Mbonea
JF-Expert Member
- Jul 14, 2009
- 640
- 20
September 24, 2009
Fundi ujenzi wa nchini Uingereza mwenye hasira ya kutolipwa pesa zake akishirikiana na mwanae alitumia masaa sita kulibomoa paa la nyumba aliyomaliza kuijenga baada ya mwenye nyumba kugoma kumlipa pesa zake.
Fundi ujenzi wa Uingereza Roydon Toon mwenye umri wa miaka 59 akishirikiana na mwanae Gavin, 33, walilibomoa paa la nyumba waliyoijenga huku mwenye nyumba na familia yake wakiwa ndani.
Toon na mwanae waliamua kulibomoa paa la nyumba hiyo yenye thamani ya £450,000 (Zaidi ya Tsh. Milioni 900) baada ya mwenye nyumba kugoma kuwamalizia pesa walizokuwa wakimdai tangia walipomaliza kazi yake ya ujenzi miaka mitano iliyopita.
Toon na mwanae walitumia masaa sita kung'oa vigae vya paa la nyumba hiyo na kukata mbao zinazolishikilia paa hilo huku magari ya polisi zaidi ya 10 na helikopta moja angani zikiwa zimewazunguka.
Toon alianza shughuli ya uharibifu kwenye nyumba hiyo iliyopo kwenye mji wa Barlborough kuanzia saa mbili asubuhi na aligoma kuwasikiliza polisi waliokuwa wakimuamuru ashuke chini.
Waliendelea kufanya uharibifu huo mpaka mida ya mchana waliposhuka chini na kukamatwa na polisi kwa kosa la jinai la kufanya uharibifu kwa nia ya kuhatarisha maisha ya watu.
Toon alisema kuwa alikuwa akimdai mmiliki wa nyumba hiyo James Arthur kiasi cha paundi £47,000 kwa ujenzi wa vyumba vya ziada katika jumba lake la kifahari.
Toon alisema kuwa bwana Arhur alimlipa kiasi cha paundi 32,000 na kukataa kumalizia deni la paundi 15,000 baada ya kazi ya ujenzi kumalizika kwasababu kulikuwa na gesi inayovuja katika mojawapo ya vyumba vipya vilivyojengwa.
Toon alisema kuwa kabla ya kufanya uharibifu huo alimtumia Arthur barua akimtaarifu kuwa atafanya uharibifu huo kwakuwa amegoma kumlipa pesa anazomdai kwa miaka mitano sasa.
Akiongelea kukamatwa kwake Toon alisema "Nashangaa hatua ya polisi kutukamata, hakutaka kulipa deni , nilimtumia barua kumtaarifu uamuzi wangu lakini alinipuuza".
"Kulikuwa na helikopta ya polisi angani iliyotuzunguka muda wote huku magari 10 ya polisi yakitusubiri tushuke chini. Sijutii chochote nilikuwa natafuta haki yangu" alimalizia Toon.
Toon na mwanae walitupwa mahabusu kwa muda mfupi na baadae waliachiwa huru kwa dhamana huku wakiwa wameishamtia hasara kubwa mwenye nyumba zaidi ya pesa wanazomdai.
Fundi ujenzi wa nchini Uingereza mwenye hasira ya kutolipwa pesa zake akishirikiana na mwanae alitumia masaa sita kulibomoa paa la nyumba aliyomaliza kuijenga baada ya mwenye nyumba kugoma kumlipa pesa zake.
Fundi ujenzi wa Uingereza Roydon Toon mwenye umri wa miaka 59 akishirikiana na mwanae Gavin, 33, walilibomoa paa la nyumba waliyoijenga huku mwenye nyumba na familia yake wakiwa ndani.
Toon na mwanae waliamua kulibomoa paa la nyumba hiyo yenye thamani ya £450,000 (Zaidi ya Tsh. Milioni 900) baada ya mwenye nyumba kugoma kuwamalizia pesa walizokuwa wakimdai tangia walipomaliza kazi yake ya ujenzi miaka mitano iliyopita.
Toon na mwanae walitumia masaa sita kung'oa vigae vya paa la nyumba hiyo na kukata mbao zinazolishikilia paa hilo huku magari ya polisi zaidi ya 10 na helikopta moja angani zikiwa zimewazunguka.
Toon alianza shughuli ya uharibifu kwenye nyumba hiyo iliyopo kwenye mji wa Barlborough kuanzia saa mbili asubuhi na aligoma kuwasikiliza polisi waliokuwa wakimuamuru ashuke chini.
Waliendelea kufanya uharibifu huo mpaka mida ya mchana waliposhuka chini na kukamatwa na polisi kwa kosa la jinai la kufanya uharibifu kwa nia ya kuhatarisha maisha ya watu.
Toon alisema kuwa alikuwa akimdai mmiliki wa nyumba hiyo James Arthur kiasi cha paundi £47,000 kwa ujenzi wa vyumba vya ziada katika jumba lake la kifahari.
Toon alisema kuwa bwana Arhur alimlipa kiasi cha paundi 32,000 na kukataa kumalizia deni la paundi 15,000 baada ya kazi ya ujenzi kumalizika kwasababu kulikuwa na gesi inayovuja katika mojawapo ya vyumba vipya vilivyojengwa.
Toon alisema kuwa kabla ya kufanya uharibifu huo alimtumia Arthur barua akimtaarifu kuwa atafanya uharibifu huo kwakuwa amegoma kumlipa pesa anazomdai kwa miaka mitano sasa.
Akiongelea kukamatwa kwake Toon alisema "Nashangaa hatua ya polisi kutukamata, hakutaka kulipa deni , nilimtumia barua kumtaarifu uamuzi wangu lakini alinipuuza".
"Kulikuwa na helikopta ya polisi angani iliyotuzunguka muda wote huku magari 10 ya polisi yakitusubiri tushuke chini. Sijutii chochote nilikuwa natafuta haki yangu" alimalizia Toon.
Toon na mwanae walitupwa mahabusu kwa muda mfupi na baadae waliachiwa huru kwa dhamana huku wakiwa wameishamtia hasara kubwa mwenye nyumba zaidi ya pesa wanazomdai.