Fungukeni Wanawake wa Tanzania ....!

HorsePower

JF-Expert Member
Aug 22, 2008
3,612
2,566
Kwa muda mrefu sana, wapendwa wetu akina dada wamekuwa wakibanwa na utamaduni wa asili kwa kusubiri kuimbishwa na wakaka. Najaribu kufikiria kuwa, hata kama wao wamempenda mkaka ni ngumu kutamka wazi wazi, na wakijitahidi sana, huishia kuonyesha mapenzi kwa vitendo au kwa kumtega mtu.

Mara nyingi wao wakifunguka huwa inaleta tafsiri isiyo nzuri sana ndani ya jamii wakati kiukweli ilipaswa na wao pia wapate nafasi nzuri ya kumtamkia yule wanayempenda maana ni haki yao kimsingi.

Kwa tamaduni za wenzetu wahindi (sina uhakika kama ni wote), wanawake ndiyo huenda kumpropose mwanaume na hii imekubalika kabisa.

Naomba tuchangie jamani, kuna tatizo gani watanzania wakikubaliana na huu utaratibu wa kugawa fursa sawa kwa wote ikiwemo kuwakubalia na kutokuwatafsiri vibaya wadada wanaofunguka mbele ya wakaka?

Nawasilisha.

HP
 
HP itachukua muda sana kwa hilo kuweza kufanyika
Bado tuna ile dhana kuwa mwanamke akikuambia anakupenda yaani akikuanza wewe lazima ana element za ubaya zaidi
Hata kama atakuwa amevumilia kwa muda mrefu bado dhamira yake na kutoa kile alicho nacho bado inamsuta
Atakufa na tai shingoni akiona mtu anayempenda anatoka anaenda kumpenda dada mwingine
Maana kuna wanaume wengine hata zile signs tuu za kuonyeshwa kuwa anapendwa hazioni wala nini
 
HP itachukua muda sana kwa hilo kuweza kufanyika
Bado tuna ile dhana kuwa mwanamke akikuambia anakupenda yaani akikuanza wewe lazima ana element za ubaya zaidi
Hata kama atakuwa amevumilia kwa muda mrefu bado dhamira yake na kutoa kile alicho nacho bado inamsuta
Atakufa na tai shingoni akiona mtu anayempenda anatoka anaenda kumpenda dada mwingine
Maana kuna wanaume wengine hata zile signs tuu za kuonyeshwa kuwa anapendwa hazioni wala nini

Tufanye nini ili hiyo dhana ya ubaya kwa mwanamke kufunguka iwatoke watu?
 
Tufanye nini ili hiyo dhana ya ubaya kwa mwanamke kufunguka iwatoke watu?

Kukubaliana na dhana kuwa wanawake nao wana nafasi yao kumuapproach mwanaume na wana nafasi sawa ya kudevelop hisia na kumpenda mtu na kuonyesha wazi hisia zao
Sio suala la kusema kuwa wanaume tuu ndo tuanze hata wao wanaweza
 
Kwa muda mrefu sana, wapendwa wetu akina dada wamekuwa wakibanwa na utamaduni wa asili kwa kusubiri kuimbishwa na wakaka. Najaribu kufikiria kuwa, hata kama wao wamempenda mkaka ni ngumu kutamka wazi wazi, na wakijitahidi sana, huishia kuonyesha mapenzi kwa vitendo au kwa kumtega mtu.

Mara nyingi wao wakifunguka huwa inaleta tafsiri isiyo nzuri sana ndani ya jamii wakati kiukweli ilipaswa na wao pia wapate nafasi nzuri ya kumtamkia yule wanayempenda maana ni haki yao kimsingi.

Kwa tamaduni za wenzetu wahindi (sina uhakika kama ni wote), wanawake ndiyo huenda kumpropose mwanaume na hii imekubalika kabisa.

Naomba tuchangie jamani, kuna tatizo gani watanzania wakikubaliana na huu utaratibu wa kugawa fursa sawa kwa wote ikiwemo kuwakubalia na kutokuwatafsiri vibaya wadada wanaofunguka mbele ya wakaka?

Nawasilisha.

HP
Kwa kadiri siku zinavyozidi kwenda na kizazi cha dot com haya mambo yanabadilika sana, itakuwa wanaume ndio wanatongozwa na kuringa kama wanawake wanavyofanya.
 
Back
Top Bottom