Challenger
Member
- Sep 5, 2007
- 53
- 21
JF members,
Ni jambo lakusikitisha kuwa Afrika imempoteza mwanamuziki nguli, Freddy Mayaula Mayoni, tarehe 26 Mei 2010, ni siku ambayo Mayaula amemaliza maisha yake hapa duniani.
Mwandishi mzuri wa mashairi ya muziki na pia mpiga gita la kati (rythim), pamoja na mwanasoka aliyewahi kuchezea klabu ya Yanga, amefariki Brussels Ubeligiji akiwa baada ya kuugua kwa muda mrefu kutokana na ugonjwa wa kiharusi (stroke); ambayo ilimpata akiwa hapa Tanzania (Dar-es-salaam) miaka ya 2006.
Wengi, uhusuani wale wapenzi wa Franco akiwa na bendi yake ya TP OK Jazz, watamkumbuka Mayaula kutokana na album zake hasa ile ya Mizele iliyotolewa miaka ya 1990 na L'Amour Au Kilo iliyotolewa miaka ya 1993 ikiwa na wimbo uliopendwa Mbongo. Nyimbo nyingine alizowahi kutunga akiwa na TOP OK Jazz ni kama Nabari Misere (ambao uliimbwa kwa ufundi mkubwa na mwanamuziki mwingine ambaye pia ni marehemu, Djo Mpoy Kaninda), na pia wimbo Cherie Bondowe.
Mwanamuziki Freddy Mayaula Mayoni amefariki akiwa na umri wa miaka 64, akiungana na wanamuziki wengine aliowahi kupiga nao akiwa na bendi ya TP OK Jazz kama Madilu System, Franco, Djo Mpoy Kaninda, Aime Kiwanaka, Dalienst Ya Ntesa, Lola Checain, Decca Mpudi, Gerry Dialungana, Mongo, Ntoya Pajos, Empopo Loway, Issack Musekiwa, Rondot Kasongo nikiwataja kwa uchache.
Mungu aiweke Roho Ya Marehemu Freddy Mayaula Mayoni mahali pema Peponi AMENI
Kisondella
Ni jambo lakusikitisha kuwa Afrika imempoteza mwanamuziki nguli, Freddy Mayaula Mayoni, tarehe 26 Mei 2010, ni siku ambayo Mayaula amemaliza maisha yake hapa duniani.
Mwandishi mzuri wa mashairi ya muziki na pia mpiga gita la kati (rythim), pamoja na mwanasoka aliyewahi kuchezea klabu ya Yanga, amefariki Brussels Ubeligiji akiwa baada ya kuugua kwa muda mrefu kutokana na ugonjwa wa kiharusi (stroke); ambayo ilimpata akiwa hapa Tanzania (Dar-es-salaam) miaka ya 2006.
Wengi, uhusuani wale wapenzi wa Franco akiwa na bendi yake ya TP OK Jazz, watamkumbuka Mayaula kutokana na album zake hasa ile ya Mizele iliyotolewa miaka ya 1990 na L'Amour Au Kilo iliyotolewa miaka ya 1993 ikiwa na wimbo uliopendwa Mbongo. Nyimbo nyingine alizowahi kutunga akiwa na TOP OK Jazz ni kama Nabari Misere (ambao uliimbwa kwa ufundi mkubwa na mwanamuziki mwingine ambaye pia ni marehemu, Djo Mpoy Kaninda), na pia wimbo Cherie Bondowe.
Mwanamuziki Freddy Mayaula Mayoni amefariki akiwa na umri wa miaka 64, akiungana na wanamuziki wengine aliowahi kupiga nao akiwa na bendi ya TP OK Jazz kama Madilu System, Franco, Djo Mpoy Kaninda, Aime Kiwanaka, Dalienst Ya Ntesa, Lola Checain, Decca Mpudi, Gerry Dialungana, Mongo, Ntoya Pajos, Empopo Loway, Issack Musekiwa, Rondot Kasongo nikiwataja kwa uchache.
Mungu aiweke Roho Ya Marehemu Freddy Mayaula Mayoni mahali pema Peponi AMENI
Kisondella