Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 10,773
- 2,545
Nimekaa mbele ya tv yangu nikitazama chanel ya fashion tv kupitia king'amuzi nikisubiri mechi ya udachi na hispania kuanza. Wanapita vijana wa kiume walio na miili ya kiume hasa katika mavazi tofauti kuanzia suti hadi boxer. Vifua vimetanuka, matumbo flat, misuli miguuni na mikononi na nyuso mvuto. Hii pia ni kwa mabinti. Ina maana imefanyika segmentation kwa ajili ya watu kama hao tu? Mbona dunia hii ina kila aina ya shepu? Mbona hawana uwakilishi katika fashen show? Mbona hao wabunifu wana miili mikubwa tofauti na wanachotangaza? Mcheki idarus, hasanal ndo kashtuka na kwenda kujikondesha. Hawa jamaa huwalenga nani katika ubunifu wa mavazi? Angalia matoy kwenye maduka ya mavazi.