~ * ~ Fisadi wa Penzi (R - Rated)~ * ~

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
fisadiwapenzi.jpg

Habari zilivuma kwa haraka na kwa nguvu utadhani upepo wa kimbunga cha Katrina. Rais Rajab H. Fungo amemfukuza kazi Naibu Waziri Dk. Laurent Magosi kufuatia madai ya ukosefu wa nidhamu, matumizi mabaya ya madaraka, na udhalilishaji wa ofisi. Hakuna aliyetarajia kitendo hicho cha kijasiri kwani Dk Magosi alikuwa ni rafiki na msiri mkubwa wa Rais. Kila mtu alitaka kujua ni nini hasa kilichotokea kiasi cha marafiki hao wa karibu kukosana. Ilipita karibu mwezi mmoja ndipo kisa kamili cha kilichotokea kilipojulikana wazi baada ya mwandishi mashuhuri wa makala za magazeti nchini alipochapisha habari za kisa chenyewe kwenye mtandao maarufu wa Jambo Forums, mtandao ambao miezi michache kabla yake ulijaribu kufungwa na Waziri Magosi.

* * *

Viwanja vya ikulu vilikuwa vimepambwa kwa mapambo ya kila aina yenye rangi za Taifa. Bendera ndogondogo zilikuwa zimewekwa kila kona ya jengo na kila mtu alijitahidi kuwa na bendera ndogo mkononi. Ilikuwa ni siku iliyosubiriwa kwa hamu na wananchi wa Jamhuri ya Tanzania. Upepo wenye harufu ya chumvi toka Bahari ya Hindi ulivuma na kuwapoza watu waliokuwa wamejawa tabasamu za kila aina. Rais mpya Mheshimiwa H. M. Fungo alitarajiwa kuwaapisha wananchi karibu aliowaamini na kuwapa nafasi mbalimbali katika Baraza lake la Mawaziri. Walikuwa ni Mawaziri na Manaibu Waziri wa serikali ya awamu ya nne. Ngoma za kienyeji zilisikika na muziki wa dansi uliendelea kuporomoshwa kungojea muda wa kuapishwa kufika

Miongoni mwa waliongojea kwa hamu kuapishwa siku hiyo ni Dk. Laurent Magosi ambaye aliteuliwa kuwa Naibi Waziri wa Elimu ya Juu na Maendeleo ya Sayansi. Dk Magosi alikuwa amevalia kinadhifu suti ya rangi ya kijivu na tai iliyoendana nayo. Alikuwa ni kijana wa miaka 32 hivyo kumfanya miongoni mwa mawaziri vijana zaidi katika historia ya uongozi wa kisiasa za Tanzania hivi karibuni.. Dk. Magosi alizungukwa na familia yake akiwemo mkewe na mtoto wao wa pekee na marafiki ambao walikuja kumpa pongezi. Viongozi wengine wa ngazi za juu wa CCM walimpa mikono ya pongezi na heri kwani Dk. Magosi alitumia uwezo wake mkubwa wana wakati wa kampeni ulioweza kumpatia ushindi mgombea wa uraisi wa CCM. Hata hivyo kuna watu walioona kitendo cha yeye kuteuliwa Unaibu Uwaziri kama malipo ya mchango wake wa kisiasa. Hata hivyo hilo halikumkatisha tamaa.

* * *
Baada ya sherehe za kuapishwa kulikuwa na mlo wa jioni pamoja na Rais na baadaye viongozi walianza kutawanyika na kwenda majumbani kwao kupumzika. Dk. Magosi alimtaka radhi mkewe kuwa anahitajiwa kubakia pale Ikulu kwa muda kidogo lakini atakuwa njiani kurudi nyumbani kwao kule O’Bay. Mkewe hakusema kitu kwani alijua kuwa sasa mumewe amekuwa kiongozi wa serikali na mambo kama hayo yatakuwa yakiongezeka siku kwa siku.

Kitu ambacho Mama Magosi hakukijua ni kuwa Dk. Magosi alikuwa na mahusiano ya karibu na binti wa aliyewahi kuwa Waziri Mkuu. Binti huyo alikuwa ameolewa na Mbunge mmoja machachari wa mikoa ya kanda ya ziwa. Baada ya Dk. Magosi kumwaga mkewe na kuhakikisha ameondoka pale Ikulu, alichukua simu yake na kumpigia hawara yake Beatrice Mvumi aliyekuwa anapiga zogo na wake wengine wa wakubwa. Hakusema mengi aliandika ujumbe tu waonane baada ya nusu saa. Beatty (kama alivyojulikana) aliwaaga wake za vigogo hao mara tu baada ya kuangalia ujumbe kwenye simu yake. Mheshimiwa Mvumi (mumewe) alikuwa ameenda hoteli ya Movenpick ambapo yeye na wabunge wengine wachache waliamua kwenda kujipongeza. Aliandika majibu machache na kumtumia Dk. Magosi . Dk. Magosi na Beatty waliondoka kwa magari tofauti huku wakitoa visingizo visivyo na kichwa wala miguu. Walianza kuzungumza mambo ya mapenzi kwa simu, wakichokozana na kunyegeshana.

Haikuwachukua muda mrefu kufika kwenye Hoteli ya Millenium Towers, mojawapo ya hoteli za kisasa na mpya kabisa jijini Dar-es-Saalam. Chumba alichokodi mheshimiwa Magosi kilikuwa na kila aina ya vikolombwezo. Kilikuwa kipana na kitanda chake kilikuwa kikubwa chenye shuka za rangi ya machungwa na udongo. Kila kitu kilipangiliwa kiufundi. Kutokana na hekaheka za uchaguzi na kuweka serikali mpya makinda hawa wawili hawakupata muda mwingi wa kuwa pamoja

“Nimekumiss sana Beatty” Alisema Dk. Magosi
“Mimi pia, mpenzi” Alijibu Beatty akijirusha mikono mwa Dk. Magosi .

Kama wehu, wapenzi hao wawili walianza kurushiana mabusu motomoto huku wakipasasana na kuchezeana miili. Dk. Magosi alikuwa ni mahiri wa mabusu, alimbusu, Beatty kwenye shingo na kwenye shafu, mdomoni na kidevuni. Beatty, nguvu zilianza kumtoka. Alijihisi anaishiwa nguvu za kusimama. Ashki kubwa ilimpanda. Bila kuchelewa wala kufanya ajizi alianza kufungua shati la Dk. Magosi , na yeye Mheshimiwa hakumlazia damu. Dk. Magosi alizungusha mikono yake hadi kwenye mgongo wa Beatty na pole pole alianza kuteremsha zipu. Akaanza kumchojoa mwanamama huyo gauni lake la rangi nyekundu lililombana vyema mwilini mwake. Hilo gani lilimvaa mwanamama huyo utadhani alizaliwa nalo.

Walimalizana kuchojoana nguo. Kama vile Adamu na Eva kwenye bustani ya Edeni wapenzi hao wawili walitazamana kwa hamu na tamaa kubwa. Dk. Magosi alikuwa amedinda utadhani sanamu ya “Askari”.

Kwa shauku Beatty alimsogolea Mheshimiwa Magosi . Mikono yake mwanadada huyo ilikuwa laini, yenye kucha ndefu zilizopakwa rangi nyekundu. Viganja vyake vilikuwa vimepambwa kwa michoro mbalimbali ya maua kwa rangi ya hina. Walikumbatiana wakiwa wamesimama, huku wakiendelea kubusiana na kutomasana. Dk. Magosi alimnyanyua Beatty na kumweka kwenye meza iliyokuwa imeegama ukutani. Na mbele yake kulikuwa na kioo kikubwa cha kuvalia. Beatty aliinyanyua miguu yake na kuipanua pembeni. Dk. Magosi aliuangalia mgongo wa Beatty kwenye kioo. Alimsogolea taratibu huku akianza kumwingia. Beatty alikuwa amelowa kama mvua! Dk. Magosi alilipenda hilo. Hakulaza damu aliendelea kumwingie huku akimkatikia taratibu. Jasho lilianza kumtoka licha ya chumba kuwa na kiyoyozi kilichokuwa kikitoa hewa baridi! Beatty alizungusha miguu yake na kumfunga utadhani kufuli Dk. Magosi . Dk. Magosi aligangamaa na kumwinua Beatty toka hapo kwenye meza. Kwa sekunda alisimama wakijiangalia walivyopendeza katika “mkao huo wa kula”. Walibusiana.

Pole pole alimlaza Beatty chali kitandani. Kama mtu aliyepagawa alianza kufanya mapenzi kwa nguvu huku akiguna na kuhema kwa kasi. Beatty naye alizungusha kiuno chake utadhani anacheza ngoma ya kimakonde! Dk. Magosi alimpa, Beatty naye akarudisha! Akienda kushoto, Beatty kulia, akienda chini, Beatty anakuja juu. Ilikuwa raha juu ya raha! Jasho lilimtoka mheshimiwa wa watu, hakusumbuka kujipangusa.

Wakakumbatiana tena halafu wakageuziana nafasi. Beatty sasa alikuwa juu. Alikuwa anapenda sana kuwa juu kwani anakuwa na uwezo wa kufanya lolota analotaka na anakuwa ni mtawala wa kazi ya mapenzi. Beatty alianza kumkatia huyo Mheshimiwa mtukufu Naibu Waziri.

“Hii ni zawadi yako Mhe. Naibu Waziri” Alisema kwa sauti iliyolegea huku akitabasamu na kujiuma mdomo wa chini.

“Asante, sana” Mheshimiwa alijibu kwa kigugumizi.

Beatty aliivuta mikono ya mheshimiwa na kuishikisha juu ya kichwa cha mheshimwa ikiwa imeegama kwenye mto. Alianza kumbusu kifua na kumnyonya chuchu zake huku akiendelea kukatika kiuno. Mheshimiwa hakujua Mungu ampe nini tena. Kaukwaa uwaziri, na sasa anafanya mapenzi na mwanamke ambaye anampenda kuliko hata mke wake. Beatty alianza kuongeza kasi huku akipiga kelele za mapenzi. Mwili wa binti huyo ulikuwa umelowa jasho kitu kilichomfanya apendeze zaidi na kungara. Mikufu yake ya dhahabu iliyokuwa ikining’inia shingoni ilimfanya aonekane kama vile ni Malkia Nerfititi wa Misri ya Kale.

Wapenzi hao waliendelea kupeana mapenzi ya nguvu hadi walipofika kilele. Walihisi wako mbingu ya saba. Hawakujali nani ni Rais, wako wapi, au nini. Nyoyo zao zilikuwa zimetiwa ganzi ya mapenzi. Hawakusikia cha mtu wala kuambiwa. Siku hiyo ilikuwa ni siku ya pekee. Dk. Magosi alimuhakikishia Beatty kuwa licha ya nafasi yake hiyo mpya wataendelea kukutana kimapenzi kila wapatapo nafasi.

Waliagana usiku huo wa pongezi majira ya saa nane za usiku na kila mmoja aliondoka na kurejea kwa wenzi wao wa ndoa.

* * *

Ilipita miezi mitatu tangu Mhemishiwa Dk. Magosi ateuliwe kuwa Naibu Waziri na mahusiano yake na Beatty yaliendelea kwa siri na kwa kweli yalipamba moto. Makutano hayakuishia hotelini tu hata wakati mwingine Beatty alimtembelea waziri huyo ofisini na bila haya walijifungia kwa karibu saa nzima wakipeana mavitu. Msiri mkubwa wa mahusiano hayo alikuwa ni Katibu muhtasi wa Naibu waziri huyo, mama mmoja wa makamo toka Tabora. Waziri hakusita kumkatia kitu cha “nguvu” ili aendeleze ukimya wake na kuwasukia kila aina ya udhuru.

Ilikuwa siku ya Ijumaa majira ya nne za asubuhi Beatty aliegesha gari lake si mbali sana na makao makuu ya Wizara ya Dk. Magosi . Alivalia miwani yake ya jua na kichwani alijifunga kilemba cha maua maua. Alipofika kwenye ofisi ya Waziri mama Makula (karani) alionyesha furaha kwani alijua atapata kitu kidogo siku hiyo. Mama Makula aliingia ofisini kwa Naibu Waziri.

“Mzee, mgeni wako amefika” Alisema huku akimwangalia naibu waziri aliyekuwa amevalia shati jeupe na tai yake ya kijivu iliyolegezwa shingoni.

“Asanteni sana mama Makula, nipe kama dakika tano hivi” Alisema Dk. Magosi

“Hamna maneno, niashirie tu ukiwa tayari” Mama Makula alijibu huku akiurudisha mlango.

Alimgeukia Beatty aliyekuwa amekaa utadhani malkia wa mbingu kwenye mojawapo ya sofa za wageni. Hakukuwa na mtu mwingine hapo. Baada ya kama dakika tano hivi simu iliita na baada ya kusikiliza kwa sekunde chache Mama Makula alimwashiria Beatty kuwa yuko huru kuingia ofisini kwa naibu Waziri.

Mheshimiwa alikuwa amesimama kumsubiri na aliurudisha mlango lakini hakuufunga kwa funguo. Mama Makula hakumruhusu mtu yeyote kuingia hapo ofisini kwani mzee alikuwa na “mkutano muhimu”.

“Nimekumiss sana gorgeous!” Alihamaki kwa shauku Dk. Magosi huku akifungua mikono yake kumkumbatia Beatty na kumrushia busu la nguvu.

“Mimi pia, baby!” Alijibu Beatty bila kuchelewa, huku akiguna.

Dk. Magosi hakuchelewa kuanza kumvua chupi mwana dada huyo. Mviringo wa matako yake ulizuia kidogo kazi hiyo lakini ilikuwa ni changamoto rahisi kwa Mheshimiwa huyo. Wakati huo huo Beatty alikuwa akiulegeza mkanda wa suruali ya Dk. Magosi na haikuchukua muda suruali ilianguka sakafuni. Walisogea kwenye kochi kubwa la rangi nyeusi na Dk. Magosi alijilaza chali. Bila haya wala kujiuliza mara mbili Beatty “alimkalia”. Hakuweza kupiga kelele kama alivyopenda lakini hilo halikumzuia kumpa vitu vya nguvu mheshimiwa huyo. Alikuwa amelowa tepe utadhani ardhi iliyonyeshewa mvua za masika!

Baada ya kama dakika kumi hivi, ilikuwa ni zamu ya Dk. Magosi kuja juu na kuanza kumpa vitu vya nguvu huku akimbusu kwa nguvu. Mikono laini ya Beatty ilikuwa chini ya shati la waziri huyo ikiupapasa mgongo wake na kumwongezea raha isiyo na kifani. Ilikuwa ni karibu wafikie kilele waliposikia sauti mlangoni. Hawakutaka kukatisha kwani walijua mama Makula atashughulikia hilo. Mheshimiwa hakuweza kujizuia na akaongeza mwendo na nguvu zaidi, huku jasho likimtoka. Akili na ufahamu ukamtoka alipolipuka uatadhani volcano ya El Donyo Lengai! Walikumbatiana wakati Beatty naye akifika kilele. Beatty alijikunja na kujikungua utadhani samaki Ngise!

Walipofumbua macho, walisikia mtu akikohoa kutoka upande wa meza ya Naibu Waziri. Hakuwa mwingine ila Mheshimiwa Rais Fungo. Bila kusema maneno mengi, Mheshimiwa Rais alimwangalia Dk. Magosi .

“Jiandae kufunga virago” Rais alisema bila hata kutaka nafasi ya maelezo.

“Mheshimwa Rais... ahh.. samahani sana... nilipitiwa” Dk. Magosi alijaribu kujitetea. Beatty alikuwa anamaliza kuvaa nguzo zake haraka haraka na kutaka kuelekea mlangoni.

“Beatty, ningekuwa wewe nisingeenda huko” Rais alimwambia. Beatty aligeuka na kumwangalia Rais.

“Kuna waandishi huko na Mumeo yuko kwenye msafara wangu” Rais alitoa sababu

“Mungu wangu!” Dk. Magosi alihamaki

“Hawajui nilichokiona huku, kwani wanadhani ninafanya mazungumzo na Magosi hapa” Aliendelea. “hivyo subiri sisi tuondoke, kwani nafanya ziara za dharura leo katika wizara mbalimbali” Aliwausia.

* * *

Jioni ya siku hiyo, kwenye taarifa ya habari ya saa mbili, ndipo habari ziliposikika kuwa Rais Fungo amemfukuza kazi Naibu waziri Dk. Luenamme Magosi kwa sababu ya ukosefu wa nidhamu, matumizi mabaya ya madaraka, na udhalilishaji wa ofisi. Watanzania walipigwa na butwaa lakini pia walifurahia kwani wakati wa utendaji kazi hatimaye umefika!

Wananchi walishangazwa na kitendo cha Rais kumfukuza kazi kwani kwa muda mrefu wale wote waliokuwa wakihusishwa na matukio ya kashfa waliachwa wajiuzulu. Watu wakakumbuka kisa cha yule Waziri Mkuu aliyelazimka kujiuzulu na ambaye aliporudi jimboni kwake alipokelewa kwa shangwe kama shujaa. Na wapo wanaokumbuka kisa cha waziri mwingine aliyekuwa anajulikana kama “mzee we vijisenti” ambaye naye baada ya kujiuzulu baada ya kashfa yake kuibuliwa alioporudi kwao alipokelewa kwa ngoma na matamasha.

Kitendo cha Rais kumtimua kazi Dr. Magosi kilipokelewa kwa shangwe kubwa na furaha na wananchi wakafanya na matembezi ya kumuunga mkono Rais kwani sasa walijua ile sura yake nzuri na tabasamu vimewadanganya wengi.

Wananchi wakiwa bado wanafurahia jambo hilo taarifa nyingine mpya ikaanza kutumwa kwenye simu mbalimbali za watu kwa njia ya sms kuwa Dr. Magosi amekunywa sumu! Hawakujua walie, au wacheke. Waliopata kauli wakajikuta wanasema “fisadi wa penzi kaondoka”

MWISHO

Kanusho:
Kisa hiki ni cha kutunga. Mfano wowote na watu, mahali, au matukio halisi ni matokeo ya nasibu tu na si kusudio la mwandishi.
 
unajua mwanzoni niliweka majina ya viongoxzi fulani wa sasa... then I changed my mind.

I hope it was a good entertainment
 
Sure mkuu,
Maaanake majina ya Richmond,Vasco Da Gama na......

Ila i wish kama prez wetu angekua na nguvu ya kumkuta mwanamtandao akichafua ofisi na kumfukuzia mbali.Ingependeza eeh?
 
u c that is the fantasy part.. HIvi mnajua nchi italipuka kwa furaha kiasi gani wakisikia "Rais Jakaya Kikwete leo amemfukuza kazi waziri wa mawasiliano na technolojia"....
 
That was really entertaining! Lakini is far from being true. Rais hawezi kuingia kwenye ofisi ya Naibu Waziri peke yake hata bila ya Waziri wa ofisi hiyo..... again siamini kabla kuna fisadi wa penzi kama huyo Dr. yaani mapenzi ofisini bila kufunga mlango! najaribu tu kuisoma hadithi hii na critical mind!
 
jobo... kuna mambo ya kufikirika duniani na mengine yanawezekana katika ulimwengu wa kufikirika. Ndio maana nimesema ni hadithi ya kubuni.
 
Kwa serikali yetu hii, kuna waziri gani alishawahi kufukuzwa kazi?
Kwa Tanzania bado sana, hasa kwa awamu hii
 
mekapendaje sasa kasehemu haka!


Kwa shauku Beatty alimsogolea Mheshimiwa Magosi . Mikono yake mwanadada huyo ilikuwa laini, yenye kucha ndefu zilizopakwa rangi nyekundu. Viganja vyake vilikuwa vimepambwa kwa michoro mbalimbali ya maua kwa rangi ya hina. Walikumbatiana wakiwa wamesimama, huku wakiendelea kubusiana na kutomasana. Dk. Magosi alimnyanyua Beatty na kumweka kwenye meza iliyokuwa imeegama ukutani. Na mbele yake kulikuwa na kioo kikubwa cha kuvalia. Beatty aliinyanyua miguu yake na kuipanua pembeni. Dk. Magosi aliuangalia mgongo wa Beatty kwenye kioo. Alimsogolea taratibu huku akianza kumwingia. Beatty alikuwa amelowa kama mvua! Dk. Magosi alilipenda hilo. Hakulaza damu aliendelea kumwingie huku akimkatikia taratibu. Jasho lilianza kumtoka licha ya chumba kuwa na kiyoyozi kilichokuwa kikitoa hewa baridi! Beatty alizungusha miguu yake na kumfunga utadhani kufuli Dk. Magosi . Dk. Magosi aligangamaa na kumwinua Beatty toka hapo kwenye meza. Kwa sekunda alisimama wakijiangalia walivyopendeza katika "mkao huo wa kula". Walibusiana.

Pole pole alimlaza Beatty chali kitandani. Kama mtu aliyepagawa alianza kufanya mapenzi kwa nguvu huku akiguna na kuhema kwa kasi. Beatty naye alizungusha kiuno chake utadhani anacheza ngoma ya kimakonde! Dk. Magosi alimpa, Beatty naye akarudisha! Akienda kushoto, Beatty kulia, akienda chini, Beatty anakuja juu. Ilikuwa raha juu ya raha! Jasho lilimtoka mheshimiwa wa watu, hakusumbuka kujipangusa.

Wakakumbatiana tena halafu wakageuziana nafasi. Beatty sasa alikuwa juu. Alikuwa anapenda sana kuwa juu kwani anakuwa na uwezo wa kufanya lolota analotaka na anakuwa ni mtawala wa kazi ya mapenzi. Beatty alianza kumkatia huyo Mheshimiwa mtukufu Naibu Waziri.

"Hii ni zawadi yako Mhe. Naibu Waziri" Alisema kwa sauti iliyolegea huku akitabasamu na kujiuma mdomo wa chini.

"Asante, sana"
 
Back
Top Bottom