Gang Chomba
JF-Expert Member
- Feb 29, 2008
- 20,301
- 4,681
Magoli mawili ya kiungo mshereheshaji anayeaminika kucheza kandanda toka Mbinguni na pia inaaminika kuwa awapo uwanjani basi shughuli zote huko mbinguni husimama Ronaldo De Assis Moreirra al maaruf kama Ronaldinho Dinho the Saint ama Dinho Gaucho yameisaidia klabu yenye mafanikio zaidi duniani yaani Assozionale di Calcio Milan kuibuka na ushindi wa magoli matatu dhidi ya wajukuu wa bibi Laverchia Signora yaani Juventus.
Katika mechi hiyo ya mwisho ktk msimu huu wa ligi ya serie A tulishuhudia timu ya juve ikikubali kulambwa goli 3-0 dhidi ya AC Milan katika uwanja wa Sansiro Meazza hapa Milan.
Goli la kwanza la Milan liliwekwa kimiani na Beki chipukizi Luka Antonini kabla ya mtakatifu Gaucho kuja kumalizia magoli mawili ambayo ni mpasho na msuto kwa Kocha wa Brazil Dungayembe ambaye amejichumia dhambi kwa kuacha kumjumuisha mtakatifu ktk kikosi kinachotaraji kuja Bondeni hivi karibuni.
katika mechi hiyo saint Gaucho aliitumia kwa kuisaidia Milan kupata ushindi na kutambuliza aina mpya ya chenga na skills ambazo hazijapata kuonekana hapa duniani.
Pia Katika mechi hiyo Milan pia walimuaga rasmi kocha wao Leonaldo baada ya kuitumikia klabu hiyo kwa takriban miaka 13 akiwa kama mchezaji, kiongozi na kocha.
Kwa niaba ya washabiki wa AC Milan waliopo ktk nchi hii iliyojaa ufisadi na kuogopana napenda kumshukuru Leo kwa yoote mema aliyotutendea, na kama kutakuwa na mapungufu basi tunamwomba atusamehe, kwani yoote yalitokea ktk hali ya ubinaadamu.
Forza Milan.
Sempre Dinho.
Katika mechi hiyo ya mwisho ktk msimu huu wa ligi ya serie A tulishuhudia timu ya juve ikikubali kulambwa goli 3-0 dhidi ya AC Milan katika uwanja wa Sansiro Meazza hapa Milan.
Goli la kwanza la Milan liliwekwa kimiani na Beki chipukizi Luka Antonini kabla ya mtakatifu Gaucho kuja kumalizia magoli mawili ambayo ni mpasho na msuto kwa Kocha wa Brazil Dungayembe ambaye amejichumia dhambi kwa kuacha kumjumuisha mtakatifu ktk kikosi kinachotaraji kuja Bondeni hivi karibuni.
katika mechi hiyo saint Gaucho aliitumia kwa kuisaidia Milan kupata ushindi na kutambuliza aina mpya ya chenga na skills ambazo hazijapata kuonekana hapa duniani.
Pia Katika mechi hiyo Milan pia walimuaga rasmi kocha wao Leonaldo baada ya kuitumikia klabu hiyo kwa takriban miaka 13 akiwa kama mchezaji, kiongozi na kocha.
Kwa niaba ya washabiki wa AC Milan waliopo ktk nchi hii iliyojaa ufisadi na kuogopana napenda kumshukuru Leo kwa yoote mema aliyotutendea, na kama kutakuwa na mapungufu basi tunamwomba atusamehe, kwani yoote yalitokea ktk hali ya ubinaadamu.
Forza Milan.
Sempre Dinho.