kwahiyo anaongea na wazee au wabunge na viongozi wa serikali?
Kuongea na wazee wa Dar
Halafu kwanini JK hatoagi nafasi ya kuulizwa maswali na hao wazee?
Kuongelea nini?
nani aliwambi wazee wako dar peke yake?.kila siku anaongea na wazee wa dar kwani mbeya hakuna wazee....hahhaha
Sitting arrangment iko poa, waheshimiwa wabunge upande wao, viongozi wa serikali upande wao ila sijaona upande wa mhimili wa mahakama!.
Ukiangalia mawazi ya wengi wa hawa wazee wa Darisalama, wamevalia sare ya chama chao wanachokifahamu tangu zamani, nadhani organization ya mahudhurio ni kupitia wale mabalozi wetu wa nyumba kumi kumi!.
OB Vans 2 za TBC-1 na TBC-Taifa zimetia nanga hapo nje, nadhani wanasubiri tuu rais aingie waanze kurusha live!.TBC kimyaaaaaa wao wako baharini na viumbe vya Munyaazi Mungu. Angalao hata watoto wetu watajifunza aina ya viumbe waishio baharini!
Serikali nzima iko hapa wakiongozwa na mawaziri, miongoni mwao ni wale mawaziri na naibu wake ambao ndio muhimu kuliko mawaziri wengine wote. Hawa ni wale wanaoshikilia ile wizara nyeti kwa afya na uhai wa Watanzania!. Kama kuna watu mnadhania kuwa JK atawatemesha mzigo mtakuwa mmepotea sana!.