Francis Godwin Alivyofanyiwa unyama na Polisi iringa

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,883
6,884
IMG_9731.JPG

Awali ya yote ninapenda kumshukuru Mungu aliyenileta duniani na atakayenitoa hapa duniani,Ndungu zandu na wadau zangu wapendwa nitakuwa si mpiganaji wa kweli kama nitabaki na siri hii ya kukamatwa kwangu na jeshi la polisi na pia sitakuwa muungwana kama nisipowashukuru wote kwa dua zenu hadi nimeachiwa huru.

Ninaomba kwa sehemu niweze kuelezea yaliyonikuta hadi nikakamatwa na polisi ilikuwa ni jumanne ya Mei 31 majira ya saa 7.45 eneo la shule ya sekondari Tosamaganga wakati nikitoka kufuatilia sakata la mgomo wa wanafunzi ndipo nilipokamatwa na askari wa upelelezi watatu . Dalili za kuwepo kukamatwa zilianza kujionyesha toka jumatatu ya mei 30 eneo la Mseke wakati nikiwa na mwenzangu wa Radio Ebony Fm ambapo mkuu wa polisi wilaya ya Iringa alitupiga stop kuendelea kufuatilia sakata la FFU kuwapiga mabomu wa wanafunzi wa sekondari ya Tosamaganga bila kuwa na kibali cha polisi . kutokana na kiongozi huyo wa polisi wilaya kututaka kuomba kuifanya kazi hiyo tulilazimika kuondoka na kwenda kuripoti tukio la wanafunzi hao kugoma katika vyombo vya habari ukiwemo mtandao huu wa Francis Godwin ni mzee wa matukio daima.


" Kabla ya kuondoka eneo la tukio kijiji cha Mseke mpakani mwa Iringa vijijini na mjini ambako wanafunzi hao zaidi ya 1000 walitawanywa na FFU kwa mabomu tulipata kumuuliza mkuu huyo wa Polisi aina ya vibali ambavyo vinatolewa na jeshi la polisi kwa waandishi wa habari wanapotakiwa kufuatilia tukio " Hata hivyo siku ya pili ambayo ni jumanne Mai 31 majira ya saa 7.45 nikiwa katika shule ya sekondari Tosamaganga kufuatilia hali ya mgomo huo ghafla alizingirwa na polisi wa upelelezi ambao waliziba barabara na kunishusha katika gari kwa nguvu huku wenzangu wawili akiwemo wa Radio Ebony na ITV wakiachwa .

"Pamoja na madai hayo nilishangazwa hatua ya askari mmoja ambaye anaitwa Mrisho kwa kuanza kunitukana matusi ya nguoni na kudai kuwa mimi nimejifanya mjuaji na kupitia gazeti la Tanzania Daima na blogu ya Francis Godwin nimeonyesha tukio la wao kuwapiga mabomu wanafunzi hao na tukio jingine alilonihusisha ni lile la madai ya polisi kudaiwa kumpiga kwa risasi mwanamke mmoja mkazi wa Don Bosco " Pamoja na askari huyo Mrisho kutishia kuwa angempiga sana ila hakuweza kufanya hivyo baada ya kuwasiliana na wakuu wake ambao wamemtaka asinipige wala kunitesa kwa namna yeyote ile.


Baada ya kukamatwa nikiwa eneo la shule hiyo alipelekwa kituo kidogo cha polisi Tosamaganga na baadae kupakizwa katika gari iliyokuwa na askari wa FFU zaidi ya 10 huku wakipiga king'ora mfano njia nzima na kumfikisha kituo cha polisi mfano wa jambazi sugu amekamatwa na baada ya kufika mkuu wao aliagiza niwekwa mahabusu bila maelezo kwa zaidi ya masaa mawili.

Majira ya saa 12.49 ndipo mwandishi wa habari za Chanel Ten mkoa wa Iringa Daud Mwangosi na mwandishi wa gazeti la Majira mkoa wa Iringa Eliasa Ally walifika kituoni hapo kwa ajili ya kuniwekea dhamana na ndipo nilipotoa maelezo yangu kuelezea mazingira ya kukamatwa japo katika maelezo hayo sehemu ya kosa haikujazwa chochote zaidi ya askari aliyokuwa akichukua maelezo kudai kuwa kosa ni kuwaonyesha wanafunzi hao zaidi ya 1000 askari wawili wa upelelezi na dhamana ya shilingi milioni 1 ipo wazi.

"Nikiwa ndani ya gari ya FFU baadhi ya askari walikuwa wakinihoji ili kujua kama ni mfuasi wa Chadema na kuwa wao walielezwa kuwa nimetumwa na Chadema katika shule hiyo huku wengine wakitoa vitisho kuwa yaliyompata Jerry Muro na Said Kubenea ndio wanayotaka kunifanyia mimi"

Maelezo ya polisi na yale ya kamanda wa polisi mkoa kwa vyombo vya habari yalionyesha kutofautiana baada ya polisi kudaiwa kuwaonyesha wanafunzi askari wa upelelezi na kuhatarisha maisha yao huku kamanda wa polisi akidai kuwa sababu ya kushikiliwa na polisi ni kuchochea mgomo wa wanafunzi.

"Hata nawashukuru wanahabari ndani ya mkoa wa Iringa na Tanzania kwa ujumla kwa kulishughulikia suala hilo kwa uzito wake pamoja ....pia namshukuru mkuu wa polisi wilaya (OCD) Semunyu kwa kuniachia huru na kunitaka kuendelea na kazi yangu kwa amani"
 
Tanzania inaendeshwa na sheria za kikwete na jeshi. Watanzania bado hatujua na kukubali haya na matokeo yake sio haya tunaona sheria zilivyo na zinavyofanya kazi. Tufanye kazi kubwa sasa kuziondoa kwa nguvu kuanzia leo na wiki hii nzima.

Fundisho la kikwete ndio wiki hii mjulishe mwenzio na hakikisha uwajulishe hata ndugu zako kwenye jeshi la polisi waelezeni wasiende kazini wataajiriwa upya kwenye serikali mpya ya Tanzania baada ya serikali mpya.
 
Pole sana mkuu ila naona kama umeandika kuhusu mtu mwingine na sehemu nyingine umeandika kwamba ni wewe so hapo sijaelewa ila zaidi pole sana, na huyo askari kama angekuwa mwenyewe ungemchapa makonde tu maana hawana adabu kabisa..........
 
Duh, pole mkuu. Kwa mtu ambaye hajawahi kukutana na mkono wa polisi daima atawatetea polisi kwamba wanafanya kazi nzuri. Lakini kwa mtu kama mimi niliyewahi kukamatwa bila kosa, nikalala rumande na siku ya pili nikatolewa kwa hela, ninawachukia polisi kupita kawaida. Maana huwa sioni kabisa msaada wao zaidi ya kuongeza foleni za magari tu wanapoamua kujifanya taa za barabarani. Yaani polisi wa tanzania ni aina nyingine ya majambazi tunaotakiwa kuanza kukabiliana nao. Maana wanashindwa kukamata vibaka na majambazi wanaishia kukamata watu wasio na hatia na kuwaua pamoja na kuwasababishia stress zisizo za lazima.
 
Pole sana mkuu. Ila uliyemtaja kwenye heading ni tofauti na unayemzungumzia.
 
IMG_9731.JPG

Awali ya yote ninapenda kumshukuru Mungu aliyenileta duniani na atakayenitoa hapa duniani,Ndungu zandu na wadau zangu wapendwa nitakuwa si mpiganaji wa kweli kama nitabaki na siri hii ya kukamatwa kwangu na jeshi la polisi na pia sitakuwa muungwana kama nisipowashukuru wote kwa dua zenu hadi nimeachiwa huru.

Ninaomba kwa sehemu niweze kuelezea yaliyonikuta hadi nikakamatwa na polisi ilikuwa ni jumanne ya Mei 31 majira ya saa 7.45 eneo la shule ya sekondari Tosamaganga wakati nikitoka kufuatilia sakata la mgomo wa wanafunzi ndipo nilipokamatwa na askari wa upelelezi watatu . Dalili za kuwepo kukamatwa zilianza kujionyesha toka jumatatu ya mei 30 eneo la Mseke wakati nikiwa na mwenzangu wa Radio Ebony Fm ambapo mkuu wa polisi wilaya ya Iringa alitupiga stop kuendelea kufuatilia sakata la FFU kuwapiga mabomu wa wanafunzi wa sekondari ya Tosamaganga bila kuwa na kibali cha polisi . kutokana na kiongozi huyo wa polisi wilaya kututaka kuomba kuifanya kazi hiyo tulilazimika kuondoka na kwenda kuripoti tukio la wanafunzi hao kugoma katika vyombo vya habari ukiwemo mtandao huu wa Francis Godwin ni mzee wa matukio daima.


" Kabla ya kuondoka eneo la tukio kijiji cha Mseke mpakani mwa Iringa vijijini na mjini ambako wanafunzi hao zaidi ya 1000 walitawanywa na FFU kwa mabomu tulipata kumuuliza mkuu huyo wa Polisi aina ya vibali ambavyo vinatolewa na jeshi la polisi kwa waandishi wa habari wanapotakiwa kufuatilia tukio " Hata hivyo siku ya pili ambayo ni jumanne Mai 31 majira ya saa 7.45 nikiwa katika shule ya sekondari Tosamaganga kufuatilia hali ya mgomo huo ghafla alizingirwa na polisi wa upelelezi ambao waliziba barabara na kunishusha katika gari kwa nguvu huku wenzangu wawili akiwemo wa Radio Ebony na ITV wakiachwa .

"Pamoja na madai hayo nilishangazwa hatua ya askari mmoja ambaye anaitwa Mrisho kwa kuanza kunitukana matusi ya nguoni na kudai kuwa mimi nimejifanya mjuaji na kupitia gazeti la Tanzania Daima na blogu ya Francis Godwin nimeonyesha tukio la wao kuwapiga mabomu wanafunzi hao na tukio jingine alilonihusisha ni lile la madai ya polisi kudaiwa kumpiga kwa risasi mwanamke mmoja mkazi wa Don Bosco " Pamoja na askari huyo Mrisho kutishia kuwa angempiga sana ila hakuweza kufanya hivyo baada ya kuwasiliana na wakuu wake ambao wamemtaka asinipige wala kunitesa kwa namna yeyote ile.


Baada ya kukamatwa nikiwa eneo la shule hiyo alipelekwa kituo kidogo cha polisi Tosamaganga na baadae kupakizwa katika gari iliyokuwa na askari wa FFU zaidi ya 10 huku wakipiga king'ora mfano njia nzima na kumfikisha kituo cha polisi mfano wa jambazi sugu amekamatwa na baada ya kufika mkuu wao aliagiza niwekwa mahabusu bila maelezo kwa zaidi ya masaa mawili.

Majira ya saa 12.49 ndipo mwandishi wa habari za Chanel Ten mkoa wa Iringa Daud Mwangosi na mwandishi wa gazeti la Majira mkoa wa Iringa Eliasa Ally walifika kituoni hapo kwa ajili ya kuniwekea dhamana na ndipo nilipotoa maelezo yangu kuelezea mazingira ya kukamatwa japo katika maelezo hayo sehemu ya kosa haikujazwa chochote zaidi ya askari aliyokuwa akichukua maelezo kudai kuwa kosa ni kuwaonyesha wanafunzi hao zaidi ya 1000 askari wawili wa upelelezi na dhamana ya shilingi milioni 1 ipo wazi.

"Nikiwa ndani ya gari ya FFU baadhi ya askari walikuwa wakinihoji ili kujua kama ni mfuasi wa Chadema na kuwa wao walielezwa kuwa nimetumwa na Chadema katika shule hiyo huku wengine wakitoa vitisho kuwa yaliyompata Jerry Muro na Said Kubenea ndio wanayotaka kunifanyia mimi"

Maelezo ya polisi na yale ya kamanda wa polisi mkoa kwa vyombo vya habari yalionyesha kutofautiana baada ya polisi kudaiwa kuwaonyesha wanafunzi askari wa upelelezi na kuhatarisha maisha yao huku kamanda wa polisi akidai kuwa sababu ya kushikiliwa na polisi ni kuchochea mgomo wa wanafunzi.

"Hata nawashukuru wanahabari ndani ya mkoa wa Iringa na Tanzania kwa ujumla kwa kulishughulikia suala hilo kwa uzito wake pamoja ....pia namshukuru mkuu wa polisi wilaya (OCD) Semunyu kwa kuniachia huru na kunitaka kuendelea na kazi yangu kwa amani"

Hizi sera za utanda wazi ni porojo au ni mask? Kama vyombo vya dola vinafanya haki kwa nini vizuie vyombo vya habari kufuatilia habari za matukio?
 
Pole sana mkuu. Ila uliyemtaja kwenye heading ni tofauti na unayemzungumzia.

Yeah mkuu ni vizuri kama angechange heading maana hata mimi hapo juu sijamuelewa vizuri.....
 
Pole sana kaka Mungu akutie nguvu na hiyo iwe filimbi ya kusonga mbele kwa haki zaidi; hakuna historia inayoandikwa kwa mtu kuwa lelemama au goigoi; ndio maana hata akina kimweri; kinjekitile na wengineo wanakumbukwa maana walisimama imara bila kujali; after all hata wenye mibunduki watakufa tena kifo kibaya tu siku moja huenda wakakuacha au ukawaacha njia ni moja; pole sana mkuu
 
Godwin ukiona hivyo ujue ujumbe umefika na since unafanya kazi kwa Maslahi ya Watanzania songa mbele tupo nyuma yako na kazi yako tunaikubali sana.
 
Polisi wanajifanya kana kwamba wao wana ishi maisha standard sana, kumbe wanaishi kwenye mabanda ya kufugia njiwa tena vyumba vyenyewe utazania ni gest.

Wao wanafanya kazi kwa minajiri ya mafisadi na hamna wanacho faidi. Wakimbizi wa kule ngala wanaishi sehemu nzuri kuliko hawa mapolisi wetu.
 
Hii andika barua kwa KOVA. Alafu tutaendelea kufuatilia hili swala kwa hali na mali...
 
Rais JK anaendekeza udini.
Watu wanauwawa TARIME,MBEYA na ila haimuumi kwa sababu wanaokufa si waislam wenzie

Maeneo hayo yana wakristo kwa wingi so ni sawa kabisa kusema rais haumizwi na vifo vya wasio waislam.
Alipokufa sheikh yahya (mtu mmoja ) rais alihudhuria mazishi kisa UISLAM.

mimi ni CCM damdamu ila sipendezwi na move za udini wa JK.ikilazimu ntahamia NCCR
 
..aluta continua, ukombozi umekaribia, soon uta-enjoy harakati zako mkuu, siwezi kukupa pole, ila nakuomba uzidishe harakati!!!!
 
Polisi ni kama mbwa tu, wameumbwa kwa ajili ya kukimbia kimbia na kukimbiza binadamu wenzao, siamini kamawana uwezo wa kufika hata kwenye hii mitandao ya kijamii, watu wana lala nje maisha yao yote hawana tofauti na wanyama, ni heri walipwe misha hara duni ili wasijikimu kimaisha waendelee kuzaa mapolisi wenginie sidhani kama kwa msha hara wao kama wana hata uwezo wa kusomesha watoto wao, wana ishi kwa rushwa tu hawa, na kutii amri. Its only dog that he who obey, they dont get time to value their opinion
 
pole sana mkuu ukitaka kujua jinsi askari wetu wanavyotumia tumbo kufikiri badala ya ubongo ndo hapo
kama traffic anaweza kuacha eneo lake la kazi na kuhangaika na mtu mmoja siku nzima na kuacha wengine wakivunja sheria
kisa tu anataka sh elfu 10 ,,,,,
 
Back
Top Bottom