Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
Mficha maradhi mwisho humwumbua. Yalisemwa, yanasemwa na viongozi wa juu wameamua yaendelee kama yalivyo kwani kuyafanyia kazi inawawia vigumu kwa kuwa wahusika ni wao na kila wanakogeukia wanajitazama wao wenyewe, sawa na hadithi ya nyani utamwonea huruma kumpiga atakavyoonyesha huruma wakati akikuibia mahindi yako, lakini kesho utakaporudi kushuhudia mabua tu shambani ndipo utakapojawa na simanzi lisilo kifani.
Kama kuna wenye malengo ya kukalia Ikulu kwa mwendo huu inatia shaka ushupavu walio nao, maana kuna kila dalili ya mgawanyiko, hawa ni vijana wenye ile motomoto wanaolipuka kwa kasi kama moto wa gas, lakini kuna kundi jingine ambalo halionyeshi hamasa kwa uwazi ile yamebaki moyoni mwao, nini watafanya kwa yanayojilia wao wenyewe ni siri yao wanajua. Bora anayeonyesha kwa uwazi una nafasi ya kumsoma na kutafuta tahadhari, lakini kwa wenye kuficha hisia zao ipo siku itabaki duwazo lisilotabirika.