Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 301
WANAHARAKATI wa kada mbalimbali nchini, wameanzisha umoja unaojulikana kwa jina la Friends Of Dk. Slaa (FOD) kwa ajili ya kumsaidia kwa hali na mali kuhakikisha mgombea huyo wa kiti cha urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), anashinda.
FOD ambao wameanza harakazi za kuhamasishana nchini nzima, leo wanatarajia kuwa na kikao kizito kwa ajili ya kuangalia namna bora ya kuhakikisha Dk. Slaa anaibuka kidedea.
Akizungumza na Tanzania Daima Jumatano, Mratibu wa FOD, Seleman Rehani, alisema kuwa kundi hilo linajumuisha wafanyabiashara wakubwa nchini, wanafunzi wa vyuo, wanawake na kada zingine katika jamii ambao pia wana itikadi tofauti za vyama.
"Marafiki wa Dk. Slaa (FOD) ni jumuiya kubwa ambayo inaundwa na watu mbalimbali wenye itikadi tofauti za vyama. Kundi hilo linaunganishwa na masuala ya msingi yanayolihusu taifa na linakerwa na ufisadi na umaskini wa Watanzania.
Limeamua kuuanzisha umoja huo kuhakikisha mpiganaji wao anaingia Ikulu, kuleta maendeleo," alisema Rehani.
Kwa mujibu wa mratibu huyo, FOD imefungua akaunti maalum na mtandao wa mawasiliano unaoelekeza namna ya kujiunga na kumsaidia Dk. Slaa katika mkakati wake wa kutaka kuingia Ikulu.
"Tumeanza hivi karibuni, tulipoanza tulikuwa kama marafiki 200, lakini sasa mtandao wetu ni mkubwa. Tumejipanga kuhakikisha Dk. Slaa atakapoanza kampeni, anawafikia wananchi wote na kundi letu kwa sasa lipo nchi nzima," alitamba mratibu huyo.
Alisema hivi sasa wanaangalia namna bora ya kuwafikia vijana wa kati ambao bila shaka wanampenda Dk. Slaa, lakini hawakujua namna ya kumfikia na kumchangia.
"Kundi letu sio la matajiri tu. Tunataka hata Mtanzania wa chini mwenye mchango wa mawazo na kila hali amsaidie Dk. Slaa na ndio moja ya malengo ya FOD kuwa na mkutano huo kesho (leo)," alisisitiza.
.........Yaani kampeni za Slaa kama ya Obama vile..........mwaka huu yetu macho.
FOD ambao wameanza harakazi za kuhamasishana nchini nzima, leo wanatarajia kuwa na kikao kizito kwa ajili ya kuangalia namna bora ya kuhakikisha Dk. Slaa anaibuka kidedea.
Akizungumza na Tanzania Daima Jumatano, Mratibu wa FOD, Seleman Rehani, alisema kuwa kundi hilo linajumuisha wafanyabiashara wakubwa nchini, wanafunzi wa vyuo, wanawake na kada zingine katika jamii ambao pia wana itikadi tofauti za vyama.
"Marafiki wa Dk. Slaa (FOD) ni jumuiya kubwa ambayo inaundwa na watu mbalimbali wenye itikadi tofauti za vyama. Kundi hilo linaunganishwa na masuala ya msingi yanayolihusu taifa na linakerwa na ufisadi na umaskini wa Watanzania.
Limeamua kuuanzisha umoja huo kuhakikisha mpiganaji wao anaingia Ikulu, kuleta maendeleo," alisema Rehani.
Kwa mujibu wa mratibu huyo, FOD imefungua akaunti maalum na mtandao wa mawasiliano unaoelekeza namna ya kujiunga na kumsaidia Dk. Slaa katika mkakati wake wa kutaka kuingia Ikulu.
"Tumeanza hivi karibuni, tulipoanza tulikuwa kama marafiki 200, lakini sasa mtandao wetu ni mkubwa. Tumejipanga kuhakikisha Dk. Slaa atakapoanza kampeni, anawafikia wananchi wote na kundi letu kwa sasa lipo nchi nzima," alitamba mratibu huyo.
Alisema hivi sasa wanaangalia namna bora ya kuwafikia vijana wa kati ambao bila shaka wanampenda Dk. Slaa, lakini hawakujua namna ya kumfikia na kumchangia.
"Kundi letu sio la matajiri tu. Tunataka hata Mtanzania wa chini mwenye mchango wa mawazo na kila hali amsaidie Dk. Slaa na ndio moja ya malengo ya FOD kuwa na mkutano huo kesho (leo)," alisisitiza.
.........Yaani kampeni za Slaa kama ya Obama vile..........mwaka huu yetu macho.