From Goatherd to Governor, Edwin Mtei's Autobiography

Ningependa kumuuliza Mzee Bw. Edwin Mtei natumaini huwa labda anasoma humu au kama kuna mtu anayeweza kumjibia pia sio mbaya!

Ni hivi majuzi nilinununua Kitabu chake kiitwacho From Goatherd to Governor au (kutoka uchungaji kondoo mpaka kufikia Cheo cha Ugavana wa Benki Kuu)!

Na lengo hasa la kununua hicho Kitabu lilikuwa ni kupata undani wa Mwana Chadema Nr.1 TZ ili kuweza kupata angalau picha ya ni nini nitegemee endapo CHADEMA ikiweza kupata nafasi ya kuongoza!

Moja ya jambo lililonigusa ni pale hasa alipoelezea yeye kutofautiana na Raisi wa 1 wa Tz
Bw. JK Nyerere hasa kuhusiana na sera, ambapo yeye alitaka kwamba sisi tukubali ushauri wa Benki ya Dunia na Shirika la Fedha Duniani ili kunusuru hali mbaya ya uchumi wetu, jambo ambalo bosi wake wakati huo alilikataa, na hivyo kupelekea yeye kujiuzulu!

Baadaye Tanzania ikaja kukubali kufwata mfumo na ushauri wa Benki ya Dunia, na yeye
Bw.Mtei kulingana na maelezo yake mwenyewe ndani ya Kitabu, alishiriki ktk kuishauri Serikali ya awamu ya 2 jinsi ya kufanya mageuzi ya kiuchumi wakati huo akiwa yuko Shirika la Fedha, na moja ya Ushauri ulikuwa ni sisi kukubali kushusha thamani ya fedha yetu (jambo ambalo Bw.Nyerere alilipinga siku zote ingawaje mwisho wa siku ilibidi asalimu amri) na pia kufungua Uchumi wetu Duniani, mambo ambayo Serikali ilitekeleza!

Sasa swali langu ni hivi, Je bado unaamini kwamba ushauri ulioupa Serikali ya Awamu ya 2 ulikuwa sahihi? ukichukulia kwamba matatizo au changamoto zinazotukabili sasa zimetokana na sisi kufwata ushauri wako wakati wewe ukiwa mshauri wa Shirika la Fedha Duniani?

Je bado unafikiri kwamba swala la sisi kukubali kushusha Thamani ya Shilingi yetu lilikuwa sawa ukichukulia sasa pesa yetu imepoteza thamani kabisa? Sasa hivi Tz haina maana hata kuweka akiba kwani kila siku Fedha yetu inashuka thamani ukiwa na milioni 2 leo miaka 2 baadaye haina maana yoyote!

Je CHADEMA bado watafuata hizo Sera ulizoshiriki kuishauri Serikali ya awamu ya 2 izifwate?

 
Kijakazi

what matters most today is to do a right thing at the right time.........

mugabe hakunyang'anya wazungu ardhi wakati ule.....wakaja kunyang'anya uzeeni....imewagarimu zimbabwe....

nyerere aliwanyang'anya kupitia azimio la arusha......... leo tunawaita kwa kutumia hata ushirikina...TUNA AKILI KWELI?
 
Last edited by a moderator:
Ukweli ni kwamba kufuata kwetu masharti ya IMF kwa miaka takriban 30 hakujatusaidia watanzania bali kumetudhoofisha sana,.... hao ndiyo washauri walioisaidia Tanzania kuuza kila tulicho nacho, mpaka vitalu.

I've never been a fan, I am not a fan and will never be a fan.
 
Ukweli ni kwamba kufuata kwetu masharti ya IMF kwa miaka takriban 30 hakujatusaidia watanzania bali kumetudhoofisha sana,.... hao ndiyo washauri walioisaidia Tanzania kuuza kila tulicho nacho, mpaka vitalu.

I've never been a fan, I am not a fan and will never be a fan.

Duh! Basi kazi ipo, kama mtu unatukanwa kwa kutaka kufahamu, Msimamo wa Chama ambacho kinatafuta ridhaa ya kuongoza Nchi, hilo linaacha maswali mengi kuliko majibu!

 
Ubovu wa nchi hii ni vilaza walioko juu kutekeleza mipango mizuri ya taifa hili, mbona nchi nyingine zimevuka hatua hii?
 
Ubovu wa nchi hii ni vilaza walioko juu kutekeleza mipango mizuri ya taifa hili, mbona nchi nyingine zimevuka hatua hii?

Hatua ipi unayojaribu kuilezea? Je kuna uhusiano na yale niliyopenda kuyafahamu, na maelezo yako? Embu funguka kidogo kama ukiweza!
 
Ubovu wa nchi hii ni vilaza walioko juu kutekeleza mipango mizuri ya taifa hili, mbona nchi nyingine zimevuka hatua hii?
 
Duh! Basi kazi ipo, kama mtu unatukanwa kwa kutaka kufahamu, Msimamo wa Chama ambacho kinatafuta ridhaa ya kuongoza Nchi, hilo linaacha maswali mengi kuliko majibu!

Sasa hapa kobelo kakutukana wapi? Na kwa nini uamini kuwa aliye-comment ni mwanachama wa Chadema?
Halafu mbona kwenye maelezo yako hujasema unatafuta msimamo wa chama pekee bali swali linaelekezwa kwa Mtei
au wanaoweza kusaidia kujibu. Na hapo ndipo unapoalika wengine waingie kwenye mjadala, na si lazima wawe
wanachama wa Chadema au Mtei peke yake.

Mkuu unapoandika kutaka Opinion (umesema usaidiwe) usiwe na yako mfukoni. Sikiliza halafu chambua mwenyewe.
BTW maelezo ya Kobelo haya hapa chini:

Ukweli ni kwamba kufuata kwetu masharti ya IMF kwa miaka takriban 30 hakujatusaidia watanzania bali kumetudhoofisha sana,.... hao ndiyo washauri walioisaidia Tanzania kuuza kila tulicho nacho, mpaka vitalu.

I've never been a fan, I am not a fan and will never be a fan.
 
Last edited by a moderator:
Mzee Mtei ni mjanja wa zamani, kila kitu ni ujanja ujanja tu! Serikali ilimsomesha kwa gharama lakini output yake kwa hii nchi ni ndogo sana ukilinganisha na ya mtu kama Mh. Mwigulu.
 
Ukweli ni kwamba kufuata kwetu masharti ya IMF kwa miaka takriban 30 hakujatusaidia watanzania bali kumetudhoofisha sana,.... hao ndiyo washauri walioisaidia Tanzania kuuza kila tulicho nacho, mpaka vitalu.

I've never been a fan, I am not a fan and will never be a fan.
Kobello,
Moja ya udhaifu wa serikali ya Mwinyi ilikuwa kutokukusanya kodi. Hii ilipelekea bidhaa zetu kushindwa kushindana na bidhaa toka nje ambazo hazikulipiwa kodi, hivyo viwanda vyetu vikaoonekena mzigo na kuvigeuza mabohari. Siamini kuwa IMF walimshauri Mwinyi asitoze kodi.
Hata swala la thamani ya shilingi, tusingeng'ang'ania kubaki na thamani ileile ya shilingi wakati kiuhalisia thamani yake ilikuwa chini sana kulingana na mali tuliyokuwa nayo. Nakumbuka wakati fulani hata Mwalimu mwenyewe amewahi kuulaumu utawala wa Mwinyi kwamba wakati ilikuwa sahihi kuyaacha yale makosa yaliyofanywa na Mwalimu, alishangaa kuwa hata mazuri wanayaacha. In a way, alikubali kuwa kuna makosa aliyafanya.
 
Sasa hapa kobelo kakutukana wapi? Na kwa nini uamini kuwa aliye-comment ni mwanachama wa Chadema?
Halafu mbona kwenye maelezo yako hujasema unatafuta msimamo wa chama pekee bali swali linaelekezwa kwa Mtei
au wanaoweza kusaidia kujibu. Na hapo ndipo unapoalika wengine waingie kwenye mjadala, na si lazima wawe
wanachama wa Chadema au Mtei peke yake.

Mkuu unapoandika kutaka Opinion (umesema usaidiwe) usiwe na yako mfukoni. Sikiliza halafu chambua mwenyewe.
BTW maelezo ya Kobelo haya hapa chini:

Wewe nafikiri utakuwa na matatizo na unakurupuka kujibu bila kusoma vizuri, embu rudia kusoma mada yangu, halafu usome na ya kobelo halafu rudia tena kusoma niliyomjibu Kobelo, labda utaelewa!

 
Moja ya udhaifu wa serikali ya Mwinyi ilikuwa kutokukusanya kodi. Hii ilipelekea bidhaa zetu kushindwa kushindana na bidhaa toka nje ambazo hazikulipiwa kodi, hivyo viwanda vyetu vikaoonekena mzigo na kuvigeuza mabohari. Siamini kuwa IMF walimshauri Mwinyi asitoze kodi.
Hata swala la thamani ya shilingi, tusingeng'ang'ania kubaki na thamani ileile ya shilingi wakati kiuhalisia thamani yake ilikuwa chini sana kulingana na mali tuliyokuwa nayo. Nakumbuka wakati fulani hata Mwalimu mwenyewe amewahi kuulaumu utawala wa Mwinyi kwamba wakati ilikuwa sahihi kuyaacha yale makosa yaliyofanywa na Mwalimu, alishangaa kuwa hata mazuri wanayaacha. In a way, alikubali kuwa kuna makosa aliyafanya.
Tatizo la IMF halihusiani na kukusanya kodi.Kwani Tanzania ilikuwa haiweki fedha IMF? Kama tulikuwa tunaweka fedha IMF, kwanini nchi kama Uruguay katika kipindi hichohicho ambacho serikali ya Tanzania ilikuwa inahitaji fedha kusurvive, ipewe mkopo mkubwa wa fedha bila kuwa na akiba yeyote IMF na bila kuwa na shida ya fedha kuendesha serikali kulinganisha na Tanzania??

Pili, kwa taarifa yako tu, wakati Tanzania inaingia mkataba na IMF hakukuwa na bidhaa za nje ambazo zilikuwa zinashindana bei na za Tanzania. Bado beer ya Safari ilikuwa inapendwa kuliko Tusker, bado sportsman ya Tanzania ilipendwa kuliko ya Kenya, Tan Bond ilikuwa inapendwa kuliko Blue Band......

Labda ungeniambia specifically ni bidhaa zipi kwa mfano, ambazo zilikuwa cheap kuliko za Tanzania.
 
nategemea kuona hoja tetezi, toka kwa die hard members wa Chadema, Babu mtei pia aje atuambie kama maono yake yalikua sahihi au yalituingiza shimoni, na kama maono ya kuanzisha Chadema tuamini pia au ndio kutuingiza motoni kabisa
 
Wewe nafikiri utakuwa na matatizo na unakurupuka kujibu bila kusoma vizuri, embu rudia kusoma mada yangu, halafu usome na ya kobelo halafu rudia tena kusoma niliyomjibu Kobelo, labda utaelewa!

Duh! Basi kazi ipo, kama mtu unatukanwa kwa kutaka kufahamu, Msimamo wa Chama ambacho kinatafuta ridhaa ya kuongoza Nchi, hilo linaacha maswali mengi kuliko majibu!

Labda hayo maelezo yana-relate vipi na maoni ya Kobelo (umem-quote). Umetukanwa na Thread, Kobelo AU wewe mwenyewe? Au unahisi utatukanwa?

BACK TO THE TOPIC:

Masharti yaliyokuwa yanatolewa na IMF hayakuwa 'unique" kwa Tanzania peke yake, rungu hilohilo lilizidondokea hata
nchi zilizoko Asia, ndiyo maana hata reforms kwa hizo Nchi hazikuwa na tofauti sana na zetu.

Nafikiri kwa namna fulani ilikuwa ni lazima kufanya mageuzi, kwa mfano Tanzania ilkuwa imeziba milango kwa bidhaa kutoka nje, Sekta binafsi haikupata fursa ya kufanya mambo yake. Udhibiti ulikuwa mkubwa sana na kupelekea kuadimika kwa bidhaa nyingi muhimu. Hata watu kufanya biashara kwa uhuru ili kuimarisha Private sector ilikuwa shida.

Na hata idadi ya wafanyakazi kwenye Public service ilikuwa kubwa mno. Ofisi moja watu ishirini, wengine hata kazi wanazofanya hazijulikani alimradi kuhamisha file kutoka hapa kwenda kule!

Kosa moja kubwa tulilolifanya. kama alivyosema Mzee Mwinyi: Badala ya kufungua madirisha ili tupate hewa safi, tukafungua na milango yoote na humo wakaingia na Mbu.
 
Ningependa kumuuliza Mzee Bw. Edwin Mtei natumaini huwa labda anasoma humu au kama kuna mtu anayeweza kumjibia pia sio mbaya!

Ni hivi majuzi nilinununua Kitabu chake kiitwacho From Goatherd to Governor au (kutoka uchungaji kondoo mpaka kufikia Cheo cha Ugavana wa Benki Kuu)!

Na lengo hasa la kununua hicho Kitabu lilikuwa ni kupata undani wa Mwana Chadema Nr.1 TZ ili kuweza kupata angalau picha ya ni nini nitegemee endapo CHADEMA ikiweza kupata nafasi ya kuongoza!

Moja ya jambo lililonigusa ni pale hasa alipoelezea yeye kutofautiana na Raisi wa 1 wa Tz
Bw. JK Nyerere hasa kuhusiana na sera, ambapo yeye alitaka kwamba sisi tukubali ushauri wa Benki ya Dunia na Shirika la Fedha Duniani ili kunusuru hali mbaya ya uchumi wetu, jambo ambalo bosi wake wakati huo alilikataa, na hivyo kupelekea yeye kujiuzulu!

Baadaye Tanzania ikaja kukubali kufwata mfumo na ushauri wa Benki ya Dunia, na yeye
Bw.Mtei kulingana na maelezo yake mwenyewe ndani ya Kitabu, alishiriki ktk kuishauri Serikali ya awamu ya 2 jinsi ya kufanya mageuzi ya kiuchumi wakati huo akiwa yuko Shirika la Fedha, na moja ya Ushauri ulikuwa ni sisi kukubali kushusha thamani ya fedha yetu (jambo ambalo Bw.Nyerere alilipinga siku zote ingawaje mwisho wa siku ilibidi asalimu amri) na pia kufungua Uchumi wetu Duniani, mambo ambayo Serikali ilitekeleza!

Sasa swali langu ni hivi, Je bado unaamini kwamba ushauri ulioupa Serikali ya Awamu ya 2 ulikuwa sahihi? ukichukulia kwamba matatizo au changamoto zinazotukabili sasa zimetokana na sisi kufwata ushauri wako wakati wewe ukiwa mshauri wa Shirika la Fedha Duniani?

Je bado unafikiri kwamba swala la sisi kukubali kushusha Thamani ya Shilingi yetu lilikuwa sawa ukichukulia sasa pesa yetu imepoteza thamani kabisa? Sasa hivi Tz haina maana hata kuweka akiba kwani kila siku Fedha yetu inashuka thamani ukiwa na milioni 2 leo miaka 2 baadaye haina maana yoyote!

Je CHADEMA bado watafuata hizo Sera ulizoshiriki kuishauri Serikali ya awamu ya 2 izifwate?


Kwanza aingefaa tujue kuwa Tanzania kama ilivyo kuwa mataifa mengine wakati ule kulikuwa na MIFUMO MIKUU YA UCHUMI either mfumo wa uchumi SOKO WENYE KUSHIKILIWA NA UWEKEZAJI BINASFI au uchum hodhi IKIENDESHWA NA SERIKALI (STATE). UCHUMI HODHI ULIKUWA NA MIRENGO YA kijamaa/Kisoshalisti kama hapa kwetu Tanzania na USSR ya wakati ule au UKOMUNISTI kule China. Na mfumo wa Kiliberali wa soko ndio uliokuwa ukishauriwa na WB na IMF. Miongoni mwa matakwa ya mfumo wa soko ni Ubinafsishaji na uwekezaji binafsi.

Sasa kabla ya kuuliza kwa mtu yeyote inafaa tuumize vichwa kidogo tu, Kama China imefanikiwa kukuza uchumi wake hadi kufikia nambari mbili duniani, Urusi baada ya kuvunjika iliyokuwa USSR ni miongoni mwa mataifa 8 yenye uchumi mkubwa wa viwanda duniani (G8) na mataifa mengine mengi chumi zao zimekua katika mfumo huohuo wa SOKO wenye uwekezaji bunafsi kwanini Tanzania imeshindikana? Ikumbukwe kuwa CHINA uwekezaji mkubwa ni wa makampuni ya ulaya na America.


Turejee uwekezaji hapa Tanzania: Makampuni ya nchi mbalimbali kama canada, Ulaya, Marekani nk yamewekeza pia TZ katika secta za madini, gesi viwanda, utalii na mahoteli, Kandarasi za uzalishaji wa umeme (Simbion, IPTL ) orodha ni ndefu....Sasa swali kwanini mfumo huu unaleta mafanikio ya kukuza uchumi katika maifa mengine na mfumo huohuo uwe ni failure? Huo kungine CHINA, URUSI, nk IFM iliongeza kitu gani cha ziada wakafanikiwa ambacho sisi tulinyimwa tukashindwa? IFM ndio waliowashauri watawala wetu waingie mikataba ya madini kwa mirabaha ya 3%? MBONA KENYA HAWANA MADINI KAMA SISI, WALISHAKUWA NA UCHUMI WA MFUMO WA SOKO TUNAOTAKA KUUTUPIA LAWAMA TAGU UHURU WAO, HAWANA ARDHI KUBWA KAMA SISI LAKINI UCHUMI WAO UKO JUU SANA? Tusitafute mchawi. TANZANIA TUNA LAANA NA OMBWE LA UONGOZI/USIMAMIZI WA KIUCHUMI (POOR ECONOMIC MANAGEMENT). CCM NDIO INAYOTAWALA TANGU TUPATE UHURU WULIZWE HAO SIO MTU MWINGINE YEYOTE!!!
 
Kijakazi

what matters most today is to do a right thing at the right time.........

mugabe hakunyang'anya wazungu ardhi wakati ule.....wakaja kunyang'anya uzeeni....imewagarimu zimbabwe....

nyerere aliwanyang'anya kupitia azimio la arusha......... leo tunawaita kwa kutumia hata ushirikina...TUNA AKILI KWELI?

Unayosema ni sawa na ndio maana ningependa kujua Muandishi wa Kitabu ana maoni gani kuhusu hili.

K
wa Bahati mbaya sana hajajitokeza kujaribu kunielezea kutokana na sababu ambazo siwezi kuzifahamu, lkn kwangu mimi ni muhimu sana kujua maoni ya mtu mwenye ushawishi mkubwa sana ndani ya CHADEMA, hasa ukichukulia kwamba CHADEMA wanajaribu kutushawishi kwamba wao ni bora kuliko CCM, na kwamba tukiwapa ridhaa yakuongoza watafanya mengi mazuri kuliko CCM, wakati huo huo mtu aliyeshiriki kuishauri Serikali yetu ya CCM kufwata sera ambazo tunazifwata sasa hivi ndio mwasisi wa CHADEMA!
 
Duh leo nilikuwa napekua pekua nondo za zamani nikakutana na kitabu cha Mzee Mtei sijui kama kinapatikana katika bookshop zetu.
 
Watanzania tujenge tabia ya kufiki chanya, Mzee Mtei ni Role Model kwa kizazi cha sasa ambacho hakipendi kujishughulisha na badala yake ni kulaumu kila kitu. Nani kakuambia umaskini wako utaondoka kwa kubeza juhudi za wenzio. Do something good to leave behind your footprints
 
Back
Top Bottom