technology ya zamani hiyo mkuu...siku hizi kuna materials zinaitwa "Melamine boards" na "MDF boards" zinakuwa na profile ya Formica at the facing side
Heshima mbelee mkuu LAT, nakukubali sana mkuu! Hizo boards huwa haziniridhishi ubora wake mkuu, labda kama zinatofautiana quality! Mfano mtu unataka kitu cha harwood mtipori halisi, lakini pale juu unataka kuweka material ambayo itazuia scratch na kupendezesha zaidi, hauoni kwamba hizo "fomaika" zinafaa zaidi? Au kama mtu anataka kutengeneza kitu kama makabati ya jikoni kwa kutumia mbao za kawaida kwa uimara, lakini anataka jiko liwe mordenish, huoni kuwa ni wazo zuri kutumia fomaika? Mawazo zaidi mkuu, kama kuna fundi seremala ashushe mawazo pia.
mkuu Amoeba .... Kitu cha hardwood huwezi kuweka formica utapoteza intrinsic value yake ...imagine mninga/mvule/mkongo au panga panga unaiweka formica juu yake .... itakuwa ni waste of resources ... hivyo formica matumizi yake ni kwenye boards na softwoods .... hivyo basi wenzetu wameamua kurahisisha matumizi kwa kuziunganisha zote kwa pamoja
kumbuka kwamba kuna matumizi ya aina mbali mbali na matumizi yote pia yana materials ambazo ni tofauti pia
sehemu zilizo dry kama book shelves na wadropbes za nguo boards zinazotumika ni normal ... lakini wet areas kama kitchens/kitchenettes tunatumia water resistant boards ... hata gypsum boards zipo ambazo ni water resistant .... na worktops za jikoni au wc tops tunatumia marble au granite ... haya ndiyo matumizi proper .... pia finishing ya formica ni ngumu sana especially at the edges na ugundishaji huu wa kienyeji haiachi kubanduka mara kwa mara ... hii ndiyo inayopelekea wenzetu kuigundisha na boards kwa kutumia industrial process ambayo ni surface pressing
kwa kweli kwa karne hii hata mafundi kuwauliza formica walishasahau ingawa bado zipo .... nakubaliana na wewe kwmba kama kawaida kuna bidhaa za boards zinazotoka sehemu kama china hazina ubora ... hebu pata boards za South Africa utaniambia mkuu
Thanx Brother, wewe ni seremala? Kazi zako unfanyia wapi kaka?
Nimeipenda hii mkuu nataka fomaika kwa ajili nataka kutengeneza shelf za ukutani kwa kutumia mbao kwani sijaona mbao ambazo ni special kwa shelf,napenda kama zile za display ukienda kama kwenye maduka ya Samsung/Tigo/Voda huwa na display nzuri.Pia nataka fomaika kwa ajili ya kutumika kama wall paper, nataka kusanifisha ukuta .technology ya zamani hiyo mkuu...siku hizi kuna materials zinaitwa "Melamine boards" na "MDF boards" zinakuwa na profile ya Formica at the facing side