Gaidi ni nani hasa?: Je marekani sasa inakimbia kivuli chake?

Hofstede

JF-Expert Member
Jul 15, 2007
3,577
1,107
Nimekuwa nikifuatilia kwa karibu sana kuhusu mwenendo wa hii vita inayoendeshwa na marekani na washirika wake tangu walipopigwa na ndege za abiria kwenye minara ya kibiashara ya New York na Pentagon september 2001.

Baada ya hapo kumetokea mambo mengi tu kuhusu vita hii wanayoiita ya ugaidi, kama kitendo Shoe Bomber, Anthrax attack, mashambulizi ya mtu aliyejiita mungu aliyenyongwa last year virginia, Mnigeria aliyetaka kujilipua kupia bomb la kwenye pant et al.

Lakini pia kumetokea matukio makuu mawili hivi karibuni ya raia wa marekani kufanya mauaji ya kukusudia
1. Tukio la Forthood Major Nadal Malik la kuua askari wenzake kwa kile kilichodhaniwa kuwa ni upinzani wa vita dhidi ya mataifa aliyosema ni ya kiislamu ( Huyu mtu aliitwa gaidi, islamic terrorist n.k) hasa right wingnuts waliotaka kuonesha kuwa Obama is not making US safe,

2. Tukio jingine ni la juzi juzi ambapo Joe Stack aliamua kuchoma nyumba yake na kujaza ndege mafuta na kuibamiza kwenye jengo la serikali kitendo kilichomuua yeye mwenyewe na mfanyakazi mmoja wa Idara ya kodi. Hapa tuliambiwa kuwa hii ni separate incident na kwamba si shambulio la kigaidi. Hivi sasa kuna mjadala wa kuwa bwana huyu ni shujaa kwa kupinga serikali kumtoza kodi bila kuangalia kuwa kitendo chake kimefanya uharibu wa mali, maisha na kujeruhi raia wasio na hatia. Soma zaidi hapa: http://abcnews.go.com/GMA/joe-stacks-daughter-samantha-bell-calls-dad-hero/story?id=9903329

Swali langu ni: Gaidi ni mtu wa aina gani hasa na hero ni mtu wa aina gani hasa?. Je kuna double standards katika kulebo watu hawa?.

Ni nani Gaidi? ni lazima kuwe na standard moja tu bila kuangalia ethnicity au imani ya mtu. Koleo liitwe Kolea kila wakati na si kuliita kijiko wakati mwingine
 
Let's define terrorism from Western perspectives. According to the Oxford Dictionary, "terrorism is the use of violent action in order to achieve political aims or to force a government to act".

My definition of terrorist is someone who intentionally attacks non-combatants as the intended, rather than accidental, victims for the purpose of creating a politically influential state of terror.

 
Let's define terrorism from Western perspectives. According to the Oxford Dictionary, "terrorism is the use of violent action in order to achieve political aims or to force a government to act".

My definition of terrorist is someone who intentionally attacks non-combatants as the intended, rather than accidental, victims for the purpose of creating a politically influential state of terror.


Nashukuru Mkuu, Kumbe Joe ni gaidi, Nadal ni gaidi kama Osama na kundi lake. Sasa Marekani ianze kuwatafuta wafuasi wa hawa watu, tukianzia na Right wingnuts na binti wa huyu jamaa (Joe Stack), siyo kumtafuta sheikh wa Nadal tu aliyeko Yemen
 
Nashukuru Mkuu, Kumbe Joe ni gaidi, Nadal ni gaidi kama Osama na kundi lake. Sasa Marekani ianze kuwatafuta wafuasi wa hawa watu, tukianzia na Right wingnuts na binti wa huyu jamaa (Joe Stack), siyo kumtafuta sheikh wa Nadal tu aliyeko Yemen

Watafanyaje hayo ndugu unafikiri wanapigana Afghanistani kutafuta magaidi? mistake wao wanatafuta mali na hawajali maisha ya watoto wala wanawake wanaouliwa na majeshi..

Kwangu mimi ni shetani (greedy for power and money) at work! hakuna cha kutafuta magaidi wala nini? magaidi hawatafutwi kwa mabomu bali intelingensia period!
 
Back
Top Bottom