Faida katika kiroho

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,955
22,136
FAIDA KATIKA KIROHO
Watafiti wengi wanakiri kwamba kuna sexual energy kama energy zingine ambayo wakati wa sex ikiunganishwa kati ya mwanaume na mwanamke hasa wakati wa kufika kileleni huweza kuwaunganisha wawili in deepest part of of selves.

Na hii energy (non physical) huweza kuimarisha maeneo mengine ya maisha yetu, hutufanya kujisikia ni kitu kimoja na kuwa stronger zaidi katika nafsi na mahusiano kwa ujumla.
Hivyo matokeo ni kujisikia vizuri wewe mwenyewe, mwenzi wako na maisha kwa ujumla


tahadhari


TAHADHARI:
Hii mada ni kwa ajili ya kupeana habari tu (ndiyo maana hakuna reference links, ingawa unaweza mwenyewe ku- Google),
Jambo la msingi ni kwamba kuna umuhimu wa hali ya juu sana kuzingatia kwamba hapa tunazungumzia sex katika ndoa tu na si zaidi ya hapo.
Pia ni muhimu kuzingatia kwamba ili kushiriki sex ni muhimu kuangalia afya ya mwenzi wako, maadili na kutii sheria na amri za Mungu otherwise badala ya sex kukupa afya inaweza kukuua kimwili na kiroho.

Upendo daima!


 
[h=3]Ni kuingia tu![/h]

Kawaida ikiona kuna alama ya NO EXIT kuingia humo lazima ufikiria mara mbili Kitendo cha kutoa ahadi kwamba Hadi kifo kitakapotutengenisha ukweli binadamu unakuwa ume –launch moja ya ahadi za pekee duniani.
No turning back, no escape route kulia au kushoto, wawili mnaingia kwenye life boat, hakuna kwa kwenda zaidi ya kubaki na huyo umemkubali.

Ukweli ni kwamba mtu mwenye akili timamu akiambiwa nyumba unayoingia haina EXIT atafikiria kwa makini zaidi na zaidi ya mara mbili.

Kazi yako ipo well defined hakuna kutoka, hapa nazungumzia mtu ambaye kweli yupo serious kwanza kuhakikisha ndoa yake inampa Mungu utukufu na kwamba Kristo ni Bwana katika maisha yake.
Na kwamba suala la dini na imani ni muhimu sana kwake otherwise hakuna shida.
Mambo ambayo wakati mwingine huleta shida sana kwenye ndoa ni dini, rangi (race) na taifa hata hivyo linaloweza kuwa mwiba mkali ni suala la dini.

General rule ni kwamba
“The more couples have in common the better the chance of success”

Ukweli unabaki palepale kwamba waumini wa kweli wa dini tofauti (let say muislam wa swala tano na mkristo aliyeokoka) wakioana kuna uwezekano mkubwa kukumbwa na matatizo yanayohusiana na dini katika ndoa yao.
(Najua ukianza kuzungumzia dini unaweza kuwasha moto ambao kuzima ni ngumu hata hivyo lazima kuongea ukweli)

Watu ambao hupuuza hiki kipengele baada ya kuoana wanayo ya kusimulia kwa masikitiko.
Jambo la msingi kabla ya kuoa au kuolewa ni vizuri kupata solution ya suala la dini au suala la imani, usijidangany kwamba mkioana utanyoosha kwa pasi ya umeme kirahisi suala la hili la dini, hapa unahitaji kuwa genius tumia akili zako zote kuhakikisha umejua nini hatima yake.

Unaweza kuvuka mito mingi tu lakini mto wa dini ni lazima uvuke ukiwa makini kabisa maana unaweza kuzama mbele ya safari.

Je, mtasali wapi na kivipi, na watoto wakizaliwa watakuwa dini gani na dini ya mwenzako ina amini vipi kuhusu ndoa?
Ni maswali ya msingi sana.

Wengi huona hii ni issue ndogo sana na tutakabiliana nayo tukiona sasa muhimu ni love maana nampenda kuliko suala la dini.
Ukweli vitu vidogo ndo hupelekea ndoa kwenda shimoni.
Na kuacha kujadili sasa haiwezi kumaliza tatizo baadae, kumbuka
“the sooner the better”
au niseme
“the more you solve now the greater your compatibility later.

Imani ya dini ni moja ya njia mke na mume huwa connected, dini ni big deal na zaidi ili ndoa iwe strong haina budi kuwa na 3 layers yaani connection ya kimwili, kihisia (emotions) na kiroho na bond ambayo hushika ndoa (siyo sex) mara nyingi ni kiroho.

"Marriage is not a trial like foreign dish sampled to see if it is tasty"
 
[h=3]Ni moto[/h]

Sex ni zawadi murua kutoka kwa Mungu yenye makusudi ya ajabu.
Sex hutufanya kuzaliana, kujenga upendo (mutual love au one flesh) pia ili tujisikia raha (pleasure).
Sex ni God given drive kama vile tunavyojisikia njaa, ili tule Mungu aliweka ndani yetu kujisikia njaa. Na ili tuzaliane, kujenga upendo na ku-enjoy kati ya mume na mke katika ndoa Mungu aliumba sex, Mungu ndiye ame-innovate sex si binadamu.

Sex ni kitu ambacho kina nguvu sana na uwezo wa ajabu (powerful) kinachoweza kuharibu na pia kupotoshwa na binadamu.

Sex ni kama moto, uweza kukufanya ujisikie joto kama kuna baridi ila huo moto ukishindwa kuithibiti unaweza kuchoma nyumba yako au misitu na kuweza kukuua.
Watu wengi sasa wamekufa kwa sababu ya sex kama vile magonjwa ya zinaa kama UKIMWi, Kisonono, Kaswende nk.

Wengine wameachwa na wake zao au waume zao na kuzifikisha familia nje ya ndoto zao na maumivu makali wka watoto.
Wengine wamekatwa mapanga na wengine kupata ngeu za kila aina kwenye miili yao.
Wengine hawana amani maana siri walizoziweka ndani ya mioyo yao kuhusiana na sex zinawatafuna kila siku.
Ni kama vile aibu kuona watu wanapata maafa na wengine kufa kutokana na bado decisions kuhusian na sex.

Kama hujaolewa au kuoa kumbuka kusubiri (abstinence) ni uamuzi wa busara kuliko kujiingiza kwenye mapenzi kabla ya ndoa.
Kama umeoa au kuolewa kumbuka mapenzi nje ya ndoa ni janga kubwa kuliko unavyofikiria.

Kwa Mungu hakuna lisilowezekana:(Luka 1:37)
 
Ni kweli shwala la imani ni la muhimu sana nalakuzingatia ktk. mahusiano yanayoelekea kwenye ndoa.
 
Back
Top Bottom