Kigarama
JF-Expert Member
- Apr 23, 2007
- 2,492
- 1,230
Kwa zaidi ya mwaka na nusu sasa nimeshindwa kabisa kuiendesha Akaunti yangu ya face Book. Tatizo kwanza marafiki zangu niliowatafuta FaceBook wengi hawakupatikana na waliopatikana nadhani kutokana na majukumu yao tumeshindwa kuzifanya Akaunti zetu ziwe hai.
Kuna Binti mmoja ni meneja Kwenye Benki fulani hapa jijini nilipomuomba urafiki akakubali, hatimaye nikaishia kuambiwa "shikamoo kaka' hata wewe una akaunti ya Facebook?" tangu hapo hajawahi kuchangia chochote kwenye wall yangu ingawa mara zote namuona yuko online.
Nimegundua kwamba inawezekana kumbe umri nao umenitupa mkono, kwani wale niliowaona wakizaliwa sasa ni mameneja kwenye mabenki kwa hiyo wananiona kama vile nimevamia viwanja vyao. sijui niifunge akaunti yangu?
Kuna Binti mmoja ni meneja Kwenye Benki fulani hapa jijini nilipomuomba urafiki akakubali, hatimaye nikaishia kuambiwa "shikamoo kaka' hata wewe una akaunti ya Facebook?" tangu hapo hajawahi kuchangia chochote kwenye wall yangu ingawa mara zote namuona yuko online.
Nimegundua kwamba inawezekana kumbe umri nao umenitupa mkono, kwani wale niliowaona wakizaliwa sasa ni mameneja kwenye mabenki kwa hiyo wananiona kama vile nimevamia viwanja vyao. sijui niifunge akaunti yangu?