Falsafa za Kambarage

Babu kawalostisha. Wakati wenzetu walifanya juhudi za kumilikisha watu ardhi, Tanzania ilifanya ardhi mali ya serikali.
Kenya wamefanya hivyo, je kuna afadhali? Asilimia 10 ya Wakenya wanamiliki 90% ya ardhi. Mahindi na chakula kinaingia Kenya kupitia Namanga, Horohoro, Taveta n.k. Afadhali ipo wapi?

Nenda sehemu inayoitwa Kisii hadi Kerako uangalie umasikini wa hali na ardhi.
Uganda ardhi ilikuwa ya Kabaka Mutesa, kuna tofauti gani ya masikini wa Arua na yule wa Mtwara?

Nenda Rwanda uone hali ilivyo. Hivi unafikiri agenda ya ardhi kwanini inaleta mzozo ndani ya EAC?

Mkulima anapolima mahindi na kukosa soko, au mkulima anapolima nyanya na kuuza tenga sh 1500, tatizo unadhani ni nini?

Njaa yetu si kwasababu ya matumizi ya ardhi, ni ukosefu wa mipango ya kuwmendeleza mkulima, ukusanyaji wa chakula na hifadhi ya chakula. Huwezi kuacha mahindi yauzwe Malawi Zambia, Kenya, Uganda na Rwanda halafu udhani kuwa ukitoa ardhi hovyo utakuwa umepata suluhu ya njaa.

Kwanini Wasonjo na Wamasai wanagombana hadi FFU ingilie kati! sasa ukiacha asilimia 5 imiliki unadahni kitatokea nini.

Angalia vision ya Nyerere in wide spectrum, sio mashamba tu.
 
1.jpg

he waz a great leader, namkubali sana nyerere, watu wengi hawakumwelewa, watamwelewa baadae sana.
 
Falsafa iliyopitwa na wakati. 5% ya waMarekani ni wakulima na wanalisha nchi zima na kuuza nje. 95% ya watanzania ni wakulima na bado wanatembeza mabakuli.

Acha uzushi, linganisha kwa sasa pato la Taifa la Marekani na pato letu na halafu uangalie GDP yao leo na ulinganishe na thamani ya GDP yao miaka ya 1840 walikokuwa bado wote ni karibu wakulima. Utaona mwelekeo wetu wa kugawa ardhi kwa wageni ni mwelekeo duni. Hatuwezi kuuza ardhi wakati zaidi ya 80% ya wanafunzi wetu wanafeli. Huyo mgeni tunamuuzia ardhi ili nani ajifunze teknolojia mpya toka kwake? Pia hao 5% wanatetea maslahi ya nani? Wao siku zote utasikia kwa hisani na msaada wa watu wa marekani, maana wanafanya kwa ajili ya nchi yao. Mafisadi hawa ni wanyang'anyi na pia mitaaji yao si ya watanzania. Nenda kituo cha uwekezaji utajua vema.

Kumuenzi mwalimu Nyerere, sisi wa-Arumeru tuwakatae waliotudhulumu ardhi yetu kwa kujenga ma-ngurudoto tusipopata hata senti moja itokanayo na ardhi yetu.
 
Siyo kuwa gate keeper lakini kingozi wa nchi anatakiwa kulinda maslahi ya nchi ikiwemo raia sio tu mtu anatoka Iowa anakuja kujichukulia ardhi.

Kwani wewe unafikiri kwanini Marekani huwa wanalazimisha wenyeshea nyingi kwenye kampuni kubwa lazima wawe raia (uliza kilichomfanya Murdock kuchukua uraia wa Marekani miaka ya themanini).Hizi zote ni sera za kulinda wazawa na kuwabana wawekezaji uchwara kwahiyo mwalimu hakukosea kabisa.

Chamoto,

Wakati Nyerere anachukua nchi, kulikuwa hakuna kitu kinachohitwa wawekezaji uchwara au for that matter wawekezaji. Mwekezaji yoyote kwake alikuwa ni BEPARI, KUPE na Mnyonyaji.

Pili kuna makampuni mengi Marekani na ambayo ni makubwa na ambayo ni ya watu kutoka nje. Kwa mfano T-Mobile, ni kampuni la wajerumani. Na ukitaka mifano mingine nipata faraja kukuletea. Hivyo sio kweli kwamba wanalazimisha. Na kama wewe ni mfanyabiashara mwenye mtaji fulani au mtu mwenye kipaji mahiri, ukitaka visa ya kuja marekani kukaa na kufanya shughuli zako utawepewa. Hivyo tusidanganyane hapa.

Kuhusiana na masuala ya ardhi, siasa ya Mwalimu ya umma kumiliki ardhi ilikuwa mbaya na imewafanya kutojua thamani ya ardhi na kushindwa ku-create wealth.
 
Kenya wamefanya hivyo, je kuna afadhali? Asilimia 10 ya Wakenya wanamiliki 90% ya ardhi. Mahindi na chakula kinaingia Kenya kupitia Namanga, Horohoro, Taveta n.k. Afadhali ipo wapi?

Nenda sehemu inayoitwa Kisii hadi Kerako uangalie umasikini wa hali na ardhi.
Uganda ardhi ilikuwa ya Kabaka Mutesa, kuna tofauti gani ya masikini wa Arua na yule wa Mtwara?

Nenda Rwanda uone hali ilivyo. Hivi unafikiri agenda ya ardhi kwanini inaleta mzozo ndani ya EAC?

Mkulima anapolima mahindi na kukosa soko, au mkulima anapolima nyanya na kuuza tenga sh 1500, tatizo unadhani ni nini?

Njaa yetu si kwasababu ya matumizi ya ardhi, ni ukosefu wa mipango ya kuwmendeleza mkulima, ukusanyaji wa chakula na hifadhi ya chakula. Huwezi kuacha mahindi yauzwe Malawi Zambia, Kenya, Uganda na Rwanda halafu udhani kuwa ukitoa ardhi hovyo utakuwa umepata suluhu ya njaa.

Kwanini Wasonjo na Wamasai wanagombana hadi FFU ingilie kati! sasa ukiacha asilimia 5 imiliki unadahni kitatokea nini.

Angalia vision ya Nyerere in wide spectrum, sio mashamba tu.

Ng3,

Wewe unamsoma Nyerere au unachukua quote za watu hapa JF na kuzifanya kuwa vision za Nyerere? Ki-utu na kibinadamu nina mapenzi makubwa na Nyerere. Tunapingana kifalsafa tu.

Wakati Nyerere anatoa quote hii mwaka 1958, GNP ya Somalia ilikuwa kubwa kuliko ya China. Zambia, Ghana zilikuwa na uchumi mzuri kuliko Malaysia.

Mwaka 1958 wakulima Marekani walikuwa matajiri wakubwa. Sasa hivi matajiri wakubwa wanatokana na intellectual capital.
 
Acha uzushi, linganisha kwa sasa pato la Taifa la Marekani na pato letu na halafu uangalie GDP yao leo na ulinganishe na thamani ya GDP yao miaka ya 1840 walikokuwa bado wote ni karibu wakulima. Utaona mwelekeo wetu wa kugawa ardhi kwa wageni ni mwelekeo duni. Hatuwezi kuuza ardhi wakati zaidi ya 80% ya wanafunzi wetu wanafeli. Huyo mgeni tunamuuzia ardhi ili nani ajifunze teknolojia mpya toka kwake? Pia hao 5% wanatetea maslahi ya nani? Wao siku zote utasikia kwa hisani na msaada wa watu wa marekani, maana wanafanya kwa ajili ya nchi yao. Mafisadi hawa ni wanyang'anyi na pia mitaaji yao si ya watanzania. Nenda kituo cha uwekezaji utajua vema.

Kumuenzi mwalimu Nyerere, sisi wa-Arumeru tuwakatae waliotudhulumu ardhi yetu kwa kujenga ma-ngurudoto tusipopata hata senti moja itokanayo na ardhi yetu.

Ukiwa unajibu posti zangu basi jaribu kubakia kwenye mada. Hiyo ya wanafunzi kufeli ina sehemu yake.

Kuhusiana na mada, 1840 uchumi ulikuwa local. 2012 Uchumi hupo kwenye globalization. Hivyo Tanzania ya leo na Marekani ya 1840 ni mapapai na mapera hivyo usijaribu kulinganisha.
 
100% nina uhakika 87 vs 13 ya wataalam wetu wametoka st. maria, kama wakiamua kuacha ufisadi wakaamua kusimamia haki nchi itapata neema lakini wamekalia kula mlungula tu na "proposals" za kunyonya pesa za umma..madiwani si wataalamu halafu wengi wao pia st. maria..nafikiri turudi kwenye basics tuwafundishe watu uzalendo na mapenzi kwa watu na si fedha..wanaweza wakaanza huko kwa st. maria ambao ndio wanaotoa human resources wengi serikali (unfortunelty without positive impact)..

Nyerere alinyang'anya wazalendo wakulima mashamba yao akawapa viongozi wa chama na serikali..mwishowe njaa tupu..

Uchumi na siasa vitu viwili tofauti mkuu

Shida hapa sio wataalam kutoka St. maria au Al farouq, tatizo ni sera za chama tawala za Chukua Chako Mapema kwa Ari zaidi, Nguvu zaidi na Kasi zaidi ambazo wanazitekeleza
 
@ Jasusi

Tatizo ni ardhi kutopewa wazalendo wakulima badala yake wakachukua serikali (wakati wa nyerere)..kosa kwanza

Serikali ya sasa (baada ya nyerere) walitakiwa wawape wakulima wazalendo badala yake wanawapa wawekezaji wahuni ..(kosa la pili)..

Bado tunaendelea kufanya makosa sijui hadi lini?

Kama mtu hujui kitu ni bora ukanyamaza siyo lazima uchangie thread. Pima kwanza uwezo wa ubongo wako kufikiri na kuchanganua mambo. Kuvua nguo sehemu husika na kwa wakati husika ni jambo la kawaida, kinyume chake unaonekana mwendawazimu. Kunyamaza pia ni hekima.

 
Back
Top Bottom