Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,316
- 33,112
Na Imelda Mtema
Gari la mcheza filamu hot Bongo, Jacqueline Wolper Masawe limefumwa likiwa na kondom za aina mbalimbali.
Ishu hiyo ilidakwa na Weekly Exclusive Star, Jumanne ya wiki hii nyakati za mchana wakati msanii huyo akiwa katika mishemishe zake za kila siku.
Mwenyewe alipobanwa na paparazi wetu kuhusiana na ishu hiyo, alikiri mipira hiyo ya kiume ni yake na kwamba, ndiyo silaha kubwa kuliko yoyote hapa duniani, hivyo lazima awe nayo popote.
Staa huyo ambaye kwa sasa yuko kwenye muonekano wa ki-Amber Rose, alikwenda mbele zaidi kwa kuweka wazi kwamba katika ulimwengu huu kondom ni kitu cha kawaida sana.
Ni bora kutembea na kondom ndani ya gari kuliko pesa kwa sababu zana hiyo ndiyo uhai wa mtu na kwa ulimwengu huu ni kitu muhimu.
Unajua wengi wanaamini pesa ndiyo kitu muhimu, lakini kondom ndiyo silaha bora kuliko zote. Kwa kweli mimi kwenye gari langu lazima ziwepo, alisema.
Msanii huyo aliongeza kwamba hata kama yupo na mtu wake faragha na amesahau kifaa hicho, yeye hutoa na kumkabidhi akimwambia: Baba usipate tabu, kwa vile nakupenda nakulinda.
Aidha, amewaomba wasanii wenzake (Aunt, Shumileta, Odama, Shamsa Ford na wengine), waige mfano wake kwa kuwa silaha hiyo hata kwenye pochi inakaa.