Elections 2010 Gari la Mrema lavunjwa kioo na wafuasi wa CCM

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,271
47,271
MGOMBEA ubunge wa jimbo la Vunjo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labour (TLP), Agustine Mrema, amenusurika kupata kipigo kutoka kwa kundi la vijana wanaodaiwa kuwa ni wafuasi wa Chama cha Mapinduzi (CCM).

Mbali ya Mrema kunusurika katika tukio hilo, gari lake liliharibiwa vibaya kwa kupigwa mawe hadi kioo chote cha mbele kupasuliwa na yeye kunusurika.

Tukio hilo, ambalo lilikuwa kama mchezo wa kuigiza, lilitokea juzi eneo la njia panda ya Himo, wakati Mrema alipokuwa akipita barabara kuu iendayo Dar es Salaam karibu na eneo ambalo mgombea ubunge wa CCM, Crispin Meela, alikuwa akifanya mkutano wa kampeni za kuomba kura kwa wapiga kura wake.


Mrema, aliwaambia waandishi wa habari kuwa katika tukio hilo, yeye hakujeruhiwa, lakini gari lake aina ya Toyota Land Cruizer lenye namba za usajili T 317 ALK lilivunjwa vibaya.

"Mimi nimesurika kupata kipigo, lakini gari langu limeharibiwa vibaya, kioo chote cha mbele kimevunjwa na kundi la watu wanaosadikiwa kuwa ni wafuasi wa CCM," alisema Mrema.

Alisema tayari amefungua kesi katika kituo cha polisi Himo, yenye nambari HI/RB/2979/2010 akimshtaki mwana CCM Humphrey Njau maarufu kwa jina la Rasta ambaye anadai alimtambua wakati wa vurugu hizo.


Mrema, alisema tukio hilo lilitokea majira ya saa 11.50 jioni, wakati akitokea kijiji cha Lole, kata ya Mwika Kaskazini, akiwa ameongozana na gari lake la matangazo, lakini alipofika njia panda ambako ndiko yalipo makazi yake, aliona wananchi waliokuwa kwenye mkutano wa CCM wakianza kumshangilia, ghafla akatokea Rasta akarusha jiwe likapasua kioo.


"Njia panda hakuna uwanja wa kufanya mkutano wa kampeni, pale ni maduka ya watu ya biashara, sasa CCM wameona watu hawawafuati kwenye viwanja vya mikutano wameamua kuja kujibanza pembeni ya nyumba zao na kufanya mikutano, huku ni kuwasumbua wananchi kwenye biashara wanazoziendesha kwa mujibu wa sheria za nchi," alisema Mrema.


"Kwa kweli ni hatari jana (juzi) nilikuwa niuawe na CCM huku Vunjo, baada ya kuona wanazidiwa wameamua kutumia vurugu," alisema Mrema.


Kutokana na hali hiyo, Mrema amelihimiza Jeshi la Polisi kuchukua tahadhari ya kujipanga vizuri ili kukabiliana na fujo zisizokuwa za lazima. Kwa siku za hivi karibuni Mrema anadaiwa kuwa mstari wa mbele kumpigia debe mgombea urais wa CCM Jakaya Kikwete.


Akionyesha hali hiyo, hata alipoalikwa kwenye Mkutano Mkuu mkoani Dodoma, Mrema hakuficha hisia zake pale aliposimama na kucheza muziki uliokuwa ukiporomoshwa na kundi la Sanaa la Tanzania One Theatre (TOT).


Juhudi za kumpata Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro, Lucas Ng'ohoboko, kuzungumzia tukio hilo, ziligonga mwamba kutokana na simu zake za kiganjani kuita bila kupokelewa muda.

Hili ni tukio la kwanza kutokea tangu kivumbi cha kampeni kilipoanza Agosti 21 mwaka huu.
 
MGOMBEA ubunge wa jimbo la Vunjo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labour (TLP), Agustine Mrema, amenusurika kupata kipigo kutoka kwa kundi la vijana wanaodaiwa kuwa ni wafuasi wa Chama cha Mapinduzi (CCM).


Mbali ya Mrema kunusurika katika tukio hilo, gari lake liliharibiwa vibaya kwa kupigwa mawe hadi kioo chote cha mbele kupasuliwa na yeye kunusurika.

Tukio hilo, ambalo lilikuwa kama mchezo wa kuigiza, lilitokea juzi eneo la njia panda ya Himo, wakati Mrema alipokuwa akipita barabara kuu iendayo Dar es Salaam karibu na eneo ambalo mgombea ubunge wa CCM, Crispin Meela, alikuwa akifanya mkutano wa kampeni za kuomba kura kwa wapiga kura wake.

Mrema, aliwaambia waandishi wa habari kuwa katika tukio hilo, yeye hakujeruhiwa, lakini gari lake aina ya Toyota Land Cruizer lenye namba za usajili T 317 ALK lilivunjwa vibaya.
"Mimi nimesurika kupata kipigo, lakini gari langu limeharibiwa vibaya, kioo chote cha mbele kimevunjwa na kundi la watu wanaosadikiwa kuwa ni wafuasi wa CCM," alisema Mrema.

Alisema tayari amefungua kesi katika kituo cha polisi Himo, yenye nambari HI/RB/2979/2010 akimshtaki mwana CCM Humphrey Njau maarufu kwa jina la Rasta ambaye anadai alimtambua wakati wa vurugu hizo.

Mrema, alisema tukio hilo lilitokea majira ya saa 11.50 jioni, wakati akitokea kijiji cha Lole, kata ya Mwika Kaskazini, akiwa ameongozana na gari lake la matangazo, lakini alipofika njia panda ambako ndiko yalipo makazi yake, aliona wananchi waliokuwa kwenye mkutano wa CCM wakianza kumshangilia, ghafla akatokea Rasta akarusha jiwe likapasua kioo.

"Njia panda hakuna uwanja wa kufanya mkutano wa kampeni, pale ni maduka ya watu ya biashara, sasa CCM wameona watu hawawafuati kwenye viwanja vya mikutano wameamua kuja kujibanza pembeni ya nyumba zao na kufanya mikutano, huku ni kuwasumbua wananchi kwenye biashara wanazoziendesha kwa mujibu wa sheria za nchi," alisema Mrema.

"Kwa kweli ni hatari jana (juzi) nilikuwa niuawe na CCM huku Vunjo, baada ya kuona wanazidiwa wameamua kutumia vurugu," alisema Mrema.

Kutokana na hali hiyo, Mrema amelihimiza Jeshi la Polisi kuchukua tahadhari ya kujipanga vizuri ili kukabiliana na fujo zisizokuwa za lazima. Kwa siku za hivi karibuni Mrema anadaiwa kuwa mstari wa mbele kumpigia debe mgombea urais wa CCM Jakaya Kikwete.

Akionyesha hali hiyo, hata alipoalikwa kwenye Mkutano Mkuu mkoani Dodoma, Mrema hakuficha hisia zake pale aliposimama na kucheza muziki uliokuwa ukiporomoshwa na kundi la Sanaa la Tanzania One Theatre (TOT).

Juhudi za kumpata Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro, Lucas Ng'ohoboko, kuzungumzia tukio hilo, ziligonga mwamba kutokana na simu zake za kiganjani kuita bila kupokelewa muda.
Hili ni tukio la kwanza kutokea tangu kivumbi cha kampeni kilipoanza Agosti 21 mwaka huu.

Inahusu??Karibu Tandale
 
Nampongeza sana huyo Rasta na kumlaumu kwa nini hakulenga vizuri, Mrema kavuna nusu ya anachostahili, dawa ya msaliti, ndumilakuwili mwenye kutumia ujinga wa watanzania wapiga kura kama mtaji ndio hiyo. Hilo ni onyo kwa wakina mrema wote sasa Rasta kafungua mlango, kumekucha uchaguzi kabla ya kuwashughulikia ndumilakuwili wa aina ya mrema hauwezekani, Hongereni wana vunjo kwa kuwakilisha hasira za wengi tunaonyanyaswa na kunyimwa haki na the likes of Mrema.
 
Nampongeza sana huyo Rasta na kumlaumu kwa nini hakulenga vizuri...
Mkuu vipi wewe, unapongeza uhalifu...hata vipi Mrema ni mwananchi, binaadamu kama wengine kwa kosa lipi kubwa ahujumiwe na uhai wake kuhatarishwa, haya si mambo ya kupongeza ni ujinga...tu.
 
Mrema, Mtikila na Mbatia naona kama vile wanastahili kulengwa mawe vizuri kabisa kwasababu mara nyingi maamuzi yao na vyama vyao yanawakatisha tamaa sana Watanzania katika harakati za kuutafuta ukombozi wa kweli .
 
MGOMBEA ubunge wa jimbo la Vunjo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labour (TLP), Agustine Mrema, amenusurika kupata kipigo kutoka kwa kundi la vijana wanaodaiwa kuwa ni wafuasi wa Chama cha Mapinduzi (CCM).


Mbali ya Mrema kunusurika katika tukio hilo, gari lake liliharibiwa vibaya kwa kupigwa mawe hadi kioo chote cha mbele kupasuliwa na yeye kunusurika.

Tukio hilo, ambalo lilikuwa kama mchezo wa kuigiza, lilitokea juzi eneo la njia panda ya Himo, wakati Mrema alipokuwa akipita barabara kuu iendayo Dar es Salaam karibu na eneo ambalo mgombea ubunge wa CCM, Crispin Meela, alikuwa akifanya mkutano wa kampeni za kuomba kura kwa wapiga kura wake.

Mrema, aliwaambia waandishi wa habari kuwa katika tukio hilo, yeye hakujeruhiwa, lakini gari lake aina ya Toyota Land Cruizer lenye namba za usajili T 317 ALK lilivunjwa vibaya.
“Mimi nimesurika kupata kipigo, lakini gari langu limeharibiwa vibaya, kioo chote cha mbele kimevunjwa na kundi la watu wanaosadikiwa kuwa ni wafuasi wa CCM,” alisema Mrema.

Alisema tayari amefungua kesi katika kituo cha polisi Himo, yenye nambari HI/RB/2979/2010 akimshtaki mwana CCM Humphrey Njau maarufu kwa jina la Rasta ambaye anadai alimtambua wakati wa vurugu hizo.

Mrema, alisema tukio hilo lilitokea majira ya saa 11.50 jioni, wakati akitokea kijiji cha Lole, kata ya Mwika Kaskazini, akiwa ameongozana na gari lake la matangazo, lakini alipofika njia panda ambako ndiko yalipo makazi yake, aliona wananchi waliokuwa kwenye mkutano wa CCM wakianza kumshangilia, ghafla akatokea Rasta akarusha jiwe likapasua kioo.

“Njia panda hakuna uwanja wa kufanya mkutano wa kampeni, pale ni maduka ya watu ya biashara, sasa CCM wameona watu hawawafuati kwenye viwanja vya mikutano wameamua kuja kujibanza pembeni ya nyumba zao na kufanya mikutano, huku ni kuwasumbua wananchi kwenye biashara wanazoziendesha kwa mujibu wa sheria za nchi,” alisema Mrema.

“Kwa kweli ni hatari jana (juzi) nilikuwa niuawe na CCM huku Vunjo, baada ya kuona wanazidiwa wameamua kutumia vurugu,” alisema Mrema.

Kutokana na hali hiyo, Mrema amelihimiza Jeshi la Polisi kuchukua tahadhari ya kujipanga vizuri ili kukabiliana na fujo zisizokuwa za lazima. Kwa siku za hivi karibuni Mrema anadaiwa kuwa mstari wa mbele kumpigia debe mgombea urais wa CCM Jakaya Kikwete.

Akionyesha hali hiyo, hata alipoalikwa kwenye Mkutano Mkuu mkoani Dodoma, Mrema hakuficha hisia zake pale aliposimama na kucheza muziki uliokuwa ukiporomoshwa na kundi la Sanaa la Tanzania One Theatre (TOT).

Juhudi za kumpata Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro, Lucas Ng’ohoboko, kuzungumzia tukio hilo, ziligonga mwamba kutokana na simu zake za kiganjani kuita bila kupokelewa muda.
Hili ni tukio la kwanza kutokea tangu kivumbi cha kampeni kilipoanza Agosti 21 mwaka huu.

Huyo Meela ajiangalie la sivyo hivyo vijisenti alivyotoka navyo NSSF vitamuishia na akishindwa ubunge hawezi tena kurejea NSSF.
 
Sielewi taswila ya hilo tukio,

Ivi mtu akipita mahali ambako kuna mkutano nae anaenda zake kwa mkutano wake yakupasa nin kuanzisha fujo?? si umwache aendezake hata kama ali hasi chama chenu ya nini umtupie mawe je ingalikuwa ni wewe ccm ungeitoa mpaka sijui BBC, jamani kumbukeni at the end of this wote tutakuwa pammoja jamani na sijui mtazificha sura zenu wapi? na mbaya zaidi yeye awe mbunge si mtauhama mji kwa kumwogopa mbunge wenu atakaye shinda??

Tukio hili sio jema na halistahiri kutokea popote kule ndani ya nchi hii. nadhani kuna vyombo vya sheria vichukue hatua.
 
Sielewi taswila ya hilo tukio,

Ivi mtu akipita mahali ambako kuna mkutano nae anaenda zake kwa mkutano wake yakupasa nin kuanzisha fujo?? si umwache aendezake hata kama ali hasi chama chenu ya nini umtupie mawe je ingalikuwa ni wewe ccm ungeitoa mpaka sijui BBC, jamani kumbukeni at the end of this wote tutakuwa pammoja jamani na sijui mtazificha sura zenu wapi? na mbaya zaidi yeye awe mbunge si mtauhama mji kwa kumwogopa mbunge wenu atakaye shinda??

Tukio hili sio jema na halistahiri kutokea popote kule ndani ya nchi hii. nadhani kuna vyombo vya sheria vichukue hatua.


kwa kweli u er right guy. tuwe wapenda demokrasia, tushindane ila tusipigane
 
CCM wanawafanyia noma hadi wenzao wa CCM "B"? Kweli hawana jema
MGOMBEA ubunge wa jimbo la Vunjo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labour (TLP), Agustine Mrema, amenusurika kupata kipigo kutoka kwa kundi la vijana wanaodaiwa kuwa ni wafuasi wa Chama cha Mapinduzi (CCM).

Mbali ya Mrema kunusurika katika tukio hilo, gari lake liliharibiwa vibaya kwa kupigwa mawe hadi kioo chote cha mbele kupasuliwa na yeye kunusurika.

Tukio hilo, ambalo lilikuwa kama mchezo wa kuigiza, lilitokea juzi eneo la njia panda ya Himo, wakati Mrema alipokuwa akipita barabara kuu iendayo Dar es Salaam karibu na eneo ambalo mgombea ubunge wa CCM, Crispin Meela, alikuwa akifanya mkutano wa kampeni za kuomba kura kwa wapiga kura wake.


Mrema, aliwaambia waandishi wa habari kuwa katika tukio hilo, yeye hakujeruhiwa, lakini gari lake aina ya Toyota Land Cruizer lenye namba za usajili T 317 ALK lilivunjwa vibaya.

"Mimi nimesurika kupata kipigo, lakini gari langu limeharibiwa vibaya, kioo chote cha mbele kimevunjwa na kundi la watu wanaosadikiwa kuwa ni wafuasi wa CCM," alisema Mrema.

Alisema tayari amefungua kesi katika kituo cha polisi Himo, yenye nambari HI/RB/2979/2010 akimshtaki mwana CCM Humphrey Njau maarufu kwa jina la Rasta ambaye anadai alimtambua wakati wa vurugu hizo.


Mrema, alisema tukio hilo lilitokea majira ya saa 11.50 jioni, wakati akitokea kijiji cha Lole, kata ya Mwika Kaskazini, akiwa ameongozana na gari lake la matangazo, lakini alipofika njia panda ambako ndiko yalipo makazi yake, aliona wananchi waliokuwa kwenye mkutano wa CCM wakianza kumshangilia, ghafla akatokea Rasta akarusha jiwe likapasua kioo.


"Njia panda hakuna uwanja wa kufanya mkutano wa kampeni, pale ni maduka ya watu ya biashara, sasa CCM wameona watu hawawafuati kwenye viwanja vya mikutano wameamua kuja kujibanza pembeni ya nyumba zao na kufanya mikutano, huku ni kuwasumbua wananchi kwenye biashara wanazoziendesha kwa mujibu wa sheria za nchi," alisema Mrema.


"Kwa kweli ni hatari jana (juzi) nilikuwa niuawe na CCM huku Vunjo, baada ya kuona wanazidiwa wameamua kutumia vurugu," alisema Mrema.


Kutokana na hali hiyo, Mrema amelihimiza Jeshi la Polisi kuchukua tahadhari ya kujipanga vizuri ili kukabiliana na fujo zisizokuwa za lazima. Kwa siku za hivi karibuni Mrema anadaiwa kuwa mstari wa mbele kumpigia debe mgombea urais wa CCM Jakaya Kikwete.


Akionyesha hali hiyo, hata alipoalikwa kwenye Mkutano Mkuu mkoani Dodoma, Mrema hakuficha hisia zake pale aliposimama na kucheza muziki uliokuwa ukiporomoshwa na kundi la Sanaa la Tanzania One Theatre (TOT).


Juhudi za kumpata Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro, Lucas Ng'ohoboko, kuzungumzia tukio hilo, ziligonga mwamba kutokana na simu zake za kiganjani kuita bila kupokelewa muda.

Hili ni tukio la kwanza kutokea tangu kivumbi cha kampeni kilipoanza Agosti 21 mwaka huu.
 
hongera rasta kwa kumshughulikia mnafki wa siasa,naona haitoshi itabidi mumshughulikie zaidi
 
CCM ndio chanzo cha fujo siku zote. Hii inatokana na kuwa kila jimbo ambalo upinzani unanguvu lazima zionekane fujo kutokea. Jamaa huwa hawakubali kushindwa.
 
CCM kumfanyia fujo Mrema A L ni dalili za kushindwa kabla ya wananchi wa Vunjo kutoa hukumu yao October 2010.Kuna kila dalili CCM italipoteza jimbo la Vunjo nafasi ya ubunge na madiwani wanahaha na kutafuta kila njia hata haramu ili mgombea wao asiekuwa na mvuto kwa wapiga kura ashinde lakini kila siku ndyo anazidi kuporomoka kisiasa na kiuchumi.

Wakuu pia nimeshangaa kusikia baadhi ya watu wanashabikia fujo kwakuwa hawampendi Mrema wanadhani anastahili kutendewa mambo ya kihuni nadhani huu si ustaharabu hakika kila raia wa nchi yetu anahaki ya kulindwa yeye na mali zake.waliohusika kumfanyia Mrema fujo wanastahili kuchukuliwa hatua kali za kisheria.
 
Hao wanaoshabikia uhuni nao ni wahuni kwani kwa vyovyote vile uhuni na uvunjaji wa amani ni vitu vya kukemea. huyo rasta ashughulikiwe na vyombo husika...tusiache kampeni zichukue sura hiyo kwani leo akianza Mrema kesho atafuata nani? hao wahuni hawakubaliki kwenye jamii ya wastaarabu.Kampeni ziwe za kistaarabu hata kama aliasi,mbona Dr.Slaa ameasi kanisa na anatetewa iweje mrema? watu wanaasi ndoa na makubaliano kibao wanayoweka mbona hawafanyiwi fujo hizo. TUSTAARABIKE
 
Mkuu vipi wewe, unapongeza uhalifu...hata vipi Mrema ni mwananchi, binaadamu kama wengine kwa kosa lipi kubwa ahujumiwe na uhai wake kuhatarishwa, haya si mambo ya kupongeza ni ujinga...tu.
Hata Saddam alikuwa binadamu kama wengine lakini alinyongwa na je Chemical Ali aliyeuwa wa Kurd laki tano kwa sumu utamwonea huruma, ubinadamu unaendana na vitendo.
 
Hata Saddam alikuwa binadamu kama wengine lakini alinyongwa na je Chemical Ali aliyeuwa wa Kurd laki tano kwa sumu utamwonea huruma, ubinadamu unaendana na vitendo.

sidhani kama atakuelewa kirahisi hivyo
 
big up mbunge wangu mtarajiwa.

kiukweli nampenda sana mrema kwa kuwa anaweza kufanya kazi nzuri akipewa uongozi.mathalani ni mtu jasiri sana na ameweza kupata cheo ambacho hakuna mtanzania anaweza kukipata tena.
mzee endelea kupambana urudishe jimbo kwako maana 1995 ulimpa mbatia mwaka 2010 ukamkabithi makundi sasa wewe lichukue tena.ingawa natambua kuwa vijana wengi tupo huku mjini wazeee wetu na mama zetu watakupa kura nyingi kwa kuwa wanatambua mchango wako katika kukuza soko la kahawa na pia katika kukomesha gender based violance na ulinzi wa sungusungu ulipokuwa waziri.

Mungu akujalie Afya njema.
 
MGOMBEA ubunge wa jimbo la Vunjo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labour (TLP), Agustine Mrema, amenusurika kupata kipigo kutoka kwa kundi la vijana wanaodaiwa kuwa ni wafuasi wa Chama cha Mapinduzi (CCM).

Mbali ya Mrema kunusurika katika tukio hilo, gari lake liliharibiwa vibaya kwa kupigwa mawe hadi kioo chote cha mbele kupasuliwa na yeye kunusurika.

Tukio hilo, ambalo lilikuwa kama mchezo wa kuigiza, lilitokea juzi eneo la njia panda ya Himo, wakati Mrema alipokuwa akipita barabara kuu iendayo Dar es Salaam karibu na eneo ambalo mgombea ubunge wa CCM, Crispin Meela, alikuwa akifanya mkutano wa kampeni za kuomba kura kwa wapiga kura wake.

Mrema, aliwaambia waandishi wa habari kuwa katika tukio hilo, yeye hakujeruhiwa, lakini gari lake aina ya Toyota Land Cruizer lenye namba za usajili T 317 ALK lilivunjwa vibaya.
“Mimi nimesurika kupata kipigo, lakini gari langu limeharibiwa vibaya, kioo chote cha mbele kimevunjwa na kundi la watu wanaosadikiwa kuwa ni wafuasi wa CCM,” alisema Mrema.

Alisema tayari amefungua kesi katika kituo cha polisi Himo, yenye nambari HI/RB/2979/2010 akimshtaki mwana CCM Humphrey Njau maarufu kwa jina la Rasta ambaye anadai alimtambua wakati wa vurugu hizo.

Mrema, alisema tukio hilo lilitokea majira ya saa 11.50 jioni, wakati akitokea kijiji cha Lole, kata ya Mwika Kaskazini, akiwa ameongozana na gari lake la matangazo, lakini alipofika njia panda ambako ndiko yalipo makazi yake, aliona wananchi waliokuwa kwenye mkutano wa CCM wakianza kumshangilia, ghafla akatokea Rasta akarusha jiwe likapasua kioo.

“Njia panda hakuna uwanja wa kufanya mkutano wa kampeni, pale ni maduka ya watu ya biashara, sasa CCM wameona watu hawawafuati kwenye viwanja vya mikutano wameamua kuja kujibanza pembeni ya nyumba zao na kufanya mikutano, huku ni kuwasumbua wananchi kwenye biashara wanazoziendesha kwa mujibu wa sheria za nchi,” alisema Mrema.

“Kwa kweli ni hatari jana (juzi) nilikuwa niuawe na CCM huku Vunjo, baada ya kuona wanazidiwa wameamua kutumia vurugu,” alisema Mrema.

Kutokana na hali hiyo, Mrema amelihimiza Jeshi la Polisi kuchukua tahadhari ya kujipanga vizuri ili kukabiliana na fujo zisizokuwa za lazima. Kwa siku za hivi karibuni Mrema anadaiwa kuwa mstari wa mbele kumpigia debe mgombea urais wa CCM Jakaya Kikwete.

Akionyesha hali hiyo, hata alipoalikwa kwenye Mkutano Mkuu mkoani Dodoma, Mrema hakuficha hisia zake pale aliposimama na kucheza muziki uliokuwa ukiporomoshwa na kundi la Sanaa la Tanzania One Theatre (TOT).

Juhudi za kumpata Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro, Lucas Ng’ohoboko, kuzungumzia tukio hilo, ziligonga mwamba kutokana na simu zake za kiganjani kuita bila kupokelewa muda.
Hili ni tukio la kwanza kutokea tangu kivumbi cha kampeni kilipoanza Agosti 21 mwaka huu.

Walishampa pesa za matibabu Kizota, ilikua kama laki mbili na sabini.....
 
Back
Top Bottom