Japo ni vigumu kumwuliza Mungu, lkn kwa hili nina haki ya kumwuliza Mungu kwanini amemchukua Regia wakati bado ni Tumaini la wengi? ... Amen!
Nyota iliyozimika ghafla.
ni mlemavu ambae alisimama imara ktk mstari wa mbele wa mapambano,...
Kwaheri kamanda umetutangulia nasi tuko nyuma tunakuja, sina namna ya kuelezea msiba huu...Mungu awape moyo wa subira
the good die young..!!!
Wakati mwingine najiuliza "Why Regia?". Kwa nini Mungu kakuchagua Regia? Mbnona ndo kwanza ulianza kukusanya kero zetu kupitia humu mtandaoni [...] Why now?.
"Bwana ametoa na Bwana ametwa jina lake libarikiwe"
Ameen.
Jamani jamani,why had she to go when we need her so much, ...machozi
Kazi ya Mungu haina makosa.Regia sijui niseme nini [...] Niseme nini basi! Maneno yameniishia na machozi yananilengalenga. Oh Mungu wangu.Pumzika kwa amani Regia.Tutakutana Paradiso siku hiyo!
Nyota Imezimika
Ni kweli Nyota ya Regia imezimika Duniani, inasikitisha na inauma sana!
Hatutaitenda haki Tanzania kama hatutaweka ukweli na kujifunza kutokana na makosa hili tusiendele kupoteza na kuzima taa ambazo tunazitegemea kama hii ya Regia kwa kuendeleza tabia na mila yetu ya kusifu na kukwepa ukweli kwa kuwa kwetu sisi Watanzania kukwepa ukweli na kuishi kama bendera fuata upepo ndio uungwana!
Wakati kifo cha Regia kinauma na kunisikitisha hakika roho yangu inanituma kuuliza kwanini alikuwa anajiendesha mwenyewe katika Barabara za Tanzania, tena Long Safari na tena barabara ya Dar - Moro?! Huku kodi yetu ikikatwa kwa ajili ya madereva wa Wabunge wetu wapendwa, ukiachilia mbali maumbile ya Regia na kazi ya Ubunge inavyohitaji kufikiri na kuwaza kila wakati kama siyo kila dakika!
Najuwa kwa mila na uwezo wetu wengi mtashangaa haya maswali yangu, ila "smart people learn from others mistakes" kama hatutaki kuendelea kuwapoteza wapendwa wetu lazima tuwaambie ukweli na kuwaepusha na mazingira hatarishi. Wabunge waache kujiendesha wenyewe, hasa katika safari ndefu, na pale afya zao zisipowahurusu pia waheshimu hilo.
Regia tulikupenda sana, umetutoka wakati bado tunakupenda mwenyezi Mungu akurehemu.
I mean, ni kwa namna gani unaweza kukielezea kifo cha role model kama Regia?
Kama watu wakifa hua wanaona waliobaki huku wanareact vipi kwa kuondoka kwao basi atakua anatabasamu sasa hivi huku machozi yakimtoka.
RIP RM.