First Ladies Phenomenon - Is Tanzania doing that bad?

Good to learn abt the history of FLs of USA.
Back to our own situation.Ukiacha Nyerere, marais waliofuatia sidhani walikuwa na " "ambition" au ndoto ya kuja kunyakua nafasi ya juu kupita zote katika uongozi wa taifa la Tanzania, kiasi kwamba "wajiandae" kuwapata wenzi watakaoweza kwenda sambamba na majukumu yaliyoko ikulu.Mkuu wa sasa kweli alikuwa na muda lakini inaelekea maandalizi yake hayakuhusisha pia kumwandaa FL.Utakumbuka kwa mfano Hillary Clinton na hata akina Nancy Regan walikuwa na usemi sana katika shughuli wafanyazo waume zao ikiwa ni mpaka hata kupitia hotuba zao na kuweka sawa.Ukija huku Africa, hasa Africa Magaribi baadhi ya wake wa marais kama Mrs Dr.Maryam Babangida, Madam Nana Rawlings na wengine waliweza kuwa na mvuto na hata kufanya waliyoweza kuyafanya ( hata kama hayakubaliki sana na wengi) kwa vile walikuwa na kisomo na hata hao waume zao walilijua hilo na kuwaaminisha wafanye.
Tukija huku Tz, wengi wa wale waliokuja kuchukua uongozi, tayari walishajipatia wenzi wao wa maisha ambao si ajabu walijikuta tu wanalazimika kufanya u FL bila hata maandalizi yoyote.Ningetegemea Serikali yetu na hasa Wizara za Mambo ya nje wakishirikiana na Wizara ya Wanawake wangeona umuhimu wa kutengeneza induction programme ya kuwasaidia wamama wa kwanza kwa kila hali - kuanzia kuwapa msasa wa mambo ya kidiplomasia, uendeshaji wa ikulu kama makazi rasmi ya rais, na stadi nyingine ikiwa ni pamoja na public speaking na hata kuongeza elimu.
 
Last edited:
WomenofSubstenc,

Bibie hapa kidogo sintakubaliana nawe kwa sababu neno First Lady ni wadhifa (kwa kuelewa kwangu) ..Otherwise tulitakiwa kumwita Mrs. Kikwete.. Hilo neno First Lady lina uzito mkubwa sana na heshima zote anazopata zinatokana na neno hilo na mnategemea vitu fulani kutokana na wadhifa huo. Na wadhifa huu hukoma tu pindi akiondoka Ikulu...Ni sawa na wadhifa wowote ule hata iwe dereva, ataitwa dereva kwa sababu amnaendesha gari, nje ya hapo sii dereva.

Pili, kinachonisumbua mimi na hoja nyingi zinazohusiana na First Lady ni ile copy cat ya First Lady wa Marekani. Kila hoja humu inatazama kazi za First Lady wa Marekani na tunajaribu kulinganisha jambo ambalo sii lazima kabisa. Kuna mataifa mangapi duniani? na ni First Lady wangapi wanayafanya anayoyafanya mke wa Bush au Obama..
Hizo Public Appearence na misafara ni ngapi tumewaona wake wa viongozi hawa wakishiriki..Wachache sana hawaweza kuwa sawa au kulingana na rais wa Marekani. Hivi navyozungumza simfahamu mke wa Gordon hata kwa sura maana sijawahi kumwona popote..Acha huyo naweza sema asilimia 99 ya wake za Marais sina habari zao kikamilifu na umenisaidia sana kusoma baadhi ya maelezo yako ya mwanzo.

Muhimu kwetu ni tufikirie tunataka nini mke wa rais akifanye na anatweza vipi kulisaidia Taifa letu kutunza, kutangaza na kuimarisha asili na mila zetu..
- Mwanamke ndiye mtendaji mkuu (rubani) wa familia zetu!.

Nadhani Mkuu hatutofautiani katika hili na nafikiri hata ukirejea posts zangu za awali utaona tuko pamoja kabisa.Kinachogomba ni vile tunavyotarajia FL wa Tanzania awe sawa na wale wa Marekani na kwingineko wakati mazingira na historia ni tofauti kabisa.
Respect.
WoS
 
Nadhani Mkuu hatutofautiani katika hili na nafikiri hata ukirejea posts zangu za awali utaona tuko pamoja kabisa.Kinachogomba ni vile tunavyotarajia FL wa Tanzania awe sawa na wale wa Marekani na kwingineko wakati mazingira na historia ni tofauti kabisa.
Respect.
WoS

The FL positions depends on political position of the woman herself, power relations in the marriage, availability of resources, personality, and context of the country.

I believe, first lady could do more even in tanzania, they simply need support to organize their actions.
 
Mama Maria Nyerere aliulizwa swali kama mnalolijadili. Alijibu kwamba wao kama wanawake sehemu ya ilikuwa UWT basi. Hakujitutumua na lolote. Ukiuliza shughuli zake sasa hivi tunaambiwa kuwa ni muumini mzuri wa Kanisa lake Katoliki.
Kwa uadilifu wa First Ladies hatajatokea kama huyu. Ujasiri amali aliojaribisha ni wa kufuga kuku tena kwa mtaji aliopata baada ya kupata zawadi ya Rais Nyerere kustaafu.
Leo hii heshima imemjaa tele.
Wakiwekwa ma-first lady hadharani wapeane mkono na watu kila mmoja atakimbilia kwa Mama Maria na kuacha hao wengine wapewe mikono na waliowaajiri kwenye hizo NGO zao.
Paskali.
 
Wakiwekwa ma-first lady hadharani wapeane mkono na watu kila mmoja atakimbilia kwa Mama Maria na kuacha hao wengine wapewe mikono na waliowaajiri kwenye hizo NGO zao.
Paskali.

Hii kali!
Hizi NGOs zimelazimika kuanzishwa hasa baada ya mkutano wa FLs wa 1992 ambapo maazimio yaliyotolewa yalihitaji mfumo wa kuyatekeleza.Ila labda cha kujiuliza ni kwanini mama Sitti ambaye alikuwa FL wakati huo na akahudhuria huo mkutano hakuanzisha NGO?
 
Nje ya hapo nadhani tumeona kuwa First Lady wote wa Kiafrika wamekuwa mbele ktk siasa za utawala wao kitandani kuingia hadi ktk Utawala wa nchi nzima..Kutokana na Umaskini wetu hata mila na desturi zetu za kiasili zimepotea hivyo tunajaribu kuiga vitu ambavyo hatuna kabisa uwezo navyo kutokana na mazingira yetu kwani Ukitazama kati ya First Lady wote wa nchi za Kiafrika ni asilimia ndogo sana waliomaliza high school acha mbali chuo kikuu

I think this is very insulting, generalizing, and biased opinion. Yes, we could argue first ladies perhaps they have not deriver to our expected standards, perhaps they don't have the qualities we dream for. However, building an argument on "utawala wa kitandani, and low education", it is out of boundaries.
 
Umeenda mbali. Kwani viongozi wetu hapa nchini ambao waume zao sio mawaziri au viongozi wakuu waume zao umeshawahi kuwaona hadharani? Wanawake ndio zao akishakuwa mkubwa anamwacha nyuma mumewe. Hawi nae bega kwa bega. Hata kwenye sherehe hutawaona. Je, ulimwona mumewe Sophia Simba siku ile anachaguliwa kuwa mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake? Mie sikumuona.

wake wa waziri wangapi, ambao sio mawaziri ama wabunge, unawafahamu wake zao?

Naamini kwamba tamaduni zetu za public service, ukiacha nafasi za uraisi hadi ngazi ya waziri mkuu huu utamaduni wa watu wa kwenda na wenza wao bado pande zote mbili za jinsia wanahitaji kujifunza.
 
Mama Maria Nyerere aliulizwa swali kama mnalolijadili. Alijibu kwamba wao kama wanawake sehemu ya ilikuwa UWT basi. Hakujitutumua na lolote. Ukiuliza shughuli zake sasa hivi tunaambiwa kuwa ni muumini mzuri wa Kanisa lake Katoliki.
Kwa uadilifu wa First Ladies hatajatokea kama huyu. Ujasiri amali aliojaribisha ni wa kufuga kuku tena kwa mtaji aliopata baada ya kupata zawadi ya Rais Nyerere kustaafu.
Leo hii heshima imemjaa tele.
Wakiwekwa ma-first lady hadharani wapeane mkono na watu kila mmoja atakimbilia kwa Mama Maria na kuacha hao wengine wapewe mikono na waliowaajiri kwenye hizo NGO zao.
Paskali.

Inawezekana ni kweli kabisa kwamba Maria Nyerere ataendelea kuheshimika na anaheshimika zaidi ya wake wengine wa maRaisi walifuatia. Ila napenda kusema heshima yake sio inakuja kwa kuwa mama aliyekuwa hapendi makuu, ila pia heshima ya Nyerere inamuongezee heshima. Sasa, tujiulize hao maraisi, matendo yao yaharibu vipi nafasi ya mke wa raisi? Kama kila siku tunapiga kelele, kikwete hiki mara kile, je Mama Salma ataheshimika kweli? Kama watu wanavuta pesa za EPa na kupanga mikakati isiyoeleweka ya kimaendeleo, si shangazwi na atakachofanya Salma.


Pili napinga swala lako kwamba Mama Maria anaheshimika kwa kuwa hakuwa kwa kujaribu kukaa mbali na ujasiliamari na kuelewa nafasi yake kama mwanamke ipo ndani ya UWT. Nadhani mtizamo huo ni kuwafinya kinamama. FL yoyote mwenye uwezo wa kufanya maswala yoyote ya kijamii afanye, ili mradi awe mkweli, mchapakazi na mfano kwa kinamama wengine.

Naamini mke wa raisi nafasi yake ya kuleta mabadiliko ni kubwa zaidi ya mama jumanne ambaye hana resources. Mke wa raisi anaplatform anaweza kumobilize wanawake na kutete haki mbalimbali za wanawake na watoto kwa ujumla wake. Swala, ni kwamba nafasi hiyo haina hadidu rejea, kwahiyo inahitaji uaminifu na kujitolea kwa kweli.
 
Good to learn abt the history of FLs of USA.
Tukija huku Tz, wengi wa wale waliokuja kuchukua uongozi, tayari walishajipatia wenzi wao wa maisha ambao si ajabu walijikuta tu wanalazimika kufanya u FL bila hata maandalizi yoyote.Ningetegemea Serikali yetu na hasa Wizara za Mambo ya nje wakishirikiana na Wizara ya Wanawake wangeona umuhimu wa kutengeneza induction programme ya kuwasaidia wamama wa kwanza kwa kila hali - kuanzia kuwapa msasa wa mambo ya kidiplomasia, uendeshaji wa ikulu kama makazi rasmi ya rais, na stadi nyingine ikiwa ni pamoja na public speaking na hata kuongeza elimu.

Kwa mtizamo wangu mimi, kazi ya kuwa First Lady sio ndogo hata kidogo. Ni kazi kubwa sana inayohitaji nia, uelewa na maamuzi ya kuwa first lady. Sidhani, kama FL wote wanaweza kufurahi maisha yao kubadilika vu bini va.

Kwa mtizamo wangu mimi, swala la kumtayarisha first lady, linapaswa lianze kuanzia katika ngazi ya familia. Mume amuite mkewe, amweleze nia yake ya kugombea na amuulize mkewe kama yupo tayari kuwa naye katika kinyanganyiro hicho na iwapo atashinda basi kama yupo tayari kuwa first lady.

Nadhani kama maongezi haya yatatokea mke wa mgombea ataanza kuifikiria nafasi hiyo, mwisho anaweza akakubali ama kukataa mumewe asigombee. Kama akikubali atajifunza agenda za mumewe, hata kama ni apolitical atajaribu kufuatilia agenda zake. Na yeye binafsi kuanza kujitayarisha na kufikiria maisha yake ya miaka mitano ndani ya ikulu yatakuwaje.

Lakini kwa tamaduni zetu, mume akiamua basi mke afuate tu. Hii si sawa. Mke anapaswa kufanya maamuzi kama anataka kuwa sehemu ya maamuzi ya mumewe. Maana kutoka maisha ya kawaida ya uhuru wa kwenda salooni unayotaka, kwenda kariakoo kununu chakulia, kuelekea mitaa ya sinza kumsalimia shoga, kupiga pamba nyepesi wakati wa kiangazi - kuhamia kusindikizwa na walinzi, kuvaa mavazi rasmi kila siku, kuacha kazi zake za kila siku - wakati mwingine hata ajira yake- sio uamuzi rahisi.

Kwa mtizamo wangu mimi, kama mwanamke ameridhia kushiriki katika kampeni na baadaye mumewe akashinda, hawezi kupata shida kutimiza majukumu yake. Na pia itakuwa raisi kwa serikali kumsaidi. Kwahiyo hayo maamuzi yaenzi toka nyumbani kwa wagombea. Sio kuzoanazoana tu dakika za mwisho!
 
mke wa blair alikuwa anafanya kazi yake ya QC kama kawaida na siku ingine ndio anafanya za kijamii, na ana watoto wanne/tano.....

mama salma angekuwa anaenda kufundisha somo lake moja part-time shule aliyetokea na siku nyingine anafanya kazi za kijamii. TZ tunaupungufu sana wa walimu.

mama salma hawezi kuwa muongeaji mzuri na si lazima iwe hivyo, hata micheal obama amemtia aibu obama kwenye campaign mpaka wakawa wanaakikisha haongei sasa hivi amepigwa msasa ndio anajitahidi kuongea.

mama salma anasifa zote za kuwa mke wa rais anajiheshimu, anaoneka sio macho juu na anavutia. sio mnene kama watu mnavyosema mimi naona ni wanawake wana wivu. unene wake na umri vinaendana.

ukweli: tatizo ni muungwana, inaonekana hamjali ila kwa ajili ni rais hataki kutia shaka mambo ya ndoa yake.
yule mama akiboronga kitu ni kwa ajili JMK hajaakikisha anapewa msasa vizuri na JMK ndio anatakiwa kupewa matusi yote.
JMK ambatana kidogo na mke wako shauri yako, watu wamempiga kofi mzee mwinyi.....
watu watakugeuka....
 
Hapa Petu,
I think this is very insulting, generalizing, and biased opinion. Yes, we could argue first ladies perhaps they have not deriver to our expected standards, perhaps they don't have the qualities we dream for. However, building an argument on "utawala wa kitandani, and low education", it is out of boundaries.
The question remains -Is it true or false?...
 
Hapa Petu,

The question remains -Is it true or false?...

No it is not true. it simply a biased statement specifically on bed politics. Because you have never been around when they in bed, have you?

The education party, i just don't have statistics, and its unfortunate we don't document enough of our first ladies in africa. But i should bring something to show you, most of these women were not merely home wives. They had education, might not be at university level, but college level. I can assume majority of them being teachers as i was a common profession for women in from 1960's to 1980's
 
The FL positions depends on political position of the woman herself, power relations in the marriage, availability of resources, personality, and context of the country.

I believe, first lady could do more even in tanzania, they simply need support to organize their actions.

I salute our First Lady..she is really doing a commendable job so far.... especially with the country-wide campaign against early pregnancies for girls in school.Lets give her all our support.
 
Back
Top Bottom