Fedha za serikali au za umma?

Dark City

JF-Expert Member
Oct 18, 2008
16,253
11,597
Mara nyingi nimekuwa nikisikia viongozi wengi wakisema serikali haiwezi kutumia pesa zake kwa hili au lile. Hivi karibuni, Naibu waziri wa Elimu G Kabaka akaririwa akisema kuwa pesa za serikali haziwezi kutumika kumlipia kila mwanafunzi wa elimu ya juu. Mimi ninavyojua serikali imepewa jukumu na wananchi kukusanya kodi kwa niaba yao na kusimamia matumizi ya pesa hizo baada ya wananchi wenyewe (kupitia kwa wabunge wao) kuiambia jinsi ya kuzitumia. Sasa naomba nieleweshwe, hizi ni pesa za serikali au za umma? Maana huu mkanganyiko ndio unaosababisha pesa za umma (kama ninavyoamini mimi) zionekane kama hazina mwenye nazo na ni halali ya kila kibaka anayeweza kupata upenyo wa kuzikaribia. I think we need to be clear on this.
 
hapo umeongea mazee,

hawa jamaa wakishakaa kwenye 'system' wanasahau walikotoka. Wanasahau kwamba na wao walipitia elimu ya juu. tena enzi zao walikua wanagomea msosi.

Kama inawezekana kuwapa wafanyabiashara mikopo nchi nzima kwa nini wasiweze kuwapa hao watoto wa maskini. inashangaza kuona Serikali ya Tanzania haioni umuhimu wa kuwekeza katika elimu. Hivi do they know kwamba the next Tanzania will lie on the hands of the current higher education students/ au wanataka waharibu mfumo mzima wa elimu ya Tanzania, ili watoto wao na ndugu zao ambao wamesoma 'majuu' wathaminike hata kama wamesoma vyuo batili.

Inasikitisha kuona ni jinsi gani serikali yetu isivyojali kuboresha sekta ya Elimu. Ni vyema watoe mikopo ya ada 100% alaf hizo fedha za matumizi wazigawe kwa 'grades'.

Unaposhindwa kutoa fedha za Ada unategemea chuo kitajiendeshaje? Chuo kinategemea serikali, serikali inatupia mzigo kwa wananchi. Mboa mizigo yao inawatosha tayari. Imagine mtu wa kipato cha chini "Tsh. 80,000" anayeishi hapa dar es Salaam. Igawe hiyo hela yake kwa ajili ya Nauli, Chakula, Malazi, Matibabu alafu ubakishe 20% ya ada ya mwanafunzi mmoja wa chuo kikuu.

Mimi ninaamii kwa MIPANGO thabiti, serikali kutoa 100% kwa wanafunzi wote inawezekana.

kama wanashindwa sasa hivi basi watambue hawatokaa waweze kulipia hata 20% ifikapo 2015. kwa mtu wa kawaida anaweza akaona nchi inapoelekea. kama Elimu ya Msingi ni bure sasa hivi, Elimu ya sekondari na yenyewe ni 'Kama bure'. Shule za msingi na sekondari zinaongezeka kila kukicha. kizazi kijacho kitakua kimezoea 'Elimu ya bure' na hawatokua na 'MAADILI'.

MIPANGO thabiti inahitajika ili kuikomboa sekta ya Elimu, La sivyo Tanzania itaangukia kwenye mikono ya wasomi wasio na akili (EDUCATED FOOLS) ambao wanajali maslahi binafsi tu.
 
Nashukuru sana SS kwa mchango wako. Hata hivyo naomba kueleza kuwa lengo la thread hii haikuwa kujadili suala la mikopo kwa sababu linajadiliwa sehemu nyingine humu JF. Lengo langu ni kupata mawazo ya wadau. Je tuseme pesa ni za serikali au ni pesa za umma? Nchi za wenzetu wanaita public funds na matumizi yake yanakuwa public expenditures. Ila hapa kwetu nasikia ni government funds na kwa hiyo government expenditures. Naomba michango yoyote ya mambo ya mikopo ya wanafunzi (ambapo jambo hili limetumiwa kama mfano kwenye thread hii) iende kwenye thread huska. Nitashukuru sana kupata michango ya wadau.
 
Nashukuru sana SS kwa mchango wako. Hata hivyo naomba kueleza kuwa lengo la thread hii haikuwa kujadili suala la mikopo kwa sababu linajadiliwa sehemu nyingine humu JF. Lengo langu ni kupata mawazo ya wadau. Je tuseme pesa ni za serikali au ni pesa za umma? Nchi za wenzetu wanaita public funds na matumizi yake yanakuwa public expenditures. Ila hapa kwetu nasikia ni government funds na kwa hiyo government expenditures. Naomba michango yoyote ya mambo ya mikopo ya wanafunzi (ambapo jambo hili limetumiwa kama mfano kwenye thread hii) iende kwenye thread huska. Nitashukuru sana kupata michango ya wadau.

TAFAKARI.
Ukipambanua utofsuti wa haya yafuatayo unaweza kupata majibu

Serikali Vs Umma

Government expenditure vs Public Expenditure
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom