Na Padri Privatus Karugendo
KABLA ya mauaji ya kimbali yaliyotokea kule Rwanda, nilikuwa nimezeoa kutembelea nchi hiyo na hasa mji mkuu wa Kigali. Kati ya mambo niliyokuwa nikiyafurahia kwenye nchi hiyo yenye vilima vingi na vivutio visivyokuwa na idadi ni magazeti yaliyokuwa yakifanya uchambuzi katika mtindo wa kuuma na kuvuvia; mtindo wa kutawaliwa na unafiki na kuwalazimisha waandishi kubuni mbinu za kuandika kwa mafumbo.
Mwanzoni mwa miaka ya tisini, magazeti ya Rwanda na hasa la Kinyamateka,(gazeti la kanisa katoliki) nililokuwa nikipenda kulisoma nikiwa Kigali, yalianza kuandika habari zilizokuwa na mwelekeo wa kujenga utamaduni wa kutoaminiana. Iliandikwa kwa mafumbo- lakini fumbo mfumbie mjinga.
Sisi tuliokuwa wageni, hatukuweza kuelewa vizuri mafumbo yale, wale wandani walielewa; wenye kupenda kusikiliza walitambua na kuzisoma alama za nyakati; wenye uwezo wao walitimuka na kujificha nchi za nje baada ya mauaji, ndo ujumbe ulikuwa wazi. Ndo tulitambua na kuelewa kazi kubwa iliyokuwa ikifanywa na vyombo vya habari vya wakati ule kule Rwanda.
Ajali za barabarani na hasa zile zilizosababisha vifo vya viongozi wa serikali au wafanyabiashara mashuhuri kule Rwanda enzi zile zilihusishwa na njama za Akazu. Neno hili la Kinyarwanda ambalo ni aina ya fumbo, au kuipamba lugha kwa lengo la kuelezea kitu kikubwa, linamaanisha Kanyumba, lakini si Kanyumba ka kawaida, si Kanyumba ka nyasi wala udongo, ni Kanyumba ka aina yake labda kwa maneno ya kueleweka, Kanyumba ka dhahabu.
Hili lilikuwa ni kundi dogo la Wanyarwanda waliokuwa wameshika Utamu wote wa Rwanda: Walikuwa na madaraka, walikuwa na fedha, walitawala uchumi, walitawala siasa, walitawala utamaduni, walitawala Utu na walitawala dini! Hakuna aliyeingia kwenye Akazu bila kitambulisho. Si kila Mnyarwanda, aliruhusiwa kuingia kwenye Kanyumba. Si kila aliyekuwa serikalini aliruhusiwa kuingia kwenye Akazu. Kulikuwa na wateule wachache ndani ya serikali, wateule wachache ndani ya chama tawala, wateule wachache wafanyabiashara na wateule wachache viongozi wa dini; walimzunguka Rais wa nchi ya Rwanda na kupenyeza ushawishi wao kwa kila maamuzli aliyokuwa akiyafanya Rais wa nchi. Mfumo huu wa Akazu ulitengeneza utamaduni wa kutoaminiana. Ulianzisha matabaka na kuchochea ubaguzi wa kutisha.
Ajali za barabarani zilizosababisha vifo vya watu mashuhuri, kidole kilinyoshwa kwa Akazu. Nakumbuka kusoma makala kwenye gazeti la Kinyamateka, iliyokuwa ikichambua mwenendo wa mambo katika nchi ya Rwanda kwa wakati ule, kwamba ilifikia mahali ambapo hata kama mtu angekufa kwa ugonjwa kama vile malaria, watu wasingeamini kama ni kifo cha kawaida. Kidole kilinyoshwa kwa Akazu.
Iliaminika kwamba wale waliokuwa ndani ya Akazu walikuwa na uwezo wa kumpoteza mtu aliyetaka kusambaratisha Kanyumba kao; hivyo walitengeneza ajali, walitengeneza magonjwa na walikuwa na uwezo wa kuua kwa njia zozote zile; sumu, risasi, kunyonga nk.; kichocheo cha kulinda uhai wa Akazu ni madaraka milele, ni uchu wa watu wachache kutaka kumiliki uchumi wa nchi nzima: Imani kubwa ilikuwa kwamba Akazu ulikuwa mfumo wa kudumu kilele yote:Walijigamba, walitamba, walijivuna na kulazimisha watukuzwe.
Sina lengo la kuandika juu ya Mauaji ya Kimbali. Yaliyotokea tunayafahamu sote. Akazu ni mfumo uliosambaratishwa na kupotea kabisa. Maana yake hakuna mfumo wa kudumu milele; maana yake kuna mwisho wa uchu wa madaraka, kuna mwisho wa watu wachache kutaka kumiliki uchumi wa nchi nzima.
Katika Taifa letu Tanzania, kumezuka mwelekeo wa kujenga utamaduni wa kutaoaminiana kama ilivyokuwa Rwanda kwenye miaka ya tisini. Mbali na nyimbo za rushwa, ufisadi papa na ufisadi nyangumi, kuna matukio ya vifo na ajali za waheshimiwa, ambavyo vinaonyesha dalili zote za kutoaminiana. Akifa mtu anatafutwa mchawi. Hata kifo hicho kama ni cha ugonjwa wa wazi kama malaria,TB au UKIMWI, anatafutwa mchawi. Kama mchawi si Mafisadi, basi ni CCM au vyama vya upinzani.
CHANZO: kwanzajamii.com
KABLA ya mauaji ya kimbali yaliyotokea kule Rwanda, nilikuwa nimezeoa kutembelea nchi hiyo na hasa mji mkuu wa Kigali. Kati ya mambo niliyokuwa nikiyafurahia kwenye nchi hiyo yenye vilima vingi na vivutio visivyokuwa na idadi ni magazeti yaliyokuwa yakifanya uchambuzi katika mtindo wa kuuma na kuvuvia; mtindo wa kutawaliwa na unafiki na kuwalazimisha waandishi kubuni mbinu za kuandika kwa mafumbo.
Mwanzoni mwa miaka ya tisini, magazeti ya Rwanda na hasa la Kinyamateka,(gazeti la kanisa katoliki) nililokuwa nikipenda kulisoma nikiwa Kigali, yalianza kuandika habari zilizokuwa na mwelekeo wa kujenga utamaduni wa kutoaminiana. Iliandikwa kwa mafumbo- lakini fumbo mfumbie mjinga.
Sisi tuliokuwa wageni, hatukuweza kuelewa vizuri mafumbo yale, wale wandani walielewa; wenye kupenda kusikiliza walitambua na kuzisoma alama za nyakati; wenye uwezo wao walitimuka na kujificha nchi za nje baada ya mauaji, ndo ujumbe ulikuwa wazi. Ndo tulitambua na kuelewa kazi kubwa iliyokuwa ikifanywa na vyombo vya habari vya wakati ule kule Rwanda.
Ajali za barabarani na hasa zile zilizosababisha vifo vya viongozi wa serikali au wafanyabiashara mashuhuri kule Rwanda enzi zile zilihusishwa na njama za Akazu. Neno hili la Kinyarwanda ambalo ni aina ya fumbo, au kuipamba lugha kwa lengo la kuelezea kitu kikubwa, linamaanisha Kanyumba, lakini si Kanyumba ka kawaida, si Kanyumba ka nyasi wala udongo, ni Kanyumba ka aina yake labda kwa maneno ya kueleweka, Kanyumba ka dhahabu.
Hili lilikuwa ni kundi dogo la Wanyarwanda waliokuwa wameshika Utamu wote wa Rwanda: Walikuwa na madaraka, walikuwa na fedha, walitawala uchumi, walitawala siasa, walitawala utamaduni, walitawala Utu na walitawala dini! Hakuna aliyeingia kwenye Akazu bila kitambulisho. Si kila Mnyarwanda, aliruhusiwa kuingia kwenye Kanyumba. Si kila aliyekuwa serikalini aliruhusiwa kuingia kwenye Akazu. Kulikuwa na wateule wachache ndani ya serikali, wateule wachache ndani ya chama tawala, wateule wachache wafanyabiashara na wateule wachache viongozi wa dini; walimzunguka Rais wa nchi ya Rwanda na kupenyeza ushawishi wao kwa kila maamuzli aliyokuwa akiyafanya Rais wa nchi. Mfumo huu wa Akazu ulitengeneza utamaduni wa kutoaminiana. Ulianzisha matabaka na kuchochea ubaguzi wa kutisha.
Ajali za barabarani zilizosababisha vifo vya watu mashuhuri, kidole kilinyoshwa kwa Akazu. Nakumbuka kusoma makala kwenye gazeti la Kinyamateka, iliyokuwa ikichambua mwenendo wa mambo katika nchi ya Rwanda kwa wakati ule, kwamba ilifikia mahali ambapo hata kama mtu angekufa kwa ugonjwa kama vile malaria, watu wasingeamini kama ni kifo cha kawaida. Kidole kilinyoshwa kwa Akazu.
Iliaminika kwamba wale waliokuwa ndani ya Akazu walikuwa na uwezo wa kumpoteza mtu aliyetaka kusambaratisha Kanyumba kao; hivyo walitengeneza ajali, walitengeneza magonjwa na walikuwa na uwezo wa kuua kwa njia zozote zile; sumu, risasi, kunyonga nk.; kichocheo cha kulinda uhai wa Akazu ni madaraka milele, ni uchu wa watu wachache kutaka kumiliki uchumi wa nchi nzima: Imani kubwa ilikuwa kwamba Akazu ulikuwa mfumo wa kudumu kilele yote:Walijigamba, walitamba, walijivuna na kulazimisha watukuzwe.
Sina lengo la kuandika juu ya Mauaji ya Kimbali. Yaliyotokea tunayafahamu sote. Akazu ni mfumo uliosambaratishwa na kupotea kabisa. Maana yake hakuna mfumo wa kudumu milele; maana yake kuna mwisho wa uchu wa madaraka, kuna mwisho wa watu wachache kutaka kumiliki uchumi wa nchi nzima.
Katika Taifa letu Tanzania, kumezuka mwelekeo wa kujenga utamaduni wa kutaoaminiana kama ilivyokuwa Rwanda kwenye miaka ya tisini. Mbali na nyimbo za rushwa, ufisadi papa na ufisadi nyangumi, kuna matukio ya vifo na ajali za waheshimiwa, ambavyo vinaonyesha dalili zote za kutoaminiana. Akifa mtu anatafutwa mchawi. Hata kifo hicho kama ni cha ugonjwa wa wazi kama malaria,TB au UKIMWI, anatafutwa mchawi. Kama mchawi si Mafisadi, basi ni CCM au vyama vya upinzani.
CHANZO: kwanzajamii.com