Figisu figisu Uchaguzi wa Mwenyekiti wa CCM Taifa

Malata Junior

JF-Expert Member
Nov 29, 2011
3,101
2,536
CCM ni chama kinachojinasibu kwamba ni chama cha kidemokrasia! Aidha katiba ya chama hicho inaainisha wazi kwamba kila mwanachama ana haki ya kugombea nafasi yoyote ile ikiwemo ya mwenyekiti wa chama Taifa.

Katiba inaeleza pia muda wa viongozi wa chama hicho kukaa madarakani ni miaka mitano kila baada ya uchaguzi.

Leo hii tunaona figisufigisu zimeanza za kutaka kumng'oa madarakani mwenyekiti Kikwete kabla ya muda wake kwisha kinyume na katiba.Tumesikia pia eti kuna mpango wa 'kumkabidhi' madaraka ya mwenyekiti wa Taifa Rais Magufuli.

Tulitarajia kusikia wanachama wakitangaziwa tarehe ya kuchukua fomu ya kugombea nafasi hiyo ili atakayeshinda ndiyo akiongoze chama hicho lakini huko kinachotaka kufanyika ni ukiukwaji mkubwa WA demokrasia na katiba ya chama hicho.

Haya yangefanyika kwenye vyama vingine vya siasa tungesikia kelele nyingi kutoka CCM na vyombo vyama vya propaganda ikiwemo ofisi ya msajili WA vyama vya siasa. Tuliona jinsi msajili alivyoingilia uchaguzi wa CHADEMA mpaka kufikia hatua ya kutaka kuwapangia nani agombee na nani asigombee!

Tunamtaka msajili aingilie kati ukiukwaji huu WA demokrasia na katiba ya chama hicho unaofanywa na CCM. Najiuliza kama wanasigina katiba ya chama chao wataweza kuilinda katiba ya nchi?
 
CCM ni chama kinachojinasibu kwamba ni chama cha kidemokrasia! Aidha katiba ya chama hicho inaainisha wazi kwamba kila mwanachama ana haki ya kugombea nafasi yoyote ile ikiwemo ya mwenyekiti wa chama Taifa. Katiba inaeleza pia muda wa viongozi wa chama hicho kukaa madarakani ni miaka mitano kila baada ya uchaguzi.Leo hii tunaona figisufigisu zimeanza za kutaka kumng'oa madarakani mwenyekiti Kikwete kabla ya muda wake kwisha kinyume na katiba.Tumesikia pia eti kuna mpango wa 'kumkabidhi' madaraka ya mwenyekiti wa Taifa Rais Magufuli. Tulitarajia kusikia wanachama wakitangaziwa tarehe ya kuchukua fomu ya kugombea nafasi hiyo ili atakayeshinda ndiyo akiongoze chama hicho lakini huko kinachotaka kufanyika ni ukiukwaji mkubwa WA demokrasia na katiba ya chama hicho.Haya yangefanyika kwenye vyama vingine vya siasa tungesikia kelele nyingi kutoka CCM na vyombo vyama vya propaganda ikiwemo ofisi ya msajili WA vyama vya siasa. Tuliona jinsi msajili alivyoingilia uchaguzi wa CHADEMA mpaka kufikia hatua ya kutaka kuwapangia nani agombee na nani asigombee! Tunamtaka msajili aingilie kati ukiukwaji huu WA demokrasia na katiba ya chama hicho unaofanywa na CCM. Najiuliza kama wanasigina katiba ya chama chao wataweza kuilinda katiba ya nchi?
wakati wa fomu sio mwaka huu tunatarajia JPm kukabidhiwa uenyekiti akimalizia kipindi kilichopaki ja JK.
kwa taarifa yako CCM sio chadema nimbie katibu mkuu wa chadema ni nani baada ya dr slaa kujiuzuru
 
Mimi sio CCM ila nathubutu kusema hoja yako ni dhaifu sana.Utaratibu wa kumpata mwenyekiti unaeleweka vyema kwamba atakayekuwa rais wa nchi kupitia chama hicho ndiye atakayekabidhiwa uenyekiti wa chama pia.Vyama vya upinzani ni tofauti kidogo,mwenyekiti huchaguliwa na wanachama.Tatizo linakuja kwa viongozi waliopo madarakani kutokuwa kuwapisha wengine waongoze,hawana tofauti na viongozi wa nchi za kiafrika ambao hupenda kung'ang'ania madaraka.
 
wakati wa fomu sio mwaka huu tunatarajia JPm kukabidhiwa uenyekiti akimalizia kipindi kilichopaki ja JK.
kwa taarifa yako CCM sio chadema nimbie katibu mkuu wa chadema ni nani baada ya dr slaa kujiuzuru
ni wapi ilipoandikwa kwenye katiba ya CCM utaratibu huo?
 
ccm mara hawataki kumpa uenyekiti jpm mara wanampa sijui niwe upande gan mm
 
Mimi sio CCM ila nathubutu kusema hoja yako ni dhaifu sana.Utaratibu wa kumpata mwenyekiti unaeleweka vyema kwamba atakayekuwa rais wa nchi kupitia chama hicho ndiye atakayekabidhiwa uenyekiti wa chama pia.Vyama vya upinzani ni tofauti kidogo,mwenyekiti huchaguliwa na wanachama.Tatizo linakuja kwa viongozi waliopo madarakani kutokuwa kuwapisha wengine waongoze,hawana tofauti na viongozi wa nchi za kiafrika ambao hupenda kung'ang'ania madaraka.
Mkuu si kweli katiba ya CCM haisemi Rais ndiyo mwenyekiti wa CCM Taifa. Je CCM isiposhinda urais mwenyekiti atapatikana vipi?
 
CCM ni chama kinachojinasibu kwamba ni chama cha kidemokrasia! Aidha katiba ya chama hicho inaainisha wazi kwamba kila mwanachama ana haki ya kugombea nafasi yoyote ile ikiwemo ya mwenyekiti wa chama Taifa. Katiba inaeleza pia muda wa viongozi wa chama hicho kukaa madarakani ni miaka mitano kila baada ya uchaguzi.Leo hii tunaona figisufigisu zimeanza za kutaka kumng'oa madarakani mwenyekiti Kikwete kabla ya muda wake kwisha kinyume na katiba.Tumesikia pia eti kuna mpango wa 'kumkabidhi' madaraka ya mwenyekiti wa Taifa Rais Magufuli. Tulitarajia kusikia wanachama wakitangaziwa tarehe ya kuchukua fomu ya kugombea nafasi hiyo ili atakayeshinda ndiyo akiongoze chama hicho lakini huko kinachotaka kufanyika ni ukiukwaji mkubwa WA demokrasia na katiba ya chama hicho.Haya yangefanyika kwenye vyama vingine vya siasa tungesikia kelele nyingi kutoka CCM na vyombo vyama vya propaganda ikiwemo ofisi ya msajili WA vyama vya siasa. Tuliona jinsi msajili alivyoingilia uchaguzi wa CHADEMA mpaka kufikia hatua ya kutaka kuwapangia nani agombee na nani asigombee! Tunamtaka msajili aingilie kati ukiukwaji huu WA demokrasia na katiba ya chama hicho unaofanywa na CCM. Najiuliza kama wanasigina katiba ya chama chao wataweza kuilinda katiba ya nchi?

Absolutely right!! Kama kuna utaratibu uliwekwa kwa wakati fulani ili kukithi mahitaji ya wakati huo usifanywe sasa ndiyo sheria. Kwanza utaratibu huu ni nje ya katiba ya Chama na unakandamiza demokrasia na kazi ya Chama.Tunasema kila siku Kazi ya Chama ni kusimamia serikali halafu
Mimi sio CCM ila nathubutu kusema hoja yako ni dhaifu sana.Utaratibu wa kumpata mwenyekiti unaeleweka vyema kwamba atakayekuwa rais wa nchi kupitia chama hicho ndiye atakayekabidhiwa uenyekiti wa chama pia.Vyama vya upinzani ni tofauti kidogo,mwenyekiti huchaguliwa na wanachama.Tatizo linakuja kwa viongozi waliopo madarakani kutokuwa kuwapisha wengine waongoze,hawana tofauti na viongozi wa nchi za kiafrika ambao hupenda kung'ang'ania madaraka.

Utaratibu wowote ndani ya taasisi huandikwa na hupitishwa na wanachama. Huu utaratibu wa kuachiana madaraka uliandikwa na nani na ulipitishwa na kikao gani
 
Absolutely right!! Kama kuna utaratibu uliwekwa kwa wakati fulani ili kukithi mahitaji ya wakati huo usifanywe sasa ndiyo sheria. Kwanza utaratibu huu ni nje ya katiba ya Chama na unakandamiza demokrasia na kazi ya Chama.Tunasema kila siku Kazi ya Chama ni kusimamia serikali halafu


Utaratibu wowote ndani ya taasisi huandikwa na hupitishwa na wanachama. Huu utaratibu wa kuachiana madaraka uliandikwa na nani na ulipitishwa na kikao gani
Kweli mkuu kama wanaona utaratibu huo unawafaa wafanye marekebisho ya katiba hili liingizwe.
 
Mangu anapinga ufisadi kwa madai yake, atakuwaje Na vyeo viwili Na vyote atachukua mshahara Na posho, huo si ufisadi?? Kwanini asiachie hiyo nafasi ya uenyekiti atoe fursa kwa wengine
 
CCM ni chama kinachojinasibu kwamba ni chama cha kidemokrasia! Aidha katiba ya chama hicho inaainisha wazi kwamba kila mwanachama ana haki ya kugombea nafasi yoyote ile ikiwemo ya mwenyekiti wa chama Taifa. Katiba inaeleza pia muda wa viongozi wa chama hicho kukaa madarakani ni miaka mitano kila baada ya uchaguzi.Leo hii tunaona figisufigisu zimeanza za kutaka kumng'oa madarakani mwenyekiti Kikwete kabla ya muda wake kwisha kinyume na katiba.Tumesikia pia eti kuna mpango wa 'kumkabidhi' madaraka ya mwenyekiti wa Taifa Rais Magufuli. Tulitarajia kusikia wanachama wakitangaziwa tarehe ya kuchukua fomu ya kugombea nafasi hiyo ili atakayeshinda ndiyo akiongoze chama hicho lakini huko kinachotaka kufanyika ni ukiukwaji mkubwa WA demokrasia na katiba ya chama hicho.Haya yangefanyika kwenye vyama vingine vya siasa tungesikia kelele nyingi kutoka CCM na vyombo vyama vya propaganda ikiwemo ofisi ya msajili WA vyama vya siasa. Tuliona jinsi msajili alivyoingilia uchaguzi wa CHADEMA mpaka kufikia hatua ya kutaka kuwapangia nani agombee na nani asigombee! Tunamtaka msajili aingilie kati ukiukwaji huu WA demokrasia na katiba ya chama hicho unaofanywa na CCM. Najiuliza kama wanasigina katiba ya chama chao wataweza kuilinda katiba ya nchi?
Kikwete ana majukumu ya kimataifa, panua wigo wako wa kufikiri.
 
Mimi sio CCM ila nathubutu kusema hoja yako ni dhaifu sana.Utaratibu wa kumpata mwenyekiti unaeleweka vyema kwamba atakayekuwa rais wa nchi kupitia chama hicho ndiye atakayekabidhiwa uenyekiti wa chama pia.Vyama vya upinzani ni tofauti kidogo,mwenyekiti huchaguliwa na wanachama.Tatizo linakuja kwa viongozi waliopo madarakani kutokuwa kuwapisha wengine waongoze,hawana tofauti na viongozi wa nchi za kiafrika ambao hupenda kung'ang'ania madaraka.

ccm kikishindwa uchaguzi nani anakuwa mwenyekiti?au Rais kivuli
 
Huwa nafurahi sana mnapo_challenge taratibu mbovu zilizopo ktk taasisi zetu zinazohusiana na uendeshaji wa taasisi hizo,shida yangu ipo pale mnapokosa uthubutu huu huu kukosoa namna CHADEMA kinavyoendeshwa,namna baadhi ya viongozi wasivyo tayari kuachia madaraka kwa taratibu za kidemokrasia na kubwa kuliko yote jinsi viongozi hawa wanapoleta mafanikio kidogo sana kwa chama.Mnaipokosoa CCM mjue mnakisaidia kujiimarisha,mlipowakosoa bungeni kwa hoja moto moto mkawasaidia kujirekebisha ktk kumpata mgombea wa urais asiye na makando makando,kama sio CHADEMA CCM wangeendelea kutawaliwa na mafisadi.Umefika wakati sasa muanze kuwakosoa akina Mbowe ili mkiimarishe CHADEMA.
Absolutely right!! Kama kuna utaratibu uliwekwa kwa wakati fulani ili kukithi mahitaji ya wakati huo usifanywe sasa ndiyo sheria. Kwanza utaratibu huu ni nje ya katiba ya Chama na unakandamiza demokrasia na kazi ya Chama.Tunasema kila siku Kazi ya Chama ni kusimamia serikali halafu


Utaratibu wowote ndani ya taasisi huandikwa na hupitishwa na wanachama. Huu utaratibu wa kuachiana madaraka uliandikwa na nani na ulipitishwa na kikao gani
 
Watu mnajadili mambo ya katiba lakini hakuna hata quotations mnazonukuu halafu mnategemea mtafikia hitimisho kweli?

Wekeni vifungu hapa tuone ipi pumba upi mchele.
 
Huh haupo kisheria Bali ni desturi ya ccm ,!!

Wakimaanisha. Chama kushika hatamu +!!

Yaani wanataka Mkiti atembee Na kofia mbili !!!

Kwa ujumla ni desturi ya kulindana !!
 
CCM ni chama kinachojinasibu kwamba ni chama cha kidemokrasia! Aidha katiba ya chama hicho inaainisha wazi kwamba kila mwanachama ana haki ya kugombea nafasi yoyote ile ikiwemo ya mwenyekiti wa chama Taifa.

Katiba inaeleza pia muda wa viongozi wa chama hicho kukaa madarakani ni miaka mitano kila baada ya uchaguzi.

Leo hii tunaona figisufigisu zimeanza za kutaka kumng'oa madarakani mwenyekiti Kikwete kabla ya muda wake kwisha kinyume na katiba.Tumesikia pia eti kuna mpango wa 'kumkabidhi' madaraka ya mwenyekiti wa Taifa Rais Magufuli.

Tulitarajia kusikia wanachama wakitangaziwa tarehe ya kuchukua fomu ya kugombea nafasi hiyo ili atakayeshinda ndiyo akiongoze chama hicho lakini huko kinachotaka kufanyika ni ukiukwaji mkubwa WA demokrasia na katiba ya chama hicho.

Haya yangefanyika kwenye vyama vingine vya siasa tungesikia kelele nyingi kutoka CCM na vyombo vyama vya propaganda ikiwemo ofisi ya msajili WA vyama vya siasa. Tuliona jinsi msajili alivyoingilia uchaguzi wa CHADEMA mpaka kufikia hatua ya kutaka kuwapangia nani agombee na nani asigombee!

Tunamtaka msajili aingilie kati ukiukwaji huu WA demokrasia na katiba ya chama hicho unaofanywa na CCM. Najiuliza kama wanasigina katiba ya chama chao wataweza kuilinda katiba ya nchi?
Aisee hapo umegusa penyewe sasa tunawakaribisha wale viwavi wanao kesha wanachonga midomo yao juunya vyama vingine kukosa demokrasia,njooni hapa nyie viwavi mkanushe haya
 
Huko Chadema kuna demokrasia?
Huu uzi unawahusu ccm,hizo habari za cdm wachana nazo kwanza tuchangie hoja iliyopo mezani kwanini ccm mnaibaka demokrasia?kwani jk kawafanyia nini baya hadi mtake kumg'oa?
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom