Asprin
JF-Expert Member
- Mar 8, 2008
- 68,012
- 95,356
Hahahahaha! dah!...... mkuu kuna msemo mmoja unasema "aisifuye mvua, imemnyea"Nikiwa mwanaume na ninaeishi DAR zaidi ya miaka 25 nasema:
1. Sina shaka wanaume wa Dar wamekutenda,au wamekuingiza mjini pole sana. Labda nikuulize umepona??(sijui unanielewa?)
2. Lazima wakushangae ....Dar ni joto sana wewe ukitembea na makoti na masweta mazito mwilini kwa nini wasishangae??
3. Vilevile staili yako ya uvukaji wa barabara hasa zile za highway lazima uliwaacha hoi hao waliokushangaa.
4. Dar kuna wanaume wa kila aina,kwa watoto wa mama inaongoza, kwa wanaume walioajiriwa pia Dar inaongoza. Kwa wanaume wafanya biashara wengi zaidi pia inaongoza hapa TZ.Nenda ofisi za takwimu waweza kujua ni mji gani TZ unaongoza kwa idadi kubwa ya wafanyabiashara au walioajiriwa. ULIKUTANA NA VIJANA WA KIJIWENI.....HALAFU DAR MTU WA KIJIWENI WAWEZA DHANI NI MENEJA VILE KULE KWENU KUMBE YEYE NI.........WANAITA MISHENI TOWN.
5. Taja duka moja tu na eneo lilipo ambapo wanauza hizo dawa za nguvu za kiume. Au mkuu umechanganya wale wauza dawa za kienyeji na duka la DAWA?? ulijaribu kuwapigia kwa mtandao wa tigo ukaona bado hawasomeki???
6.Ni vigumu sana kuielewa DAR haraka haraka. Sina shaka ulipita vijiweni inawezekana nawe ni wa kijiweni.
Nenda pale kariakoo sokoni utakuta wanaume wanapiga sahani mbili za chakula na mikate miwili na hajashiba...HAO NI WABEBA LUMBESA. Ungekutana na aina hii ya wanaume ungesema duuuuu wanaume wa DAR kwa KULA !!!!!!!!
7. Siku nyingine ukija DAR acha kutembelea au kujipitisha vijiweni....... ha ha ha ha SIKU NYINGINE KARIBU TANDALE KWA MTOGOLE...........
Wabilah Tawfiq
Mwanaume wa DAR.