Fundi Mchundo
Platinum Member
- Nov 9, 2007
- 8,935
- 6,844
Wacheni wacheni wacheni ,hivi hapo kama angekodishwa mzungu mngepiga makelele,mimi nimefurahi sana kuona aliekodi ni mzalendo ingawa sijafahamu nia na madhumuni haswa ya maradi aliokusudia ,inawezekana mtu akajenga na kuinvest nyumba na kukodisha au akaweka sehemu ya Park na kuweza kujipatia fedha ,hivi ndivyo wananchi wanavyotakiwa wawekeze , mtu anaweza sehemu hiyo akaizingira na kuweka mambo ya kufurahisha jamii at the week end ndugu na jamaa wanajimwaga huko,just akaweka kiingilio labda shilingi mia tano au mia tatu kiasi hata mlala hoi anaweza kwenda kujiburudisha ,hayo ndio mambu yalioko ulaya.
na zaidi kuwa jamaa hakununua isipokuwa amekodi sasa tatizo lipo wapi Karume na Salmini wamekodisha visiwa kwa muda wa miaka 99 kuna nchi unakodi nyumba kwa miaka mia na sio unakodi unanunu nyumba kwa muda wa miaka mia ,yaani mjenzi mmiliki na hata aliekodi watakuwa hawapo tena na hiyo ndio biashala.
hapo kuna watu wamekosa mlo tu hakuna cha Chiligati wala wala Chiligate wanataka wamegewe tu ,na jamaa akimuwahi huyo wa waziri kwa donge nono basi mtaona ila hamtasikia kitu.
Watu wenye mawazo kama yako ndiyo watakaotufikisha pabaya. Wewe tatizo lako ni asikodishwe mzungu lakini hao wawahili wenzetu wanao tufanya vibaya kuliko hata huyo mgeni huoni tatizo? Ufukwe wa Oistabei ni aibu tupu. Pale palikuwa ni sehemu ambayo kila mtu anaweza kwenda kuogelea au kupunga upepo. Wakati wa enzi yake palijaa mikoko na maji na bech ilikuwa safi. Leo pamekuwa Disco (asante Coco beach), sehemu ya kutambiana magari na pikipiki, kuchomoma mishkaki ili mradi kila kitu isipokuwa kuogelea kwa usalama! Mikoko haipo tena na minazi yote vipara. Hata katika hali hii duni palikuwa ni sehemu ambapo wasioweza kwenda bongoyo waliweza kwenda kupumzika bila tatizo. Leo wahuni wanataka ku'privatise' na kuiharibu kabisa nawe unashangilia? Huu upuuzi wa kuwa ati amekodishwa na wala hakuuziwa kwani nani Tanzania anauziwa ardhi? Ardhi yote si leasehold na ina muda wake wa kumiliki? Yaani tumefika mahali kuwa hata Mungu hatumuogopi kwa ulafi wetu? Mungu atunusuru na waovu wote, wageni na waswahili wenzetu. Hawana tofauti hawa.