Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Hivi ni kweli kampuni hii ndiyo inahusika na sakata la fedha za Jairo au watu wanahisi tu? Kama wao wenyewe wanajua kuwa wanatajwa sehemu sehemu ni vizuri kama watatoa kauli mapema (pre-empty) wale wanakusudia kuitaja. Hata hivyo, kama ni kweli kampuni ilikubali kweli jukumu la kushiriki kugawa hizi fedha kwa namna yoyote nje ya sheria basi inajiweka katika mwanga mbaya sana hasa kwa vile ni kampuni ambayo imekuwa ikitumiwa bila ya shaka kwenye PR nyingine mbalimbali za serikali kama kutangaza timu yetu ya riadha kule ujerumani miaka kama miwili iliyopita. Mapema mwaka huu kampuni hiyo inayoongozwa na Bw. Aggrey Marealle ilidhamini tuzo za waandishi wa habari zinazoendeshwa kila mwaka na MCT.
Katika kutafuta ukweli, nimepata nafasi ya kuzungumza kwa kirefu na Mkurugenzi na Afisa Mtendaji Mkuu wa ES Bw. Aggrey Marealle muda mfupi uliopita ambaye kwa kauli nzito na kali amekanusha vikali kuhusika na suala la Jairo akidai kuwa kampuni yake haijawahi kuombwa, kupewa, wala kushiriki mkataba wowote unahusiana na Wizara ya Nishati na Madini, na kuwa hata kama wangeombwa wasingechukua jukumu hilo kwani wao kama kampuni ndogo ya PR ina mwelekeo wake wa shughuli zake na haihusiani na mambo ya bajeti.
"Na mimi kama Watanzania wengine, nasubiri kwa hamu kusikia ripoti ya hao watu, lakini tetesi kama hizi zinalengo la kutuchafua tu, labda pia kutokana na ushindani wa kibiashara' alisema Bw. Marealle. Nilipomuuliza zaidi kuelezea kama kwa namna yoyote kampuni yake imeshirikishwa katika kugawa fedha hizo kwa wabunge, Bw. Marealle amesema kuwa "categorically" hawakuhusika na sakata hilo kabisa, hawakupewa zabuni wala mkataba wa kufanya jambo kama hilo toka wizara ya nishati.
Katika kutafuta ukweli, nimepata nafasi ya kuzungumza kwa kirefu na Mkurugenzi na Afisa Mtendaji Mkuu wa ES Bw. Aggrey Marealle muda mfupi uliopita ambaye kwa kauli nzito na kali amekanusha vikali kuhusika na suala la Jairo akidai kuwa kampuni yake haijawahi kuombwa, kupewa, wala kushiriki mkataba wowote unahusiana na Wizara ya Nishati na Madini, na kuwa hata kama wangeombwa wasingechukua jukumu hilo kwani wao kama kampuni ndogo ya PR ina mwelekeo wake wa shughuli zake na haihusiani na mambo ya bajeti.
"Na mimi kama Watanzania wengine, nasubiri kwa hamu kusikia ripoti ya hao watu, lakini tetesi kama hizi zinalengo la kutuchafua tu, labda pia kutokana na ushindani wa kibiashara' alisema Bw. Marealle. Nilipomuuliza zaidi kuelezea kama kwa namna yoyote kampuni yake imeshirikishwa katika kugawa fedha hizo kwa wabunge, Bw. Marealle amesema kuwa "categorically" hawakuhusika na sakata hilo kabisa, hawakupewa zabuni wala mkataba wa kufanya jambo kama hilo toka wizara ya nishati.