Patriote
JF-Expert Member
- Jul 13, 2011
- 1,718
- 1,047
KAMATI ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), imebaini ufisadi mwingine wa mabilioni ya fedha kwenye marejesho ya zile zilizochotwa awali kifisadi katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA). Fedha hizo zaidi ya Sh50 bilioni zilizorejeshwa na Rais Jakaya Kikwete kutangaza kuwa zitatumika kwa ajili ya kuendeleza shughuli za kilimo nchini, zinadaiwa kuchotwa kwenye Benki ya Rasilimali Tanzania (TIB) kwa amri iliyotoka kwa vigogo serikalini.
Mkurugenzi wa TIB, Peter Noni alikiri jana mbele ya POAC kuwa sehemu ya Sh20 bilioni zilizotolewa na Hazina kwenda kwenye benki hiyo kwa ajili ya dirisha la kilimo, Serikali iliamuru zitolewe kama mkopo kwa wafanyabiashara ambao iliwataja kwa majina.Mkurugenzi wa TIB, Peter Noni alikiri jana mbele ya POAC kuwa sehemu ya Sh20 bilioni zilizotolewa na Hazina kwenda kwenye benki hiyo kwa ajili ya dirisha la kilimo, Serikali iliamuru zitolewe kama mkopo kwa wafanyabiashara ambao iliwataja kwa majina.
Ingawa baadhi ya wabunge walimtaka mkurugenzi huyo wa TIB awataje kwa majini vigogo hao, Makamu Mwenyekiti wa POAC, Deo Filikunjombe, alisita na kumtaka Noni asitaje majina hayo. Noni alitaja mbele ya kamati hiyo kuwa moja ya kampuni zilizochukua fedha hizo na sasa zinaonyesha wasiwasi katika kuzirejesha ni Simon Group Ltd. Nyingine ni kampuni tano za kuuza maua nje ya nchi zenye makao yake makuu mjini Arusha, zikiwepo Tengeru Flowers na Mount Meru Flowers.
Kwa kweli sakata la EPA ni ufisadi taslimu na linatia kichefuchefu sana. Toka Rais alipomteua Peter Noni kuwa Mkurugezi TIB nlijua lengo ilikuwa ni kufanya haya yaliyotokea. Peter Noni alihusika katika wizi wa fedha za EPA akiwa mfanyakazi BOT. Hivyo kuteuliwa kwakwe kuiongoza TIB ilikuwa ni kuhadaa wananchi na kuficha ukweli.
Kwa Rais kumteua mtuhumiwa wa wizi wa EPA kuiongoza TIB na Baadaye kutudanganya kuwa hizo hela keshazipeleka TIB na kumkabidhi Peter Noni ni kutufanya wananchi viazi, wapumbavu na mazezeta. Kimsingi hapa Rais amejipambanua kama mhusika ktk hili sakata la EPA. Ukichunguza kwa undani unaweza kukuta hizo fedha hazikupelekwa kabisa TIB, ila kwa kuwa TIB inaongozwa na mtuhumiwa wa huo ufisadi tumedanganywa tu.
Hivi nini hasa sababu ya sisi wananchi kufanywa wapumbavu??Hivi Rais hakuona mwingine wa kumweka TIB zaid ya huyu Peter Noni ambaye ni mtuhumiwa wa EPA pia???hivi kweli sisi wananchi hatuna cha kufanya katika ujinga kama huu???kwann tuliowaamini kutuongoza leo wamekuwa wanatuhujumu??Nini hasa sababu ya kuwa na serikali isiyoaminika kama hii? Kama inashindwa kuaminika kwa fedha ndogo kama hizi kwa nn tuwaamin kwa kuwaachia nchi na rasilimali zake?
Hivi hakuna utaratibu wa kuondoa viongozi wezi kama hawa? Nani aliyeiamuru TIB kukopesha hao walioshindwa kurudisha hizo fedha???Naomba tumjue aliye amuru, PCCB, wataalam wa Intellejensia (KOVA na Mwema) hamuoni kama kunaharufu ya Rushwa hapo???Hakuna kitu mnaweza fanya hapo kwa Kiongozi aliyeagiza hela ya wananchi zitoke kienyeji?
Kwa utaratibu huu wa kutoa mikopo kwa kujuana, TIB itasurvive? Tunapoelekea naona Serikali itatutia kidole jichoni, nadhani inatosha.................................Nakaribisha mawazo yenu wanaJF nn kifanyike kukomesha hii hali.
Mwananchi 03/11/2011​
Mkurugenzi wa TIB, Peter Noni alikiri jana mbele ya POAC kuwa sehemu ya Sh20 bilioni zilizotolewa na Hazina kwenda kwenye benki hiyo kwa ajili ya dirisha la kilimo, Serikali iliamuru zitolewe kama mkopo kwa wafanyabiashara ambao iliwataja kwa majina.Mkurugenzi wa TIB, Peter Noni alikiri jana mbele ya POAC kuwa sehemu ya Sh20 bilioni zilizotolewa na Hazina kwenda kwenye benki hiyo kwa ajili ya dirisha la kilimo, Serikali iliamuru zitolewe kama mkopo kwa wafanyabiashara ambao iliwataja kwa majina.
Ingawa baadhi ya wabunge walimtaka mkurugenzi huyo wa TIB awataje kwa majini vigogo hao, Makamu Mwenyekiti wa POAC, Deo Filikunjombe, alisita na kumtaka Noni asitaje majina hayo. Noni alitaja mbele ya kamati hiyo kuwa moja ya kampuni zilizochukua fedha hizo na sasa zinaonyesha wasiwasi katika kuzirejesha ni Simon Group Ltd. Nyingine ni kampuni tano za kuuza maua nje ya nchi zenye makao yake makuu mjini Arusha, zikiwepo Tengeru Flowers na Mount Meru Flowers.
Kwa kweli sakata la EPA ni ufisadi taslimu na linatia kichefuchefu sana. Toka Rais alipomteua Peter Noni kuwa Mkurugezi TIB nlijua lengo ilikuwa ni kufanya haya yaliyotokea. Peter Noni alihusika katika wizi wa fedha za EPA akiwa mfanyakazi BOT. Hivyo kuteuliwa kwakwe kuiongoza TIB ilikuwa ni kuhadaa wananchi na kuficha ukweli.
Kwa Rais kumteua mtuhumiwa wa wizi wa EPA kuiongoza TIB na Baadaye kutudanganya kuwa hizo hela keshazipeleka TIB na kumkabidhi Peter Noni ni kutufanya wananchi viazi, wapumbavu na mazezeta. Kimsingi hapa Rais amejipambanua kama mhusika ktk hili sakata la EPA. Ukichunguza kwa undani unaweza kukuta hizo fedha hazikupelekwa kabisa TIB, ila kwa kuwa TIB inaongozwa na mtuhumiwa wa huo ufisadi tumedanganywa tu.
Hivi nini hasa sababu ya sisi wananchi kufanywa wapumbavu??Hivi Rais hakuona mwingine wa kumweka TIB zaid ya huyu Peter Noni ambaye ni mtuhumiwa wa EPA pia???hivi kweli sisi wananchi hatuna cha kufanya katika ujinga kama huu???kwann tuliowaamini kutuongoza leo wamekuwa wanatuhujumu??Nini hasa sababu ya kuwa na serikali isiyoaminika kama hii? Kama inashindwa kuaminika kwa fedha ndogo kama hizi kwa nn tuwaamin kwa kuwaachia nchi na rasilimali zake?
Hivi hakuna utaratibu wa kuondoa viongozi wezi kama hawa? Nani aliyeiamuru TIB kukopesha hao walioshindwa kurudisha hizo fedha???Naomba tumjue aliye amuru, PCCB, wataalam wa Intellejensia (KOVA na Mwema) hamuoni kama kunaharufu ya Rushwa hapo???Hakuna kitu mnaweza fanya hapo kwa Kiongozi aliyeagiza hela ya wananchi zitoke kienyeji?
Kwa utaratibu huu wa kutoa mikopo kwa kujuana, TIB itasurvive? Tunapoelekea naona Serikali itatutia kidole jichoni, nadhani inatosha.................................Nakaribisha mawazo yenu wanaJF nn kifanyike kukomesha hii hali.
Mwananchi 03/11/2011​