Mliopo Iringa tujuzeni mkutano upo au haupo??na hali ikoje mpka sasa??
Hata hivyo ambao huwa wanaoenda kwenye mikutano na maandamano ya kipuuzi ka hayo ni wale ambao hawana kazi za kufanya.. Kwa hiyo hata wakifanya saa 2 Asubuhi watawapata tu..
Chezea dola wewe. mkutano utakuwepo polisi ikiruhusu. Bila hivyo hakuna kitakacho endelea zaidi ya rasharasha.Sidhani kama mkutano utakuwepo maana hamna dalili zozote, na hali ya mji ni shwari...
Mtasema yote, ila mkutano hauto fanyika ulinzi ni mkali mno ambapo hata nzi wamekimbia licha ya binadamu. Hiyo ndio maana ya dola, ikisema kitu lazima kifuatwe na hakuna anae weza kuitisha dola, asogee mtu sasa aone atakacho fanywa.
Waliopelekea wakose cha kufanya ni nani?
Hata kwa kupitia ndoto haiwezi ikatokea.Simba akivamiwa na mbwa mwitu hukimbilia miguuni pa binadamu
Hiyo kitu imeingiaje tena hapo?
Chezea dola wewe. mkutano utakuwepo polisi ikiruhusu. Bila hivyo hakuna kitakacho endelea zaidi ya rasharasha.
askari wa FFU mkoani Iringa wakiwa wametanda eneo la uwanja wa Mwembetogwa ambalo Chadema ilipanga kufanyia mkutano wake leo wa kitaifa
Mkuu wa FFU mkoa wa Iringa afande Mnunka akiwa eneo la uwanja wa Mwembetogwa kuzuia mkutano wa Chadema
Mfanyabiashara eneo hilo la Mwambetogwa akihamisha bidhaa zake kukwepa shari eneo hilo ambalo limetangazwa kuwa ni eneo la hatari na FFU
Picha kwa hisani ya blog ya Francis Godwin