Je gari zenye cc 660 (mfano: Mitsubishi pajero mini, suzuki kei, suzuki carry, suzuki alto, suzuki jimny, daihatsu mira, daihatsu miragino) zinaweza tembea safari ya kilomita 500-1000 kwa siku moja? Zinaweza kupanda milima au zinachemsha njiani?
Yanin ununue gari ya cc ndogo namna hyo? Jikakamue hadi 2500cc turbo charger!
Aaaah unaenda nayo vizuri tu ukiiandaa kwa safari(Service); mie nna swahiba wangu anayo Suzuki ile kama ki hiace ipo kama boflo hivi anapiga nacho Arusha wakati wowote akitaka na mwendo ni wa hatari (anacheza Speed ni 120 kwa 140) hadi anatamani kukopa.
Hanyanyasiki barabarani naye anawachapa raba kama yupo na VX vile.
Na hivi sasa yupo nako Singida huko kwao.
Aaaah unaenda nayo vizuri tu ukiiandaa kwa safari(Service); mie nna swahiba wangu anayo Suzuki ile kama ki hiace ipo kama boflo hivi anapiga nacho Arusha wakati wowote akitaka na mwendo ni wa hatari (anacheza Speed ni 120 kwa 140) hadi anatamani kukopa.
Hanyanyasiki barabarani naye anawachapa raba kama yupo na VX vile.
Na hivi sasa yupo nako Singida huko kwao.
Iga Ufe!!
Hahahahahahah. thanx for makin me laugh loud and all ma stresses are released nw
Dah vyema sasa unanlindaje?
Acha woga wewe, kifo kipo tu ikitokea ndo siku tarajiwa itakua ishafika"
Baadhi ya vijana wa siku hizi siwaelewi!! "Wanaweka maisha rehani kirahisi tu" ukimuuliza aliyetengeneza hizo gari haku-design kwa shurba kama hizo na ndio maana leo hii taifa letu linaongoza kwa ajali za barabarani katika ukanda huu, hii ni aibu.
Likes mbili hapo juu zinakutosha, ngoja niende nkajisaidie narudi dakika 0