Game Theory
Platinum Member
- Sep 5, 2006
- 8,545
- 835
Ndugu zangu JF,
Nimefuatilia mjadala wa Kauli yangu juu ya kifo cha Osama bin Laden katika jukwaa hili na hata nje yake na kugundua mambo kadhaa ambayo nastahili kuyaweka wazi yakaeleweka vema kwenu na wadau wengine. Moja kati ya vilivyojitokeza ni uimara wenu katika kudai, kuhamasisha na kuhimiza haki za binadamu pale mlipo na hata baada ya hapo; jingine ni namna mlivyo na matumaini makubwa juu ya kazi ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, LHRC.
Nimejifunza toka mjadala huu kuwa mko makini kujua na kufuatilia HAKI za binadamu bila kujali tofauti eyote miongoni mwa binadamu na namna wengine wanavyoweza kuwahukumu. Naheshimu mawazo yenu kwani mmetimiza wajibu wenu wa Kikatiba. Kwa msingi wa mjadala huu pia nimependelea nitoe ufafanuzi wa maneno niliyonukuliwa na BBC juzi jioni (03 Mei 2011) na kusikika jana (04 Mei 2011) asubuhi ambayo ndiyo yaliyozua mjadala mkali hapa JF. Ukweli ni kuwa maneno yaliyonukuliwa hayakuwa yenye maana ya kujitosheleza:
( kuuwawa kwa Osama kunaweza kuwa sawa kwa kuzingatia mazingira yake.)
Kichwani mwangu nilikuwa nawaza je, kwa kuzingatia mazingira ya suala hilo kulikuwa na nafasi ya kumkamata Osama/ au yeye mwenyewe kujitokeza katika vyombo vya sheria ili utawala wa sheria uchukue nafasi yake?
Maneno hayo yalitanguliwa na maneno:
ni vigumu kushangilia kifo cha mtu yeyote na msimamo wetu kupinga ukiukwaji wa haki za binadamu pia ni wajibu wa kila kulinda na kutetea haki za binadamu na kuifanya dunia ni mahali bora pa kuishi
Katika mahajiano yale, niliweka wazi siungi mkono kwa namna eyote kuuwawa kwa binadamu yeyote, achilia mbali Osama bin Laden. Na labda nirudia kusema pia kuwa hatushangilii kifo cha Osama na pia hatuungi mkono ugaidi na matendo ya kigaidi ambayo lengo lake ni kuleta hofu na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu duniani,. Huu ndio uelewa wangu.
Nawasilisha.
Francis Kiwanga
Francis K. Kiwanga
Executive Director
Legal and Human Rights Centre-LHRC
P.O.Box 75254
Dar es salaam
email; fkiwanga@humanrights.or.tz
Phone; +255 22 2773038/48
Mobile;+255 787 229933
My life is my message M. Ghandi
Nimefuatilia mjadala wa Kauli yangu juu ya kifo cha Osama bin Laden katika jukwaa hili na hata nje yake na kugundua mambo kadhaa ambayo nastahili kuyaweka wazi yakaeleweka vema kwenu na wadau wengine. Moja kati ya vilivyojitokeza ni uimara wenu katika kudai, kuhamasisha na kuhimiza haki za binadamu pale mlipo na hata baada ya hapo; jingine ni namna mlivyo na matumaini makubwa juu ya kazi ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, LHRC.
Nimejifunza toka mjadala huu kuwa mko makini kujua na kufuatilia HAKI za binadamu bila kujali tofauti eyote miongoni mwa binadamu na namna wengine wanavyoweza kuwahukumu. Naheshimu mawazo yenu kwani mmetimiza wajibu wenu wa Kikatiba. Kwa msingi wa mjadala huu pia nimependelea nitoe ufafanuzi wa maneno niliyonukuliwa na BBC juzi jioni (03 Mei 2011) na kusikika jana (04 Mei 2011) asubuhi ambayo ndiyo yaliyozua mjadala mkali hapa JF. Ukweli ni kuwa maneno yaliyonukuliwa hayakuwa yenye maana ya kujitosheleza:
( kuuwawa kwa Osama kunaweza kuwa sawa kwa kuzingatia mazingira yake.)
Kichwani mwangu nilikuwa nawaza je, kwa kuzingatia mazingira ya suala hilo kulikuwa na nafasi ya kumkamata Osama/ au yeye mwenyewe kujitokeza katika vyombo vya sheria ili utawala wa sheria uchukue nafasi yake?
Maneno hayo yalitanguliwa na maneno:
ni vigumu kushangilia kifo cha mtu yeyote na msimamo wetu kupinga ukiukwaji wa haki za binadamu pia ni wajibu wa kila kulinda na kutetea haki za binadamu na kuifanya dunia ni mahali bora pa kuishi
Katika mahajiano yale, niliweka wazi siungi mkono kwa namna eyote kuuwawa kwa binadamu yeyote, achilia mbali Osama bin Laden. Na labda nirudia kusema pia kuwa hatushangilii kifo cha Osama na pia hatuungi mkono ugaidi na matendo ya kigaidi ambayo lengo lake ni kuleta hofu na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu duniani,. Huu ndio uelewa wangu.
Nawasilisha.
Francis Kiwanga
Francis K. Kiwanga
Executive Director
Legal and Human Rights Centre-LHRC
P.O.Box 75254
Dar es salaam
email; fkiwanga@humanrights.or.tz
Phone; +255 22 2773038/48
Mobile;+255 787 229933
My life is my message M. Ghandi