Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,266
- 33,039
Msemaji wa Chama Cha Jamii (CCJ), Fred Mpendazoe.
Polisi katika kituo cha Karume jijini Dar es Salaam, imelikamata na kulishikilia kwa muda, msemaji wa Chama Cha Jamii (CCJ), Fred Mpendazoe.
Gari hilo lenye namba T 776 BAE, aina ya Corolla, lilishikiliwa jana kwa takribani saa sita, kwa madai kuwa kibali cha kuendesha kilikuwa kimeisha.
Wakati gari hilo likikamatwa, lilikuwa linaendeshwa na dereva wake, Vitalis Henzi Mpendazoe, anayesadikiwa kuwa mtoto wa Mpendazoe.
Akizungumza na gazeti hili jana nje ya kituo hicho, mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo, alisema mtoto huyo alikamatwa eneo la Msimbazi Centre, wakati akitokea Kigogo kuelekea Ilala-Boma.
Alisema askari wawili waliokuwa kwenye pikipiki, walilitilia shaka na kuanza kulikagua, ambapo ilibainika bima yake ilikuwa imemalizika muda wa matumizi.
CHANZO: NIPASHE