Dark City
JF-Expert Member
- Oct 18, 2008
- 16,253
- 11,598
Leo nimeamua kumsindikiza mjukuu wangu kwa binti yangu wa mwisho, kwenda kwenye ofisi moja ambapo alikuwa na shida. Tulipofika kwenye hiyo ofisi (ambayo nimewazoea sana kwa kuwa nafanya nao kazi mara nyingi), tulipokelewa na mmoja wapo wa ma-secretary ambaye ametupa appointment ya kuonana na boss wake kesho. Basi ikabidi tuage ila wakati tunaondoka, niligeuka na macho yangu yakagongana na secretary mwingine ambaye alikuwa anatusikiliza muda wote huku macho yake kayakazia kwa dogo muda wote!! Yaani alikuwa kadondosha bonge la smile..kama lile linalomfanya mtu adondoke udenda (to salivate chini na juu aisee)!!
Nikamwangalia na huyo mjuu wangu (alikuwa ametoka bomba kishenzi...dizaini ya form 6 fulani), kavaa ki-Tshirt cha kubana na jeans bomba...Nikakumbuka kuwa bibi huwa anasema kwamba huyu dogo ni bonge la handsome (ingawa mie huwa sijui hawa akina bibi wanatumia vigezo gani)!!
Mzee mzima nami nikaishia kucheka na kuondoka...baadaye ndo akili ya kiume ikarudi. Nikasikitika kwamba, kwa nini mtoto wa watu sikupatia tip kuwa dogo bado yuko available??? Yaani, wale enzi zangu wangesema
"hajazuiliwa chini na juu"
Babu DC!!
Nikamwangalia na huyo mjuu wangu (alikuwa ametoka bomba kishenzi...dizaini ya form 6 fulani), kavaa ki-Tshirt cha kubana na jeans bomba...Nikakumbuka kuwa bibi huwa anasema kwamba huyu dogo ni bonge la handsome (ingawa mie huwa sijui hawa akina bibi wanatumia vigezo gani)!!
Mzee mzima nami nikaishia kucheka na kuondoka...baadaye ndo akili ya kiume ikarudi. Nikasikitika kwamba, kwa nini mtoto wa watu sikupatia tip kuwa dogo bado yuko available??? Yaani, wale enzi zangu wangesema
"hajazuiliwa chini na juu"
Babu DC!!