From Diamond Jubilee: Rais Kikwete aongea na Wazee wa Darisalama!

Baada ya mkutano na madaktari ikulu madaktrai wakaomba wakutane wao ili waamue
 
Pasco kuna dalili ya TV yoyote kuwa live? TBC wapo?? Nina hamu ya kujua TBC watachagua wapi? Arumeru kwenye pesa ama Diamond kwa mwenye mali!
Cheki tbc live mkuu anaongea hoja ya kwanza ni madaktari
 
Anaanza kuongelea migomo ya madaktari kuanzia december 2011 hadi march 2012
 
vibalaghashia vimejaa ukumbini.Mkuu wa mkoa anadai rais kila akitaka kuzungumza mambo ya msingi huwa anawaita hao wazee.Kama rais anazungumza mambo ya msingi na vihiyo sijui nchi inaenda wapi

Hii ni Kama muhadhara wa baraza la Idd!
 
kumekuwa na mgomo wa madaktari mara 3,mwishon mwa desemba (INTERNS-Hawa bado ni wanafunzi wanfanyiwa tathimini na madaktari bingwa kwa miaka 2.)-sabab u ya mgomo ni posho kuchelewa
 
Ktk malipo interns wanalipwa asilimia 60 za malipo ya madaktrari,tatizo posho hazikuwekwa kwenye fungu la mishahara ila kwenye fungu la matumizi mengine
 
Binafsi nadhani JK ana tuma ujumbe kwa "mahasimu" wake wanaodhani
wana mzidi nguvu,....kwamba ana hutubia siku ambayo wana "mtangaza mteule wao"
huko arumeru!
Anaonesha kwamba anaweza tumia kila anachotaka,kwa kuanza tu,vyombo vyote vya
habari viko kwake na arumeru ni kimya.

Kesho sasa,magazeti yata muongelea JK katika front page,Arumeru itakua page moja kabla
ya page ya michezo.
 
Fungu la matumizi mengine hua linapata dharura nyingi,desemba wizara zote zilikua na matatizo katika fungu hili
 
Anazungumza na wazee wa Dar au anahutubia wanachama wa CCM waliojichokea na kukata tamaa?
Wamelipwa elfu hamsini waje wapige makofi, miluzi na vigelegele
Tunataka rais aongee na wasomi, wa-brainstorm namna ya kututoa huku shimoni tuliko sio hiyo mipasho
 
Kumbe posho za interns ziko kwenye fungu la OC badala ya PE ndio maana walichelewa kulipwa. nadhani atasema posho ziwe PE badala ya OC
 
Posho kwa interns ndo kila kitu kwao,usafiri na chakula,kuzidi kuchelewa posho kulileta mivutano na madaktari,kati ya hospitali zilizokuwa na vyanzo vingine ziliwalipa madaktari hao
 
Binafsi nadhani JK ana tuma ujumbe kwa "mahasimu" wake wanaodhani
wana mzidi nguvu,....kwamba ana hutubia siku ambayo wana "mtangaza mteule wao"
huko arumeru!
Anaonesha kwamba anaweza tumia kila anachotaka,kwa kuanza tu,vyombo vyote vya
habari viko kwake na arumeru ni kimya.

Kesho sasa,magazeti yata muongelea JK katika front page,Arumeru itakua page moja kabla
ya page ya michezo.

Kwa hili namkubali JK
 
Sitting arrangment iko poa, waheshimiwa wabunge upande wao, viongozi wa serikali upande wao ila sijaona upande wa mhimili wa mahakama!.

Ukiangalia mawazi ya wengi wa hawa wazee wa Darisalama, wamevalia sare ya chama chao wanachokifahamu tangu zamani, nadhani organization ya mahudhurio ni kupitia wale mabalozi wetu wa nyumba kumi kumi!.
...hivi hapo Dar es salaam hakuna wazee wengine zaidi ya hao wa CCM?...kunahaja sasa ya wazee ambao sio wanachama wa CCM kujitokeza kudai haki yao ya kusikilizwa,la sivyo sisi vijana wa leo tutawajumlisha ktk lawama hao wazee wengine walioamua kukaa kimya na kuwangalia wenzao wa CCM wakilipotosha na kulipeleka kombo taifa...
 
Serikali nzima iko hapa wakiongozwa na mawaziri, miongoni mwao ni wale mawaziri na naibu wake ambao ndio muhimu kuliko mawaziri wengine wote. Hawa ni wale wanaoshikilia ile wizara nyeti kwa afya na uhai wa Watanzania!. Kama kuna watu mnadhania kuwa JK atawatemesha mzigo mtakuwa mmepotea sana!.

Mkuu subira yavuta kheri. Yako macho. Ila usitarajie mapya zaidi ya kuwalaum madaktari.
 
Back
Top Bottom