Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,299
- 33,082
Na GPL Ripota
Miamba inayofanya makubwa katika Muziki wa Kizazi Kipya nchini, Farid Kubanda a.k.a Fid Q na Seleman Msindi a.k.a Afande Sele, ndiyo inayokamuana katika Nani Zaidi wiki hii...
Hawa ni wakali wa Bongo Fleva ambao walianza game kitambo, lakini walikubalika zaidi kuanzia miaka ya 2002 na kuendelea.
Wana pini kibao ambazo ziliwafanya waendelee kuwa kileleni, lakini songi kama Mwanza Mwanza lake Fid Q na Kingdom wake Afande Sele ambaye pia aliwahi kuwa Mkali wa Rymes zimekaa vizuri ile mbaya.
Sasa tuambie, kwa maoni yako, kwa jinsi unavyowafahamu wakali hawa, unadhani nani anastahili kuwa mbabe wa mwenzake? Toa maoni yako hapo kwenye poll, juu kulia.