Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,314
- 33,108
MBUNGE wa Arusha Mjini kwa tiketi ya CCM, Felex Mrema jana alihojiwa kituo cha polisi kwa zaidi ya dakika 40 kwa tuhuma za kumtishia maisha mwandishi wa habari.
Habari zilizolifikia gazeti hili zimeeleza kuwa mbunge huyo alikamatwa jana majira ya saa 7:00 mchana na kuhojiwa katika kituo kikuu cha polisi mjini hapa kwa kutoa maneno ya vitisho kwa mwandishi wa gazeti la Arusha Raha, Fortunatus Rutta.
Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha, Matei Basilio alithibitisha taarifa za kuhojiwa kwa mbunge huyo kwenye kituo hicho kikuu cha polisi mjini hapa.
Mbunge huyo anadaiwa kutoa maneno ya vitisho kwa mwanadishi huyo baada ya kuripoti taarifa ambazo mbunge huyo hakutaka ziandikwe.
Habari iliyomchukiza mbunge huyo ni ile iliyotolewa na gazeti hilo na kueleza kuwa yupo katika hali mbaya kisiasa na kwamba kundi linalosadikiwa kumpigia kampeni limeanza mbio hizo mapema na kabla ya wakati muafaka.
Ilidaiwa kuwa mbunge huyo pia amekuwa akitumia majukwaa kujipigia kampeni mapema kwa wazi licha ya kushutumiwa na baadhi ya viongozi wa chama chake kwa kukiuka ratiba yao.
Mbunge huyo pia aliripotiwa na gazeti hilo kuwa aliingiza mila na desturi za mila ya Kimaasai katika eneo la Terat alipofanya ziara hivi karibuni na kukutana na vikwazo baada ya baadhi ya wananchi kukataa mbunge huyo kuhutubia kwa sababu mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kuhoji alikuwa wapi miaka iliyopita.
Mara baada ya taarifa hizo, mbunge huyo anadaiwa alimtishia kwa maneno mwandishi huyo katika eneo la Manispaa ya Arusha na kumweleza kwamba siku zake za uandishi wa habari zinahesabika kwa sababu taarifa anazoandika dhidi yake, hazimpendezi.
Kamanda Basilio alisema kuwa sheria haichagui mtenda kosa na kwamba taratibu hizo zikikamilika, mbunge huyo ataitwa na jeshi hilo na sheria kufuata mkondo.
Mmoja wa viongozi wa Chama cha Waandishi wa Habari Arusha (APC), Claud Gwandu, ambaye pia ni mhariri mkuu wa gazeti hilo, alisema kuwa ni kweli mwanadishi wake ametishiwa na taarifa zimeshafikishwa kituo kikuu cha polisi na kwamba wanasubiri atiwe mbaroni.
"Mpaka jana tulishaandika maelezo na tunasubiri Jeshi la Polisi limtie mbaroni na kufuatwa kwa taratibu nyingine," alisema Gwandu.
Chanzo: Gazeti la Mwananchi
Habari zilizolifikia gazeti hili zimeeleza kuwa mbunge huyo alikamatwa jana majira ya saa 7:00 mchana na kuhojiwa katika kituo kikuu cha polisi mjini hapa kwa kutoa maneno ya vitisho kwa mwandishi wa gazeti la Arusha Raha, Fortunatus Rutta.
Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha, Matei Basilio alithibitisha taarifa za kuhojiwa kwa mbunge huyo kwenye kituo hicho kikuu cha polisi mjini hapa.
Mbunge huyo anadaiwa kutoa maneno ya vitisho kwa mwanadishi huyo baada ya kuripoti taarifa ambazo mbunge huyo hakutaka ziandikwe.
Habari iliyomchukiza mbunge huyo ni ile iliyotolewa na gazeti hilo na kueleza kuwa yupo katika hali mbaya kisiasa na kwamba kundi linalosadikiwa kumpigia kampeni limeanza mbio hizo mapema na kabla ya wakati muafaka.
Ilidaiwa kuwa mbunge huyo pia amekuwa akitumia majukwaa kujipigia kampeni mapema kwa wazi licha ya kushutumiwa na baadhi ya viongozi wa chama chake kwa kukiuka ratiba yao.
Mbunge huyo pia aliripotiwa na gazeti hilo kuwa aliingiza mila na desturi za mila ya Kimaasai katika eneo la Terat alipofanya ziara hivi karibuni na kukutana na vikwazo baada ya baadhi ya wananchi kukataa mbunge huyo kuhutubia kwa sababu mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kuhoji alikuwa wapi miaka iliyopita.
Mara baada ya taarifa hizo, mbunge huyo anadaiwa alimtishia kwa maneno mwandishi huyo katika eneo la Manispaa ya Arusha na kumweleza kwamba siku zake za uandishi wa habari zinahesabika kwa sababu taarifa anazoandika dhidi yake, hazimpendezi.
Kamanda Basilio alisema kuwa sheria haichagui mtenda kosa na kwamba taratibu hizo zikikamilika, mbunge huyo ataitwa na jeshi hilo na sheria kufuata mkondo.
Mmoja wa viongozi wa Chama cha Waandishi wa Habari Arusha (APC), Claud Gwandu, ambaye pia ni mhariri mkuu wa gazeti hilo, alisema kuwa ni kweli mwanadishi wake ametishiwa na taarifa zimeshafikishwa kituo kikuu cha polisi na kwamba wanasubiri atiwe mbaroni.
"Mpaka jana tulishaandika maelezo na tunasubiri Jeshi la Polisi limtie mbaroni na kufuatwa kwa taratibu nyingine," alisema Gwandu.
Chanzo: Gazeti la Mwananchi