Fahamu tafsiri sahihi ya "computer" kwa kiswahili.

Inside10

JF-Expert Member
May 20, 2011
26,060
23,940
Waswahili wengi hufikiri kwamba hakuna maana halisi ya computer na badala yake wanatohoa neno hilohilo nakuandika "Kompyuta". Hivyo ni makosa maana halisi ya Computer ni neno "NGAMIZI" na kwa laptop computer huitwa "NGAMIZI PAKATWA" Source: Ulimwengu wa kiswahili TBC1, Nawasilisha.
 
Mh! nakumbuka kuna mtu alishawahi kusema, je TARAKILISHI na NGAMIZI ni sawa? maana mimi naifahamu kuwa ni Tarakilishi
 
Nawalaumu sana hao wanatoa tafsiri za maneno na vitu mbalimbali. Tukiangalia kwa uzuri lugha ni muingiliano wa lugha mbalimbali. Ndio maana tuna maneno bora kama shati, meza, chai, pesa, hela, gari n.k. Hivi kwa nini fan iitwe pangaboi badala ya feni tulivyozoea? Computer ingekuwa komputa, television ingekuwa televisheni, fax mashine ingekuwa faksi n.k. Hakuna ubaya kuiga. Lugha zote zinaiga.
 
Congo nakubaliana na wewe ila nafikiri computer ingeitwa kompyuta badala ya komputa!
 
Congo nakubaliana na wewe ila nafikiri computer ingeitwa kompyuta badala ya komputa!
La muhimu hapa kwa mawazo yangu ni kuwa kitu tumekitumia kwa miaka nenda rudi kwa jina fulani. Wataalamu wanakuja na majina ya ajabuajabu. Ah nimekumbuka, calcultor inaitwa kikokotozi, ovyo kabisa. Tungesema kalikuleta. Asante.
 
Eti kiwembe cha kuchongea pencils kinaitwa KIFIRIO. Duh kazi kweli kweli.
 
La muhimu hapa kwa mawazo yangu ni kuwa kitu tumekitumia kwa miaka nenda rudi kwa jina fulani. Wataalamu wanakuja na majina ya ajabuajabu. Ah nimekumbuka, calcultor inaitwa kikokotozi, ovyo kabisa. Tungesema kalikuleta. Asante.

Ninajaribu kukuelewa: unaona kama ni kupoteza wakati na rasilimali kutafuta tafsiri ya 'Kiswahili' ya maneno hasa yanayohusiana na sayansi na teknolojia. Unadhani hakuna haja ya kuwa na istilahi mpya, unataka tuendelee na 'utohozi'.

Sioni shida sana ingawa sikubaliani na wewe kwenye baadhi ya maeneo.

Lakini, huu u--'hovyo' unaouona umeutoa wapi?
 
Ninajaribu kukuelewa: unaona kama ni kupoteza wakati na rasilimali kutafuta tafsiri ya 'Kiswahili' ya maneno hasa yanayohusiana na sayansi na teknolojia. Unadhani hakuna haja ya kuwa na istilahi mpya, unataka tuendelee na 'utohozi'.

Sioni shida sana ingawa sikubaliani na wewe kwenye baadhi ya maeneo.

Lakini, huu u--'hovyo' unaouona umeutoa wapi?


Nakubaliana na wewe kabisa lugha hukua hasa ukizingatia kuwa tupo katika ulimwengu wa sayansi na teknolojia na kuwa kuongeza istilahi si lazima utohoe au uangalie mazoea ya matumizi ya neno husika, tutatohoa hadi lini wakati uwezekano wa kutafuta istilahi mpya upo? kiswahili si maskini kiasi cha kutohoa kila neno, mimi naona ni vema kutumia haya maneno mapya kuliko yale tuliyoyazoea, na tuache kutumia lugha ya kiswahili kwa mazoea.
 
swahili kina wenyewe.
Ndio muwatafute majibu mtayapokea ya kutosha . Watu wa bara swahili wapi na wapi?
 
Nawalaumu sana hao wanatoa tafsiri za maneno na vitu mbalimbali. Tukiangalia kwa uzuri lugha ni muingiliano wa lugha mbalimbali. Ndio maana tuna maneno bora kama shati, meza, chai, pesa, hela, gari n.k. Hivi kwa nini fan iitwe pangaboi badala ya feni tulivyozoea? Computer ingekuwa komputa, television ingekuwa televisheni, fax mashine ingekuwa faksi n.k. Hakuna ubaya kuiga. Lugha zote zinaiga.
point tupu
 
tarakilishi ni nini?

Ni jina la sifa la Kompyuta {NGAMIZI}. NGAMIZI ina kazi kubwa 3. kazi moja kati ya hizo ni kuwa inatumika kama kitarakilishi. Isipokuwa haifai kuiita hivyo kwa kuwa hiyo ni sifa miongoni mwa sifa zake. Kwa maana nyingine tutakuwa na majina mengi tukifuata kila sifa ya NGAMIZI kuwa ni jina lake. Ukiita kwa jina la Kitarakilishi mimi naweza kuiita kwa jina la Kikumbukishi {data storage} na bado nitakuwa sahihi ila si jina lake. Mimi nae maneno meengi kama niko Mjengoni
 
Hapa kuna mgongano wa kiswahili cha kenya na tanzania. Kenya computer kiswahili chao ni tarakilishi, na Tanzania ni ngamizi.
Kumbuka kenya wanapenda kupita kwenye njia yao ya kiswahili kwa sababu wameshautangazia ulimwengu kwamba chimbuko la kiswahili ni kenya.Na ulimwengu umeamini hivyo kiasi kwamba akihitajika mtaalamu wa kiswahili simu hupigwa Nairobi.
 
Waswahili wengi hufikiri kwamba hakuna maana halisi ya computer na badala yake wanatohoa neno hilohilo nakuandika "Kompyuta". Hivyo ni makosa maana halisi ya Computer ni neno "NGAMIZI" na kwa laptop computer huitwa "NGAMIZI PAKATWA" Source: Ulimwengu wa kiswahili TBC1, Nawasilisha.
Napenda kujulisha wanaoshirki sehemu ya Lugha kwamba mimi peke yangu nimetunga Kamusi Fupi ya Istilahi ya Ngamizi/Tarakirishi. Kwa wakati huu sokoni hakuna kitabu cha namna hii kinachopatikana.
Mtu awe yeyote mwenye hamu ya kuwa na toleo la kitabu hicho (bure bilashi) kwa njia ya mtandao aombwe kuwasilisha nami klfmzungu@gmail.com. Nia yangu ndio kujaribu kuboresha hali kimsamiati ya Kiswahili. Tukishirikiana kwenye mradi huu hakika hadhi ya lugha hiyo itapata nafuu kubwa. Mimi mwalimu mstaafu MwIrish ambaye nimefundisha KiIngereza nchini TZ na Kenya kwa miaka ishirini hivi. Kwa muda mrefu sasa mvuto wa KiSwahili kwangu haupunguka hata kidogo.
 
Back
Top Bottom