BabaDesi
JF-Expert Member
- Jun 30, 2007
- 6,032
- 3,944
Wakati mwingine huwa nahisi hata kuwalaumu hawa 'waasia' pengine tunawaonea tu....zaidi ni udhaifu wa viongozi wetu na hasa Rais wetu. Mambo yote haya yanayotokea yanategemea sana 'tone at the top'! Ameshindwa kabsa kuwaambia "Ikulu ni mahali patakatifu".
Sitta aliwahi kumshauri awe mkali kidogo lakini nina mashaka makubwa kwamba alielewa alichoshauriwa! Kwa kweli tunastahili kuwa masikini.
...Una pointi hapo. Kwa mfano ningependa kufahamu Askari waliokuwa hapo geti kuu walijaribu kumuelekeza mheshimiwa sana Tanil akapitishie kigari chake geti la uani?? Aliwajibu nini? Nani alikuja ama alitoa maagizo aachiwe atumie geti hilo hilo? Sometimes hata sisi wadanganyika wenyewe tunakuwa waoga wa kutekeleza majukumu yetu kiasi kwamba wakalamba kama hawa wanatuchezea watakavyo. Kwa mfano jukumu kubwa tunalotakiwa kuwa nalo hivi sasa ni kutafuta na kufundisha Snipers....!