mirindimo
JF-Expert Member
- Nov 2, 2009
- 821
- 1,338
Nimetoka mhimbili mda si mrefu na nikaonana na daktari bingwa mmoja samahani sitamtaja jina hapa.........na akasema wao ndio wanaolea hicho kilichopo sasa wameamua kugoma ili serikali itimize wanachodai!!!! Akaongeza kua kila daktari wa kijeshi anaposaini asubuhi kufanya kazi ana laki moja nje ya mshahara wa kazi na hapo bado hajaitwa "Call",na kuna chakula special wanaletewa kutoka catering flani hivi hii nadhani ni ya fisadi mmoja......na hawaruhusiwi madaktari wa mhimbili kula pale .....alisogea mmoja akaambiwa samahani Dr. hiki ni kwa ajili ya madaktari wageni tu.......mmmmmh....akiongea kwa uchungu akasema wao hutumia usafiri wao kila wanapoitwa call na kulipwa pesa kiduchuuuuuu sana na si hivo tu usafiri wa kurudi nyumbani na kuja kazini wanajitegemea.....!!!!! Mi nilishindwa kuzungumza nilikua nawalaumu sasa naelewa madai yao ni ya msingi!!!!!!!
Naomba serikali iwasikilize na itekeleze wanachotaka.....nawasilisha:canada:
Naomba serikali iwasikilize na itekeleze wanachotaka.....nawasilisha:canada: