Huko kwenye halmashauri zetu ndiko kuna matatizo makubwa kwahiyo tukipata wasomi wengi kwenye level ya udiwani basi hapo tunakuwa na mabaraza ya halmashauri yaliyo mahiri na makini, na bila shaka utekelezaji wa miradi mingi ya maendeleo hautakuwa wa kusuasua tena kama ilivyo sasahivi.
Na nyie akina Maiko Msafiri, akina Beda Mwang'onde na wasomi wengineo igeni mfano huo kule Milo.
Hata mimi nampongeza sana Diwani Mteule Faraja Mlelwa kwa kuamua kwa dhati kutafuta nafasi ya kuwatumikia wananchi kwa nafasi ya udiwani bila kujali kiwango kikubwa cha elimu alicho nacho.
Kumekuwa na tabia za wasomi wengi wa siku hizi kwamba mtu akishakuwa na shahada moja tu yeye anawaza kuwa mbunge tu na si chini ya hapo.
Huko kwenye halmashauri zetu ndiko kuna matatizo makubwa kwahiyo tukipata wasomi wengi kwenye level ya udiwani basi hapo tunakuwa na mabaraza ya halmashauri yaliyo mahiri na makini, na bila shaka utekelezaji wa miradi mingi ya maendeleo hautakuwa wa kusuasua tena kama ilivyo sasahivi.
Hii ni changamoto kwa vijana wengi waliojiunga Chadema kila mmoja aanze kufikiria ni kata ipi inayomfaa kuwawakilisha wananchi kupitia Chadema na waanze maandalizi ili kufikia 2015 tusitarajie tena makapi ya ccm ambayo yamejidhihirisha kuwa hayana msaada wowote kwa ustawi wa chama na maendeleo ya wananchi.