Fuso lenye maiti za kufundishia

WanaJF

1. Taaluma ya medicine ina karne nyingi sana. Utaratibu wa kumfundisha Daktari unaongozwa na kanuni na misingi ya pamoja inayokubalika duniania kote. Kiapo chao cha kazi ni kile kile cha kale dunia nzima. Kama yatakuwepo mabadiliko yanatakiwa yawe ya kimataifa. Kumfunza mtu kwa kutumia miili ya binadamu kuna maana yake kitaaluma na sio suala la kubadili na kutumia njia kama za plastic. Ni science inayoongoza hapa.

2. Taaluma ya medicine inaongozwa na principles na ethics, kwahiyo suala la miili ya binadamu lina taratibu zake zinazoratibiwa na watu wenye weledi wa hali ya juu sana kwa kuzingatia vigezo vyote vya kisayansi ikiwa ni pamoja na kuhifadhili miili hiyo, kuchagua ili kupunguza 'risk' kwa watumiaji, kuzingatia cultural and social behaviour vyote vikiongozwa na principles, Laws, regulations and ethics.

3. Taarifa nyingi za kitaalamu hapa nchini pasipokuwa na professional journalists huwa ima zinapotosha au hazina ukamilifu. Ikumbukwe kuwa afisa uhusiano sio lazima awe mtaalamu wa nyanja hiyo, na waandishi wahabari wengi (nawaheshimu sana na kazi zao) lakini wapo wanaokosa kutafuta vyanzo halisi vya habari. Kama taarifa ingetolewa na mtaalamu husika (mkuu wa chuo, taaluma au mkuu wa hospitali)tungeelewa mengi kuliko kusikia fuso limekamatwa tu na miili.

Yaweza kuwa miili hiyo ilihifadhiwa kwa muda baada ya kupokelewa kutoka sehemu nyingine nje ya nchi na uhamishaji kwenda Dodoma ndio umekuwa na matatizo. Alichosema msemaji ni taratibu za kuzika marehemu siku 14, na sidhani huo ndio utaratibu wa kuaandaa miili ya marehemu ya kufundishia

Kwa misingi hiyo, si haki au vema kuanza kutoa hukumu kwa ujumla wa suala zima, inaweza kuwa ni taarifa tu kwa walinzi ilikosekana kwa makosa lakini taratibu zingine zilizingatiwa.

Nawahakikishieni kuwa kama tulichokisoma ndicho, basi yapo makosa mengi na wahusika watachukuliwa hatua.
Ningeshauri kuwepo na ufafanuzi wa jambo hili kutoka kwa wahusika kwasababu limeitisha jamii kwa namna fulani, na jamii ya wataalamu wa afya wanadhani lipo ombwe la habari au makosa ya kiutendaji kwa kusoma tu habari hii kama ilivyo.
Wanahabari wafuatilie kubaini ukweli kutoka kwa vyanzo husika.

Umemaliza mzozo........nasi tusioelewa haya mambo tumeelewa......thanks..
 
Parapanda,

Madoctor wote ndio wanavyojifunza. Hii miili kwao inaitwa cadaver. Leo hii wewe unatibiwa na daktri bingwa na kushukuru. Sasa ujue ubingwa wao wameupataje.
Si kweli kwamba watu wanaandika kuwa miili ya iwe cadaver, bali huwa wanaridhia kuwa organ donors. Maana yake kama wakifa, basi organs zao kama moyo, maini, etc ziwe donated to someone who needs a transplant.
Na mara nyingi hizi organs huwa "harvested" wakati moyo bado unadunda! Hii nayo isikutishe!
Moyo huwa unakuwa kept pumping by machines hadi pale madaktari mabingwa wakifika ku-harvest hivi viungo. At the same time the recipient huwa anakuwa prepared to receive them.
Kwa wenzetu walioendelea, helicopter huwa inatua juu ya hospital, organs zinawkewa kwenye special machine, zinapelekwa uwanjani kwenye jet. Wakati huo ndege zingine zinasimamishwa hadi hii yo viungo iondoke. Ikifika mji alipo recipient, napo hivyo hivyo. Kwenye helicopter tena, to the hospital and straight to the theatre.

Hila kwenye kujifunza, na wao hutumia miili ya watu ambayo haiko claimed na kuzikwa na serikali.

It is nasty stuff but ndio hali halisi.
 
Pia nijuavyo mimi, maiti za kujifunzia , cadaver, hupaswa kutoka mataifa ya mbali ya watu wasio na uwezekano wowote wa kinasaba na nchi husika, mfano Tanzania inapaswa kuletewa cadaver toka China etc ili wanafunzi wajifunze bila emotional wala remorse, hili la miili ya Dar kupelekwa Dodoma si wanafunzi watakuja kukuta ndugu zao?.

Hapo mkuu nakubaliana na wewe ndio utaratibu uliopo!

Haiwezekani maiti achukuliwe Muhimbili apelekwe Dodoma kwa ajili ya kujifunzia. Maiti wa hivyo wanatoka mataifa mengine kabisaa! Kama hili limefanyika UDOM hapo wamechemka na hiyo hospitali yao. Hebu fikria mko kwenye maabara halafu ndo unakutana na mwili wa Mndamba mwenzio si utazimia? Hii haiwezekani na haikubaliki labda kama hizo maiti walikuwa wanaenda kuzifanyia mambo mengine!!
 
Thanks Dr Ozzie!

"Here is the only place where the dead teaches the living"!
 
Parapanda,

Madoctor wote ndio wanavyojifunza. Hii miili kwao inaitwa cadaver. Leo hii wewe unatibiwa na daktri bingwa na kushukuru. Sasa ujue ubingwa wao wameupataje.
Si kweli kwamba watu wanaandika kuwa miili ya iwe cadaver, bali huwa wanaridhia kuwa organ donors. Maana yake kama wakifa, basi organs zao kama moyo, maini, etc ziwe donated to someone who needs a transplant.
Na mara nyingi hizi organs huwa "harvested" wakati moyo bado unadunda! Hii nayo isikutishe!
Moyo huwa unakuwa kept pumping by machines hadi pale madaktari mabingwa wakifika ku-harvest hivi viungo. At the same time the recipient huwa anakuwa prepared to receive them.
Kwa wenzetu walioendelea, helicopter huwa inatua juu ya hospital, organs zinawkewa kwenye special machine, zinapelekwa uwanjani kwenye jet. Wakati huo ndege zingine zinasimamishwa hadi hii yo viungo iondoke. Ikifika mji alipo recipient, napo hivyo hivyo. Kwenye helicopter tena, to the hospital and straight to the theatre.

Hila kwenye kujifunza, na wao hutumia miili ya watu ambayo haiko claimed na kuzikwa na serikali.

It is nasty stuff but ndio hali halisi.

Asante sana MockingJay kwa maelezo yako. Sipingi madaktari kujifunza kuhusu mwili wa mwanadamu kwa kutumia viungo vyake halisi; ili wafuzu, ni lazima iwe hivyo. Ni kweli jambo hili lina ukakasi kulisikia, lakini ndivyo ilivyo.
Mambo haya hayajulikani kwa watu wengi kwa sababu ni mambo yanayofanywa na watu wenye weledi wa tasnia yaa utabibu, tena faraghani kwenye vyumba vya maiti, lakini kwa manufaa ya tulio hai sasa. Mimi habari hii ilinigusa, ndipo nikaomba kwa yeyote anayejua mambo haya anijuze. Nimepata maelezo mengi ya jumla, na kuna watu wamenitumia movie clips za autopsy, nimeona. Udaktari ni zaidi ya kazi ya mshahara!.
 
madhara ya kuwa na utawala legelege na hii ndo huzaa watu wenyekutoa majibu ya hovyo hovyo kutokana na ulegelege wao...pumbafu kabisa yaani 14 days una declare maiti haina wenyewe..ovyo sana nyie watu
 
jamani, picha nyingine siyo za kuwekwa hadharani. acheni anayetaka kuziona aperuzi mwenyewe. mambo mengine yanatisha jamani, waachieni wenye fani yao!
 
&
Parapanda, <br />
<br />
Madoctor wote ndio wanavyojifunza. Hii miili kwao inaitwa cadaver. Leo hii wewe unatibiwa na daktri bingwa na kushukuru. Sasa ujue ubingwa wao wameupataje.<br />
Si kweli kwamba watu wanaandika kuwa miili ya iwe cadaver, bali huwa wanaridhia kuwa organ donors. Maana yake kama wakifa, basi organs zao kama moyo, maini, etc ziwe donated to someone who needs a transplant.<br />
Na mara nyingi hizi organs huwa &quot;harvested&quot; wakati moyo bado unadunda! Hii nayo isikutishe!<br />
Moyo huwa unakuwa kept pumping by machines hadi pale madaktari mabingwa wakifika ku-harvest hivi viungo. At the same time the recipient huwa anakuwa prepared to receive them. <br /;
Kwa wenzetu walioendelea, helicopter huwa inatua juu ya hospital, organs zinawkewa kwenye special machine, zinapelekwa uwanjani kwenye jet. Wakati huo ndege zingine zinasimamishwa hadi hii yo viungo iondoke. Ikifika mji alipo recipient, napo hivyo hivyo. Kwenye helicopter tena, to the hospital and straight to the theatre.<br />
<br />
Hila kwenye kujifunza, na wao hutumia miili ya watu ambayo haiko claimed na kuzikwa na serikali.<br />
<br />
It is nasty stuff but ndio hali halisi.
<br />
<br />
 
Mimi sio mtu wa taaluma ya tiba isipokuwa nijuavyo kutokana na maelezo ya Wataalamu, miili ya binaadamu kutumika kufundishia ni jambo la kawaida sana. Wengi tumeshangazwa kutokana na taarifa kwenye vyombo vya habari na mazingira yaliyotawala tukio zima. Wengine tutafikiria na kuunganisha na matendo ya kishirikina kama mauaji ya Albino na viungo vyao kunyakuliwa. Kama makosa ya kuchukua hiyo miili yamefanyika basi wahusika warekebishe yasitokee tena, vinginevyo watatukumbusha makosa ya mgonjwa wa mguu kupasuliwa kichwa na wa kichwa kupasuliwa mguu.
 
nadhani afisa uhusiano wa muhimbili amejaribu kuelezea kitu asichokifahamu matokeo yake ameharibu.watanzania hatujui limits zet!
 
Back
Top Bottom