? Kazi kwake na mawaziri wake hewa aliyewaweka,mwaka huu kwake lazima kieleweke tu lazima aelewe na ataelewa tu!
 
Waziri mkuu wa nchi hii alishatangaza kuwa uchumi haujatetereka leo hii anakuja gavana anasema hali ni mbaya, hivi wewe pinda tukuchukulie vipi? Ulianza na albino ukalia bungeni watu wakakustahi, dowans ukasema ni genge la watu wachache wanaofahamika baadaye ukafyata mkia ukasema tuwalipe tukakustahi, ukaulizwa bungeni kuhusu maandamano ya arusha ukadanganya bungeni zaidi ya mara kumi on same day! Tukakustahi, juzi tuu hapo ukasema mgao haujasababisha uchumi kutetereka! Leo wanaojua uchumi gavana wa BOT anasema tunayumba, hivi wewe pinda kweli mbona sura yako (muonekano) haviendani kabisa na hayo mauongo unayosema kila siku! Hivi ww unajivunia kuitwa mtoto wa mkulima! Kweli tuna viongozi vilaza
 
Gavana kasema kweli, na hawa wanafik wa Chadema ndio opportunity wanayotumia ya kuwarubuni (brainwash) hawa vijana wasio na kazi maalum. Wanawadanganya kuwa Serikali iliyopo madarakani ikiondoka leo, kesho nyie wote mna kazi tena za kuwaongoza hawa tunaowatoa madarakani. Duhh, uongo mtupu!

Matatizo yanayozungumziwa sasa yanatokana na mgao wa umeme. Hapa serikali na ccm ndiyo wa kulaumiwa!

Wote tunajua kuwa hatukufika hapa kwa bahati mbaya, ni kwasababu ya ufisadi juu ya swala la nishati na si serikali wa ccm anayesimama na kukemea ufisadi huu. Matokeo yake wote wameonekana kama vile mashabiki wa ufisadi (DOWANS)

Kukumbusha tu:

Ni mwisho wa 2009 ndipo tanesco ilitaka kuinunu Dowans kwa na kuzuiwa Je kwanini tokea wakati huo hakuna mitambo mingine iliyonunuliwa?

Alafu mwenye akili ashindwe kuona kuwa serikali (yaani ccm) inahusika!. Ukibadirisha serikali utaondoa tatizo hili kwa sababu hii serikali inaendeleza tatizo kwa kutowawajibisha waliotufikisha hapa. Wekeni ushabiki wenu wa vyama pembeni na tatueni matatizo ya nchi yetu.........!

Sitashangaa kama itazaliwa Dowans nyingine uko tuendako!
 
Ndio wanagutuka??? What do you expect if 60% of youth in urban areas are unemployed (Wizara ya kazi statistics, 2006)???


Wacha vijana waingia kwenye maandamano 5 years ago I was a lone voice nikiwapiga vita wageni kupendelewa na kuchukua kazi ambazo zinaweza kufanywa na Watanzania hivi sasa sioni ajabu kwa nini wanagutuka. Wamechelewa wanavuta shuka wakati jogoo amewika khe khe khe khe kheeeeeeeeeeeeeeeeeee na bado hilo jinamizi la EAC likiingia vizuri ndio watajua zipi ni mbivu.
 
Nadhani katoa kauli hii baada ya kuona ajira moja aliyotangaza ni jinsi gani ilivyoshambuliwa kwa maombi elfu
 
Gavana alisema kuwa ingawa lengo la serikali ni kwa uchumi kukua kwa asilimia 7.1 mwaka huu, kuna uwezekano kuwa lengo hilo lisifikiwe kutokana na hofu ya ukame na kupanda kwa bei ya mafuta kwenye soko la dunia.
SASA HIVI VISINGIZIO VIMEKUWA VINGI LAKINI KWA KWELI HAKUNA UBISHI UCHUMI UNAYUMBA

Huyu Gavana nae naona anakuwa mwanasiasa, Gavana wa benki kuu hatakiwi kuwa partisan. Mbona hasemi ukweli kuwa tatizo kubwa kwa uchumi wetu ni serikali kukunbatiA WALA rushwa NA mafisadi AMBAO NDIO WAMELETA MATATIZO YOTE TUNAYOPATA YA UHABA WA UMEME; SHARTI MIKATABA YA UMEME ISINGEJAA WIZI NA UBADHIRIFU LEO HII TUSINGEKUWA NA NGAO WA UMEME NA VIWANDA VISINGEKUWA VINAZALISHA BELOW CAPACITY NA VINGINE KUFUNGWA KABISA HIVYO KUATHIRI UKUAJI WA UCHUMI WA TAIFA NA PIA KUONGEZA UNENPLOYMENT NCHINI!!
 
Hv vp kuhusu kisima cha songas hakipona tuu au ndo uvundo wenyewe unaendelea? Nyie waacheni tu cha kwanza ni ku impose no fly zone halafu baada ya hapo tutajijua na baadaye tulisha kata tamaa lolote lawezekana wasidhani bado tu wapuuuuuva. wasije vuta shuka kumekucha hebu uvumilivu wao uishe ili wajue sisi tulisha kufa ganzi?
 
Wacha vijana waingia kwenye maandamano 5 years ago I was a lone voice nikiwapiga vita wageni kupendelewa na kuchukua kazi ambazo zinaweza kufanywa na Watanzania hivi sasa sioni ajabu kwa nini wanagutuka. Wamechelewa wanavuta shuka wakati jogoo amewika khe khe khe khe kheeeeeeeeeeeeeeeeeee na bado hilo jinamizi la EAC likiingia vizuri ndio watajua zipi ni mbivu.

Wakati wa SA wakiwatoa baru wazimbanwe niliwaona wabaguziiiii lkn sasa sitokuwa na hofu kuwa kaburu kwa muda kwa ajili ya kizazi kijacho na sioni sababu ya kuwa mpofushwa na kauli ya amani na utulivu kumbe wakati mwingine ni kweli kujisacrifice kwa manufaa mema ya wajao????????
 


"Vijana wengi maeneo ya mijini na kwenye vyuo vikuu wanaichukia sana CCM na serikali kutokana na hali ngumu ya uchumi na ukosefu wa ajira. Ndiyo maana wapinzani wameonekana kuwa na nguvu kwenye miji mikubwa hapa nchini," alisema kada mmoja wa CCM.

Wadadisi wa masuala ya kisiasa wamesema kuwa ufisadi serikalini, ukosefu wa ajira na ukali wa maisha vimechangia kwa kiasi kikubwa kukisaidia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kujizolea umaarufu miongoni mwa Watanzania, wengi wao wakiwa ni vijana.

(Source: KULIKONI Toleo la Machi 4, 2011)


Uongo mkubwa.

CCM wameshinda a thunderous landslide unatuambia "wapinzani wamejizolea umaarufu"? Ridiculous.
 
Kwanini Ndulu anajua hayo matatizo wakati Rais wake hayajui!!?
 
Back
Top Bottom