Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,720
- 21,779
Gari la Mkurugenzi wa NSSF laibwa 'gesti'
Mahija Mpera
GARI la Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Ramadhan Dau, limeibwa, Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam ilisema jana.
Kamanda wa kanda hiyo, Sulemani Kova, aliwaambia waandishi wa habari kuwa gari hilo liliibwa Novemba 10 mwaka huu, jijini Dar es Salaam.
Kova alisema hata hivyo siku iliyofuata, gari hilo lilikamatwa mkoani Kilimanjaro.
Alisema mbali na kukamata gari hilo, polisi pia wamewakamata watu saba wakiongozwa na mwanamke katika wizi huo.
Kwa mujibu wa kamanda huyo, kundi hilo linahusisha pia na wizi wa magari kadhaa nchini.
Kamanda Kova alisema kukamatwa kwa gari hilo kulitokana na taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi huyo mara baada ya kuibiwa.
Alisema kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo wa NSSF, alisema wizi huo ulitokea usiku wa Novemba 10 baada ya majambazi kumvamia dereva wake Yusuf Magogo, mkazi wa Tabara.
Kova alisema hata hivyo uchunguzi wa polisi ulibaini kwamba taarifa hizo za awali hazikuwa sahihi kwa sababu gari hilo liliibwa na mwanamke ambaye aliyekuwa na dereva huyo katika nyumba ya kulala wageni.
"Kuna mwanamke (jina tunalihifadhi kwa sasa) akiwa na dereva wa gari hiyo walikwenda kwenye gesti ya Comfort iliyoko Kinondoni kwa lengo la kufanya mapenzi, wakiwa katika chumba namba 12 mwanamke huyo alimwekea madawa ya kulevya dereva huyo katika kinywaji chake aina ya vitamalta," alisema Kova.
Alisema baada ya kunywa kinywaji hicho, dereva alipoteza fahamu, jambo lilitoa fursa kwa mwanamke huyo kuchukua funguo za gari na za chumba hicho na kutokomea nazo.
Alisema hata hivyo polisi mkoani kilimanjaro kwa kushirikiana na Kampuni ya Cartrack, waliweza kukamata gari hilo katika Kijiji ncha Lyasongoro, likiwa na namba bandia.
Kova alisema Novemba 9 mwaka huu, polisi wa Kikosi cha Maalumu cha Kuzuia Wizi wa Magari, walimkamata mwanamke huyo na kumhoji.
Kwa mujibu wa kamanda huyo, mwanamke huyo alikiri kuhusika na ujambazi huo na kwamba yeye anatumiwa na kijana mmoja.
Katika tukio lingine, polisi wamekamata majambazi sita sugu wakiwa na bunduki aina ya rifle yenye namba AU-160 ikiwa na risasi 19.
Kamnda Kova amesema kwa majambazo hayo yamekiri kuhusika na ujambazi
Mahija Mpera
GARI la Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Ramadhan Dau, limeibwa, Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam ilisema jana.
Kamanda wa kanda hiyo, Sulemani Kova, aliwaambia waandishi wa habari kuwa gari hilo liliibwa Novemba 10 mwaka huu, jijini Dar es Salaam.
Kova alisema hata hivyo siku iliyofuata, gari hilo lilikamatwa mkoani Kilimanjaro.
Alisema mbali na kukamata gari hilo, polisi pia wamewakamata watu saba wakiongozwa na mwanamke katika wizi huo.
Kwa mujibu wa kamanda huyo, kundi hilo linahusisha pia na wizi wa magari kadhaa nchini.
Kamanda Kova alisema kukamatwa kwa gari hilo kulitokana na taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi huyo mara baada ya kuibiwa.
Alisema kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo wa NSSF, alisema wizi huo ulitokea usiku wa Novemba 10 baada ya majambazi kumvamia dereva wake Yusuf Magogo, mkazi wa Tabara.
Kova alisema hata hivyo uchunguzi wa polisi ulibaini kwamba taarifa hizo za awali hazikuwa sahihi kwa sababu gari hilo liliibwa na mwanamke ambaye aliyekuwa na dereva huyo katika nyumba ya kulala wageni.
"Kuna mwanamke (jina tunalihifadhi kwa sasa) akiwa na dereva wa gari hiyo walikwenda kwenye gesti ya Comfort iliyoko Kinondoni kwa lengo la kufanya mapenzi, wakiwa katika chumba namba 12 mwanamke huyo alimwekea madawa ya kulevya dereva huyo katika kinywaji chake aina ya vitamalta," alisema Kova.
Alisema baada ya kunywa kinywaji hicho, dereva alipoteza fahamu, jambo lilitoa fursa kwa mwanamke huyo kuchukua funguo za gari na za chumba hicho na kutokomea nazo.
Alisema hata hivyo polisi mkoani kilimanjaro kwa kushirikiana na Kampuni ya Cartrack, waliweza kukamata gari hilo katika Kijiji ncha Lyasongoro, likiwa na namba bandia.
Kova alisema Novemba 9 mwaka huu, polisi wa Kikosi cha Maalumu cha Kuzuia Wizi wa Magari, walimkamata mwanamke huyo na kumhoji.
Kwa mujibu wa kamanda huyo, mwanamke huyo alikiri kuhusika na ujambazi huo na kwamba yeye anatumiwa na kijana mmoja.
Katika tukio lingine, polisi wamekamata majambazi sita sugu wakiwa na bunduki aina ya rifle yenye namba AU-160 ikiwa na risasi 19.
Kamnda Kova amesema kwa majambazo hayo yamekiri kuhusika na ujambazi