Freemason...

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,268
33,041
Na Mwandishi wetu
HEKAHEKA ya wimbi la mastaa wa Bongo kutumika kwenye imani inayodaiwa kuwa ni ya kishetani duniani maarufu kwa jina la Freemason a.k.a Wajenzi Huru inazidi kuchukua nafasi kwa kasi baada ya hivi karibuni kudaiwa kuwa, staa wa sinema za Bongo, Jacqueline Wolper Massawe naye ametumbukia humo, Risasi Jumamosi limesheheni.
NI NCHINI AFRIKA KUSINI
Kwa mujibu wa chanzo cha uhakika, Wolper ameinamisha kichwa na kumwagiwa maji ya imani hiyo kama ishara ya kujiunga nchini Afrika Kusini, mapema mwaka huu.
NANI SHAHIDI?
Mmoja wa marafiki wa Wolper aliliambia gazeti hili kwamba, Wolper alishawishiwa na msanii mwingine wa kiume wa filamu Bongo ambaye hana jina kubwa kuwa ndiye aliyempa namba za mawasiliano za wahusika nchini Afrika Kusini.
“Wolper ameingia Freemason na aliyemshawishi ni msanii ….(anataja jina), yeye alimwambia akiwa huko anaona matunda yake kwani ni imani ambayo binadamu unaishi kama peponi,” alisema rafiki huyo.
UTAJIRI WA HARAKA WATAJWA
Kwa mujibu wa chanzo hicho, tangu Wolper amejiunga na imani hiyo inayosambaa kwa kasi nchini Tanzania amekuwa akipata mafanikio makubwa tena kwa haraka.
“Wee kama unataka kuamini, angalia tangu mwaka huu (2012) umeanza, Wolper mambo yanamyookea tu. Awali alikuwa akiishi eneo ambalo halimfai kama staa, sasa amehamia Mbezi, tena kwenye jumba zuri sana,” alisema mtoa habari huyo.
Aliendelea kuweka wazi kuwa, magari na miradi mingine aliyonayo si ofa kutoka kwa mchumba wake aitwaye Abdallah Mtoro ‘Dallas’ kama anavyodai mwenyewe Wolper bali ni ‘baraka’ ya Freemason.
Akasema: “Mmekuwa mkiandika eti kanunuliwa magari na mchumba wake, nani kasema? Ile ni kama njia ya kukwepea tu, lakini ukweli ni kwamba Freemason ndiyo wanambeba kwa sasa.”
Akaongeza: “Wazazi wa Wolper wapo katika wakati mgumu, mama yake amepata fununu za mwanaye kujiunga na Freemason na ndugu wakamweka chini kumwonya kama ni kweli ajitoe mara moja.”


KANUMBA ALIJIUNGIA NIGERIA
Hivi karibuni, mtu mmoja aliyejitaja kuwa ni mchungaji wa kanisa moja la kiroho jijini Dar, George Kariuki alizungumza kupitia Kituo cha Radio Times FM na kudai kuwa marehemu Steven Kanumba alijiunga na u-Freemason nchini Nigeria, nchi ambayo iko mbali kidogo kutoka Tanzania kuliko ilivyo Afrika Kusini anakodaiwa kwenda Wolper.
Hata hivyo, matokeo ya Kanumba kujiunga yalionekana, kupata mali kwa kasi ya ajabu, nyota yake kung’ara lakini mwisho wa yote ilifika mahali imani hiyo inatajwa na baadhi ya watu kuwa ndiyo chanzo kikuu cha kifo chake (Mungu amlaze pema peponi-amina).


BOFYA HAPA UMSIKIE WOLPER
Baada ya madai hayo, Risasi Jumamosi lilimsaka Wolper kwa nguvu zote na kubahatika kukutana naye siku ya Jumatano maeneo ya Mlimani City jijini Dar es Salaam.
Baada ya salamu, msanii huyo mwenye aibu kwa mbali, alisomewa ‘mashitaka’ yake yote huku akiwa amemkazia macho paparazi.
Wolper: “Mh! jamani, mnajua haya mambo bwana yana siri kubwa ndani yake. Wako watu wanatajwa ni Freemason, wengine wapo lakini hawatajwi, ni kwa nini?”


WOLPER JIBU SWALI
Paparazi: “Labda kikubwa ungetuambia ni kweli upo huko au si kweli?”
Wolper: “Unajua bwana, mimi sina hela kama wanavyosema watu. Na haya yote yametokana na nilivyomsaidia Sajuki (Juma Kilowoko). Yule nilimsaidia kwa sababu niliguswa kutoka moyoni, lakini familia yangu yenyewe ina uhitaji mkubwa sana.
“Tena naomba jamii ielewe kuwa, sina ‘minoti’ ya kumwaga. Napata tabu watu wananifuata wakilia shida zao wakiamini nina fedha kibao, si kweli jamani.”


WOLPER VIPI?
Paparazi: “Umezungumza vizuri, lakini hujajibu suala la kujiunga na Freemason kama ni kweli au si kweli?”
Wolper: “Mimi gari si alininunulia Dallas, mbona nilishasema jamani au?”
Paparazi: “Sawa, ulishasema, vipi kuhusu Freemason sasa?”
Wolper: “Ni kwa sababu ya hizi nguo au? Maana nguo navaa bila kujua alama zake, sasa kama kuna za Freemason mimi nitajuaje jamani, ee?”


HAYA SASA
“Ila labda nikiri kitu kimoja, ni kweli niliwahi kuitwa na watu wakaniambia nijiunge kwenye imani hiyo, waliniahidi kwamba nikikubali maisha yangu yatakuwa mazuri na ulinzi wa afya yangu.”
Paparazi: “Ina maana hujajiunga unafikiria kwanza?”
Wolper: “We unaonaje, nijiunge au? Mimi sitaki nasikia wengi wameingia wanafanikiwa kwa kasi.”


MASWALI YA MHARIRI
Kama kweli Wolper si Freemason, amejuaje mavazi yake yana alama ya imani hiyo? Kwa nini anaomba ushauri huku anasema haitaki imani hiyo? Risasi Jumamosi linaendelea kumfuatilia kwa karibu kuhusu shughuli zake za mchana kutwa.
 

Attachments

  • d.jpg
    d.jpg
    69.6 KB · Views: 872
Fomu ya kujiunga na Freemason.




Kiongozi wa Freemasons Bongo, Sir Ande Chande.




Pete ya Freemasons.




Alama za Freemasons.




Jacqueline Wolper.





Marehemu Steven Kanumba.

Na Mwandishi Wetu

HATIMAYE fomu zenye maelekezo ya binadamu aliye tayari kujiunga na imani inayodaiwa ni ya kishetani ya Freemason inapatikana kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii huku ikizua kizaazaaa Bongo hasa kwa vijana wanaoamini ni njia ya kupata utajiri wa ghafla.

Ufukunyuku wa Ijumaa Wikienda umeiibua fomu hiyo yenye maelekezo kwa lugha ya Kiingereza ikimtaka mjazaji kuikabidhi ndani ya mtandao husika baada ya kuijaza.

MWONEKANO WA FOMU

Fomu hiyo nyeupe, juu ina rangi ya njano yenye maandishi ya utukufu kwa Mungu na ukamilifu wa kibinadamu (To the Glory of God and Perfection of Humanity).

Kushoto mwa fomu hiyo kuna picha ya mwanamke aliyesimama akiwa amenyoosha mkono ulioshika kitu chenye ncha kali kwa mwanaume aliyepiga magoti.

Inaonekana mwanaume huyo anaapishwa ili kuingia kwenye imani hiyo na pembeni kuna watu wamesimama wakishuhudia tukio hilo.

KUNA SIFA?

Sifa na masharti ambayo mwombaji anatakiwa kuwa nayo vinashangaza watu kwani baada ya mwombaji kuijaza, kuna mtu atampigia simu kwa ajili ya kujibu maswali ya mjazaji.
Kuhusu hilo kuna maelezo yanayosomeka:

If you are interested joining or just getting some more information, please fill out the form below and some one from order will contact you for your preference to answer any question you may have.
(Kama unapenda kujiunga au kupata maelezo zaidi, tafadhali jaza fomu hii chini na kuna mtu atawasiliana na wewe kwa ajili ya kujibu maswali yako yoyote uliyonayo).

KINACHOTAKIWA KUJAZWA


Hakuna makeke mengi kwenye fomu hiyo kama zilivyo za kugombea ubunge hivyo kufanya watu kumiminika mitandaoni kwa ajili ya kuijaza.

Fomu yenyewe inatakiwa kujazwa jina la kwanza na la pili. Mji anaoishi muombaji, mkoa na nchi.
Baada ya hapo, kuna sehemu inatakiwa kujazwa baruapepe (e-mail) na simu.
Aidha, kuna sehemu ya kuandika maoni kisha mwombaji anabonyeza mahali palipoandikwa submit (wasilisha).

FOMU YAZUA KIZAAZAA BONGO


Tangu kuibuka kwa wimbi la watu kudaiwa kujiunga na imani hiyo nchini, wasomaji wengi wa magazeti wamekuwa wakitaka kuwa wanachama.

Baadhi ya wasomaji hao wamekuwa wakipiga simu kwa namba za wahariri zinazopatikana magazetini wakiuliza wapi wanaweza kujiunga na Freemason.

Mfano mzuri juzi Jumamosi, msomaji mmoja ambaye hakuwa tayari kutaja jina, alipiga simu kwa wahiriri watatu wa Global, uhitaji wake ukiwa kuelekezwa sehemu ambayo ataweza kujiunga na imani hiyo yenye utata.

WACHUNGAJI MUWE MACHO


Kutokana na hali hiyo, iko sababu kwa watumishi wa Mungu (wachungaji) kufuatilia kwa makini imani hii na kuwafundisha waumini wao kama inakubalika kwa Mungu au la!
Wapo wanaodai Freemason si imani ya kishetani bali ni mahali ambapo mtu akijiunga anakuwa na maisha mazuri.
Hata hivyo, kuna madai kwamba ni imani ya kishetani ambapo ibada zake huambatana na kafara ya damu za wanyama, hususan mbuzi.

NINI KINAFUATWA FREEMASON?


Dalili zote zinaonesha kuwa wengi wanatamani kujiunga na imani hii si kwa sababu ya kuitafuta njia ya kweli na sahihi ya kufika kwa Mungu, bali tetesi ni kwamba ukiwa mwanachama wa Freemason utajiri njenje kama inavyodaiwa kuwatokea mastaa wa Kibongo, marehemu Steven Kanumba, Naseeb Abdul ‘Diamond’ na Jacqueline Wolper.
Utafiti wa Ijumaa Wikienda umebaini kuwa, Wabongo wengi wanatamani kuwa na maisha mazuri, nyumba na magari ya kifahari, hivyo wanaamini ni Freemason tu ndiyo itakayowakomboa.

FOMU YA KUJIUNGA FREEMASON - Global Publishers
 

Attachments

  • chandewafreemasons.jpg
    chandewafreemasons.jpg
    35.8 KB · Views: 705
  • fomu.jpg
    fomu.jpg
    66.4 KB · Views: 1,214
  • kanumba6.jpg
    kanumba6.jpg
    74.1 KB · Views: 820
  • freemasons.....jpg
    freemasons.....jpg
    16.9 KB · Views: 6,032
  • peteyafreemasons.jpg
    peteyafreemasons.jpg
    17.7 KB · Views: 881
  • jackwolper.jpg
    jackwolper.jpg
    44.9 KB · Views: 752
  • FREEMASONFORM.jpg
    FREEMASONFORM.jpg
    28.3 KB · Views: 962
Mtaongea mengi sana ila ukweli mitandao mingi ya kijamii inasambaza na kueneza uzushi na kutoa fomu ila hazijazwi kwenye mtandao hata iweje na 2B1ASK1
 
Fomu ya kujiunga na Freemason.




Kiongozi wa Freemasons Bongo, Sir Ande Chande.




Pete ya Freemasons.




Alama za Freemasons.




Jacqueline Wolper.





Marehemu Steven Kanumba.

Na Mwandishi Wetu

HATIMAYE fomu zenye maelekezo ya binadamu aliye tayari kujiunga na imani inayodaiwa ni ya kishetani ya Freemason inapatikana kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii huku ikizua kizaazaaa Bongo hasa kwa vijana wanaoamini ni njia ya kupata utajiri wa ghafla.

Ufukunyuku wa Ijumaa Wikienda umeiibua fomu hiyo yenye maelekezo kwa lugha ya Kiingereza ikimtaka mjazaji kuikabidhi ndani ya mtandao husika baada ya kuijaza.

MWONEKANO WA FOMU

Fomu hiyo nyeupe, juu ina rangi ya njano yenye maandishi ya utukufu kwa Mungu na ukamilifu wa kibinadamu (To the Glory of God and Perfection of Humanity).

Kushoto mwa fomu hiyo kuna picha ya mwanamke aliyesimama akiwa amenyoosha mkono ulioshika kitu chenye ncha kali kwa mwanaume aliyepiga magoti.

Inaonekana mwanaume huyo anaapishwa ili kuingia kwenye imani hiyo na pembeni kuna watu wamesimama wakishuhudia tukio hilo.

KUNA SIFA?

Sifa na masharti ambayo mwombaji anatakiwa kuwa nayo vinashangaza watu kwani baada ya mwombaji kuijaza, kuna mtu atampigia simu kwa ajili ya kujibu maswali ya mjazaji.
Kuhusu hilo kuna maelezo yanayosomeka:

If you are interested joining or just getting some more information, please fill out the form below and some one from order will contact you for your preference to answer any question you may have.
(Kama unapenda kujiunga au kupata maelezo zaidi, tafadhali jaza fomu hii chini na kuna mtu atawasiliana na wewe kwa ajili ya kujibu maswali yako yoyote uliyonayo).

KINACHOTAKIWA KUJAZWA


Hakuna makeke mengi kwenye fomu hiyo kama zilivyo za kugombea ubunge hivyo kufanya watu kumiminika mitandaoni kwa ajili ya kuijaza.

Fomu yenyewe inatakiwa kujazwa jina la kwanza na la pili. Mji anaoishi muombaji, mkoa na nchi.
Baada ya hapo, kuna sehemu inatakiwa kujazwa baruapepe (e-mail) na simu.
Aidha, kuna sehemu ya kuandika maoni kisha mwombaji anabonyeza mahali palipoandikwa submit (wasilisha).

FOMU YAZUA KIZAAZAA BONGO


Tangu kuibuka kwa wimbi la watu kudaiwa kujiunga na imani hiyo nchini, wasomaji wengi wa magazeti wamekuwa wakitaka kuwa wanachama.

Baadhi ya wasomaji hao wamekuwa wakipiga simu kwa namba za wahariri zinazopatikana magazetini wakiuliza wapi wanaweza kujiunga na Freemason.

Mfano mzuri juzi Jumamosi, msomaji mmoja ambaye hakuwa tayari kutaja jina, alipiga simu kwa wahiriri watatu wa Global, uhitaji wake ukiwa kuelekezwa sehemu ambayo ataweza kujiunga na imani hiyo yenye utata.

WACHUNGAJI MUWE MACHO


Kutokana na hali hiyo, iko sababu kwa watumishi wa Mungu (wachungaji) kufuatilia kwa makini imani hii na kuwafundisha waumini wao kama inakubalika kwa Mungu au la!
Wapo wanaodai Freemason si imani ya kishetani bali ni mahali ambapo mtu akijiunga anakuwa na maisha mazuri.
Hata hivyo, kuna madai kwamba ni imani ya kishetani ambapo ibada zake huambatana na kafara ya damu za wanyama, hususan mbuzi.

NINI KINAFUATWA FREEMASON?


Dalili zote zinaonesha kuwa wengi wanatamani kujiunga na imani hii si kwa sababu ya kuitafuta njia ya kweli na sahihi ya kufika kwa Mungu, bali tetesi ni kwamba ukiwa mwanachama wa Freemason utajiri njenje kama inavyodaiwa kuwatokea mastaa wa Kibongo, marehemu Steven Kanumba, Naseeb Abdul ‘Diamond’ na Jacqueline Wolper.
Utafiti wa Ijumaa Wikienda umebaini kuwa, Wabongo wengi wanatamani kuwa na maisha mazuri, nyumba na magari ya kifahari, hivyo wanaamini ni Freemason tu ndiyo itakayowakomboa.

FOMU YA KUJIUNGA FREEMASON - Global Publishers
Je hiyo fomu ntaipataje??
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom