EXCLUSIVE: Ushirikiano wa Makampuni ya Mafuta na CCM

Kiranja

JF-Expert Member
May 19, 2007
751
336
Huu ni mkataba ambao Uvccm waliupeleka kwenye baraza kuu lililofanyika Dodoma na wamekubaliana kuusaini na uliosainiwa utawekwa hapa baadae kwani wanatukwamisha na mtajua ni kwanini mafuta hayashuki bei.



IDARA YA UTAWALA, UCHUMI NA FEDHA.
2. (II) MCHAKATO WA UBIA WA KIWANJA NA. 2 "AA"MCHIKICHINI ILALA – DAR ES SALAAM.

Umoja wa Vijana wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam ulikaribisha Maombi kwa Wawekezaji wenye nia ya kuendeleza kiwanja chao kilichopo Ilala – Mchikichini chenye Hati namba 24 ‘AA' Dar es Salaam.

Katika kikao cha Baraza Kuu la UVCCM Mkoa wa Dar es Salaam lililokutana tarehe 13/01/2010 kilipokea taarifa kwamba wawekezaji watatu wameomba kuwekeza ambao ni;

(a) Camel Oil Ltd
(b) World Oil
l(c) Lake Oil

Baada ya kupitia maombi ya wawekezaji Baraza Kuu la UVCCM Mkoa wa Dar es Salaam lilimpitisha Camel Oil kuingia naye Ubia, na hivyo kuyawasilisha mapendekezo katika vikao vya UVCCM Taifa na Baraza la Wadhamini wa UVCCM kwa uamuizi wa mwisho.

Kamati ya Utekelezaji ya Baraza Kuu la UVCCM Taifa ilipokea pendekezo la UVCCM Mkoa wa DSM la kuingia Ubia na Camel Oil na kuelekeza kwamba Mwekezaji alete michoro na gharama za ujenzi. Pia aonyeshe faida itakayopata UVCCM na makubaliano haya yatadumu muda gani. Pia ilielekeza Mwekezaji ajenge si chini ya ghorofa sita badala ya tatu alizoomba mwanzo na kwa kufuata taratibu na Sheria za Mipango Miji.
UVCCM umepokea kukubali kwa Mwekezaji kuingia Ubia na UVCCM na kuleta mapendekezo ya aina mbili.

(i) Camel Oil ameomba kujenga kituo cha Mafuta (Petrol Station) katika nusu ya eneo la kiwanja, na nusu nyingine atajenga Jengo la apartments lenye ghorofa sita kwa ajili ya biashara kama mchoro unavyojionyesha katika alternative one. Eneo la kiwanja hiki ni mita za mraba 3,595.

Gharama yote ya mradi huu katika pendekezo hili ni Tshs. 3,064,300,000 kama mchanganuo wake unavyosomeka katika kiambatanisho chake.

Ø Katika pendekezo hili la Mradi, Ujenzi wake utakamilika katika kipindi cha miezi 36 mara tu baada ya kupata vibali vyote vya Ujenzi toka katika mamlaka husika. UVCCM utanufaika kwa kupata……………………….na Mbia tapata ……………… katika sehemu ya………………… na katika sehemu ya kituo cha mafuta, UVCCM atafaidika kwa………………. Na Mwekezaji atapata faida ya…………….. Mkataba huu utadumu kwa kipindi cha miaka 30.

Ø Mbia (Camel Oil) ataupatia UVCCM Mkoa wa DSM jumla ya Shs. 78,000,000/= ambazo zitatumika kufidia gharama za mpangaji wa sasa ili eneo liweze kuwa wazi tayari kwa kujenga. Mara baada ya kukamilika ujenzi, UVCCM utaweka utaratibu wa kumrudishia kiasi cha Tshs. 39,000,000/= na zinazobaki katika Tshs. 78,000,000/= yaani 39,000,000/= utakuwa ni mchango wake wa kufanikisha eneo kuwa wazi.

Ø Mbia atakuwa anaulipa UVCCM kiasi cha Tshs. 1,300,000/= kama kodi kwa kipindi chote cha ujenzi hadi hapo Ujenzi utakapokamilika. Fedha hizi hazitarudishwa.

Ø Mbia atalipia gharama zote za kubadili matumizi ya ardhi na kufanya kuwa kituo cha Mafuta

Ø Hatatumia Hati ya UVCCM kukopea Benki ili kupata mtaji wa kujengea

Ø Mara baada ya miaka 30 Mkataba utafikia ukomo na Camel Oil ataomba kupangishwa.

(ii) Hoja ya aina ya pili ya Uwekezaji inatokana na ukweli kwamba ili aweze kujenga kituo cha Mafuta lazima aombe kubadili matumizi ya ardhi katika Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi. Hivyo basi Kamati ya Utekelezaji ya Baraza Kuu la UVCCM Taifa ilimtaka Mbia alete pendekezo la pili endapo ombi la kujenga kituo cha mafuta halitakubaliwa.

Ø Katika kuwasilisha pendekezo la mradi wa Ubia na UVCCM, Camel Oil amependekeza ajenge majengo mawili yenye ghorofa sita kila moja. (Two Twin Towers). Gharama ya Ujenzi katika Mradi huu ni Tshs. 3,054,460,000/= na kwamba ujenzi utakamilika katika kipindi cha miezi 36 kuanzia tarehe ya kupata kibali cha ujenzi toka mamlaka zinazohusika. Majengo haya yote yatakuwa na ukubwa unaofanana.

UVCCM utapata mapato yake katika Jengo moja na Mwekezaji atapata mapato yake katika Jengo moja. Yaani UVCCM utamiliki 50% na Mbia atamiliki 50% na Mkataba utadumu kwa kipindi cha miaka 30.

Ø Mbia (Camel Oil) ataupatia UVCCM Mkoa wa DSM jumla ya Shs. 78,000,000/= ambazo zitatumika kufidia gharama za mpangaji wa sasa ili eneo liweze kuwa wazi tayari kwa kujenga. Mara baada ya kukamilika ujenzi, UVCCM utaweka utaratibu wa kumrudishia kiasi cha Tshs. 39,000,000/= na zinazobaki katika Tshs. 78,000,000/= yaani 39,000,000/= utakuwa ni mchango wake wa kufanikisha eneo kuwa wazi.

Ø Mbia atakuwa anaulipa UVCCM kiasi cha Tshs. 1,300,000/= kama kodi kwa kipindi chote cha ujenzi hadi hapo Ujenzi utakapokamilika. Fedha hizi hazitarudishwa.

Ø Mbia atalipia gharama zote zinazohusiana na mchakato wa Ujenzi, ikiwa ni pamoja na kupata vibali vya Ujenzi.
Ø Mbia hatatumia Hati ya UVCCM kukopea Benki ili apate mtaji wa kujengea mradi huo.
Ø
Mara baada ya miaka 30 Mkataba kati ya UVCCM na Mbia utakoma na Mbia ataomba kupangishwa.

 
Wewe unazani ni kwa nini makampuni yanagoma? Hawa watu hawawezi kuwa na kiburi kiasi hicho. Kuna watu wako nyuma yao.
 
Huko nyuma niliwahi kusikia kuwa mafuta huwa yanapanda bei kwa maana kuna kiasi kadhaa makampuni haya huwa yanakata na kuingia moja kwa moja kwenye akaunti ya CCM kwa ajiri ya matumizi ya chama.

Kama fununu hizi zitakuwa na ukweli wowote basi serikali iko rehani maana kupanda kwa bei za mafuta ni moja ya chanzo cha mapato ya CCM na hivyo basi CCM kusema leo bei zishuke ni usanii na kamwe haiwezekani ama sivyo hawataki tena mapato kutoka makampuni ya mafuta, kaaazi kwelikweli!
 
we are destoyed by lack of wisdom of not re electing ccm into power last year
 

Ø Mbia atakuwa anaulipa UVCCM kiasi cha Tshs. 1,300,000/= kama kodi kwa kipindi chote cha ujenzi hadi hapo Ujenzi utakapokamilika. Fedha hizi hazitarudishwa.
Ø Mbia atalipia gharama zote zinazohusiana na mchakato wa Ujenzi, ikiwa ni pamoja na kupata vibali vya Ujenzi.
Ø Mbia hatatumia Hati ya UVCCM kukopea Benki ili apate mtaji wa kujengea mradi huo.
Ø Mara baada ya miaka 30 Mkataba kati ya UVCCM na Mbia utakoma na Mbia ataomba kupangishwa.

mkuu hapo kwenye green, hao UVCCM WAMEKUWA TRA?
 
Magamba wash******i sana kumbe mikataba ya Kichama waifanya kwa Makini lakini Mikataba ya Rasilimali zetu wanatuingiza mkenge
 
MKATABA WA KUENDELEZA PLOT NO. 24, BLOCK ‘AA', MCHIKICHINI, DAR ES SALAAM, KWA NJIA YA UBIA
MKATABA HUU WA UBIA UMEFANYIKA LEO

TAREHE¼¼¼¼¼¼ MWEZI¼¼¼¼¼¼¼¼¼2011

BAINA YA
BARAZA LA WADHAMINI LA UMOJA WA VIJANA WA CHAMA CHA MAPINDUZI
NA
CAMEL OIL CAMPANY LIMITED.
UMETAYARISHWA NA:
GLORIOUS LUOGA,
MWANASHERIA WA CCM,
MAKAO MAKUU YA CCM,
P.O.BOX 50,
DODOMA.

MKATABA WA KUENDELEZA PLOT NO. 24, BLOCK ‘AA', MCHIKICHINI, DAR ES SALAAM, KWA NJIA YA UBIA

MKATABA HUU WA UBIA UMEFANYIKA LEO

TAREHE ¼¼¼¼¼MWEZI¼¼¼¼MWAKA 2011.
BAINA YA

BARAZA LA WADHAMINI LA UMOJA WA VIJANA WA CHAMA CHA MAPINDUZI, wa S.L.P 19989, DAR ES SALAAM ( ambao hapo baadaye pale panaporuhusu katika mkataba huu wataitwa "Mmiliki" neno ambalo litamaanisha pia yeyote atakayechukua nafasi yao) kwa upande mmoja,
NA
CAMEL OIL CAMPANY LIMITED, ya S.L.P 22786, DAR ES SALAAM kampuni iliyosajiliwa chini ya sheria ya makampuni, sura 212, (ambayo hapo baadaye pale panaporuhusu katika mkataba huu itaitwa "Mbia", neno ambalo litamaanisha pia Wafilisi wake au yeyote atakayechukua nafasi yake) kwa upande mwingine,

KWA KUWA Mmiliki ndiye mmiliki halali wa eneo lenye ukubwa wa mita za mraba 3,595 linalojulikana kama Plot No. 24, Block ‘AA', eneo la Mchikichini, Dar es Salaam, ambalo Mmiliki analimiliki chini ya namba 41986( eneo ambalo hapo baadaye katika mkataba huu litaitwa "Kiwanja Kinachohusika" )



KWA KUWA Kamati ya Utekelezaji ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Dar es Salaam kwa niaba ya Baraza la Wadhamini wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi katika kikao chake kilichokutana tarehe 08/06/2008 pamoja na mambo mengine kilijadili barua ya maombi ya uwekezaji ya kampuni ya Camel Oil Campany Limited kwa njia ya ubia na Umoja wa Vijana wa CCM katika kuendeleza kiwanja kilichotajwa hapo juu.

KWA KUWA CAMEL OIL CAMPANY LIMITED, ya S.L.P 22786, Dar es Salaam, alithibitishwa na Baraza la Umoja wa Vijana wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam kwa barua ya tarehe ¼¼¼¼¼¼. yenye kumbukumbu namba ¼¼¼¼¼¼¼¼ambayo nakala yake imeambatishwa katika mkataba huu.

KWA KUWA Mbia atawasilisha ramani na michoro kwenye Kamati ya Utekelezaji ya Umoja wa Vijana wa CCM, Mkoa wa Dar es Salaam ambayo inaendana na makubaliano yaliyo chini ya Mkataba huu.

NA KWA KUWA, Mbia atashirikiana na Mmiliki juu ya upatikanaji wa kibali cha ujenzi kutoka mamlaka zinazohusika.


HIVYO BASI MKATABA HUU NI USHUHUDA KUWA PANDE ZOTE ZIMEKUBALIANA KAMA IFUATAVYO:-

1. AINA YA MRADI:

Mkataba huu unahusu uendelezaji wa kiwanja kilichotajwa hapo juu kwa kubomoa jengo lililopo wakati wa kutengeneza mkataba huu na kujenga jengo jipya la kisasa lenye urefu wa ghorofa sita(6) kwa ajili ya Malazi/biashara na kituo cha mafuta kwa gharama ya Tsh3,064,300,000/= tu. Au kama kibali cha kujenga kituo cha mafuta kitakosekana kujenga majengo pacha mawili ya ghorofa sita(6)kila moja likiwa na apartments 12 kwa ajili ya makazi,hotel na ofisi kwa gharama ya Tsh. 3,054,460,000 tu.


2. MCHANGO WA MMILIKI:

Mchango wa Mmiliki kwenye mradi huu wa ubia utakuwa ni kama ifuatavyo:-

i. Kutoa Kiwanja chake kwa ajili ya mradi wa ubia.ii. Kumhamisha mpangaji aliyopo sasa katika jengo lililopo kwenye kiwanja kinachohusika wakati wa kutengeneza mkataba huu.iii. Kuomba kibali cha ujenzi kwa kushirikiana na Mbia. 3.MCHANGO WA MBIA:


Mchango wa Mbia kwenye mradi huu utakuwa kama ifuatavyo:-


i. Kujenga kwenye kiwanja kinachohusika kwa gharama zake kama ilivyoelevya katika kifungu cha kwanza(1) hapo juu na kwa mijibu wa michoro itakayokubalika na pande zote na mamlaka husika.



ii. Mbia atatoa jumla ya Tsh. 78,000,000/= (Shilingi Milioni sabini na nane) kwa Umoja wa Vijana wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam. Kati ya hizo 39,000,000/= (Milioni thelathini na tisa) utakuwa mchango wa Mmbia kwa Umoja huo na Tsh. 39,000,000/= nyingine atawakopesha Umoja wa Vijana wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam kama sehemu ya kufanikisha kulipa madeni ambayo Umoja huo unadaiwa katika kumhamisha mpangaji aliyepo.

iii. Fedha ambazo Umoja wa Vijana wa CCM utakopeshwa na Mbia zitarejeshwa kwa Mbia kutoka kwenye mgao wa mapato ya Mmiliki baada ya ujenzi kukamilika kwa makubaliano ambayo Mbia na Mmiliki watakubaliana.

iv. Mbia atakuwa na majukumu yafuatayo:-


a) Kutayarisha mkataba wa ubia na kulipia gharama zake.
b) Kubomoa jengo lililopo kwenye kiwanja kinachohusika.
c) Kumteua Msanifu wa ujenzi (Architect) na kumlipa gharama zake.
d) Kumteua Mhandisi Mshauri wa Mradi na kumlipa gharama zake.
e) Kutayarisha michoro kwa gharama zake na kuiwasilisha kwenye kikao kati ya Mmiliki na Mbia kwa ajili a kuipitisha.
f) Kulipia gharama za kibali cha ujenzi.
g) Baada ya kukamilisha ujenzi atalisimamia kwa gharama zake katika masuala ya usafi, maji, upatikanaji wa nishati ya ziada kwa kupata umeme, ukarabati, ulinzi na huduma zingine za majengo.

4.MAJUKUMU YA PAMOJA:

Mmiliki na Mbia watashirikiana katika kufanikisha majukumu yafuatayo:-

i. Kupitisha michoro itakayochorwa na Msanifu wa Ujenzi (Architect).
ii. Kuomba na kufuatilia kibali cha ujenzi. 5.MUDA WA KUMKABIDHI MBIA KIWANJA:

Mmiliki atamkabidhi Mbia kiwanja kinachohusika na mradi huu kikiwa wazi kwa ajili ya kumwezesha Mbia kubomoa jengo lililopo kwa sasa si zaidi ya miezi 3 kuanzia tarehe ya pande zote kutia saini mkataba huu, isipokuwa tu kama mmiliki atazuiwa kufanya hivyo kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wake kama vile amri ya Mahakama, n.k. Katika mazingira hayo Mmiliki atamkabidhi kiwanja kinacho husika kikiwa wazi kwa ajili ya kubomoa jengo lililopo kwa sasa mara tu baada ya kipingamizi cha aina hiyo kutoweka.

6.MUDA WA KUKAMILISHA UJENZI:

Mbia atakamilisha ujenzi wa jengo na kituo cha mafuta katika muda wa miezi 36 kuanzia tarehe ya kupata kibali cha ujenzi, labda ikiwa Mmiliki atakuwa amechelewa kumkabidhi Mbia Kiwanja kinachohusika kikiwa wazi kama ilivyoelezwa hapo juu. Katika hali kama hiyo, muda ambao Mbia atakuwa anasubiri kukabidhiwa Kiwanja kinachohusika kikiwa wazi hautahesabiwa katika kupata hiyo miezi 36 ambayo ndani yake Mbia anatakiwa awe amekamilisha ujenzi.

7.MKATABA WA UPANGAJI

Mara baada ya ujenzi kukamilika mmiliki atampa mpangaji mkataba wa upangaji wa muda wa miaka 36 kwa masharti ambayo pande zote mbili zitaafikiana.

BILA YA KUATHIRI MATAKWA YA HAPO JUU

i. Mbia atalipa kodi ya kuanzia ya Tsh 7,500,000/= kwa mwezi .
ii. Kodi itaongezwa kila baada ya miaka mitatu kwa asilimia kumi(10%)
iii. Pande zote mbili zitaweza kukubaliana masharti mengine ya upangaji.
iv. Jengo litasimamiwa na mbia na mbia atakuwa na haki na wajibu wa kutafuta wateja wa kupanga katika jingo hilo kukusanya mapato na kulipa kodi ya mapato.
v. Mmiliki atawajibika na ulipaji wa kodi ya kiwanja

8.UTATUZI WA MIGOGORO:

Ikiwa kutatokea kutoelewana kwa aina yeyote ile baina ya Mmiliki na Mbia kuhusu jambo lolote linalohusu ubia ulioundwa chini ya Mkataba huu au linalohusu mkataba huu au fasili yake, basi katika hali hiyo pande zote zitatumia jitihada zake zote ili kumaliza kutoelewana huko kwa njia ya Muafaka na ikiwa njia hiyo itashindikana, basi pande zote zinakubaliana kushughulikia kutoelewana huko kwa njia ya usuluhishi chini ya sheria ya Usuluhishi (Arbitration Act, Cap. 15).
9. KUSITISHA MKATABA:

Ikiwa Mbia atashindwa kukamilisha mradi unaohusika katika muda uliokubalika na pande zote, basi Mmiliki anaweza kumpatia Mbia taarifa (notice) ya siku 60, ya kurekebisha ucheleweshaji huo. Ikiwa Mbia atashindwa kurekebisha ucheleweshaji huo baada ya kupewa "notice", basi Mmiliki anaweza kukatisha mkataba huu na ikiwa itatokea hivyo Mbia atakuwa na haki ya kurejeshewa pesa alizotumia katika ujenzi

unaohusika kwa kiasi ambacho pande zote zitaafikiana na ikiwa pande zote hazitaafikiana kuhusu kiasi cha pesa alizotumia Mbia, basi Mthamini Mkuu wa Serikali (Chief Government Valuer) atafanya tathimini ya gharama alizotumia Mbia. Ikiwa itaonekana kuwa Mmiliki amepata hasara kutokana na ucheleweshaji wa Mbia, basi Mbia atalipa fidia kwa Mmiliki kwa kiwango kitakacholingana na hasara atakayokuwa amepata Mmiliki. 10. WAWAKILISHI WA WAHUSIKA:

Pande zote zimekubaliana kuwa mwakilishi halali wa Mmiliki kwa ajili ya Mkataba huu ni Katibu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi, Mkoa wa Dar es Salaam, ambaye anuani yake ni S.L.P 21598, Dar es Salaam. Mwakilishi halali wa Mbia kwa ajili ya Mkataba huu ni Mkurugenzi Mtendaji, Camel Oil Campany Ltd., S.L.P 22786, Dar es Salaam.
11. FIDIA YA KODI KWA MMILIKI WAKATI WA UJENZI:

Kwa kuwa Mmiliki alikuwa anayatumia majengo yaliyokuwepo katika kiwanja husika kwa kupangisha na kulipwa kodi, Mbia amekubali kumlipa kodi ya shilingi Tsh 1,300,000/= (milioni moja laki tatu) kwa mwezi katika kipindi chote cha miezi 36 ya ujenzi.

12.VIAMBATANISHO:


Pande zote zinakubaliana kuwa nyaraka zifuatazo zitaambatabishwa kwenye Mkataba huu na kusomeka kama sehemu ya Mkataba huu: (a)Michoro ya ujenzi iliyoidhinishwa na kikao cha pamoja kati ya Mmiliki na Mbia.
(b)Vibali vya ujenzi

KAMA USHUHUDA WA MKATABA HUU PANDE ZOTE ZIMEWEKA LAKIRI ZAKE KWA NAMNA NA KATIKA TAREHE NA MWAKA KAMA ILIVYOONYESHWA HAPA CHINI.
UMETIWA LAKIRI YA BARAZALA WADHAMINI WA UMOJAWA VIJANA WA CCM na kutolewaHapa Dar es Salaam

mbele yetu leo ¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼.. ¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼.Tarehe ¼¼¼. Mwezi ¼¼. Mwaka2011Jina:¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼Sahihi: ¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼..¼¼¼¼.Anuani ya Posta: ¼¼¼¼¼¼¼..¼¼¼.¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼.Wadhifa: ¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼..Jina:¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼Sahihi: ¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼..¼¼¼¼.Anuani ya Posta: ¼¼¼¼..¼¼¼¼¼¼.¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼.Wadhifa: ¼¼¼¼¼¼¼¼.¼¼¼¼¼..

UMETIWA SAINI NA CAMEL OIL COMPANY LTD. na kutolewa

Hapa Dar es Salaam mbele yetu leo ¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼.... Tarehe ¼¼¼. Mwezi ¼¼. Mwaka2011Jina:¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼Sahihi: ¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼..¼¼¼¼.Anuani ya Posta: ¼¼¼.¼¼.¼¼¼¼¼. ¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼.Wadhifa: ¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼..Jina:¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼Sahihi: ¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼..¼¼¼¼.Anuani ya Posta: ¼¼¼¼¼¼..¼¼¼¼.¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼.Wadhifa: ¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼¼..
 
Hii ni kwenye kiwanja kimoja tu!!! Vipi kwenye madini, mafuta, gesi, wenye viwanda?
 
  • Thanks
Reactions: FJM
KINACHOTUTAFUNA TANZANIA HADI HIVI SASA NCHINI NI UKOSEFU WA UONGOZI ADILIFU NA KUKOSEKANA UTAWALA BORA KIUTENDAJI

Ni ajabu na kweli kuona jinsi ambavyo watawala wanavyoenenda katika shughuli zao za kila siku. Kama mtu bado huamini tu basi hebu tu wewe mwenyewe tupe JIBU hapa jukwani.

Hebu jaribu kutufahamisha kama kweli hali halisi kama ilivyoainishwa hapo chini kweli itasaidia kukuza MASLAHI YA UMMA katika nchi hii au ni ukuta wa kuendeleza MASLAHI BINAFSI kwa kutupora sisi kama taifa:

Mpaka hapa mtu kweli unategemea WATUMISHI WETU huko serikalini kweli watawezaje kufanya kazi yao ipasavyo na kwa mujibu wa sheria zetu bila kupindapinda pale unapomkuta mkuu wa nchi tayari katamalaki kila upande kiasi cha kuona;

1. Kikwete Mwenyekiti wa CCM Taifa

2. Akitupa geresha za Kumuagiza Kikwete Rais na Kiongozi wa Serikali ili naye

3. Akumamrishe yule Kikwete Mfanyabiashara wa mafuta pale Lake Oil akapunguze bei ya mafuta.

Ewe Mzee Wassira, kwa nini hamkuliona hili na kumshauri mkuu wa nchi; DHANA YA UTAWALA BORA sasa uko wapi hapa??? Mbona kinyaa hivi!!!!!!!!!!!!

Mzee Simbeye, Wakuhenga, Warioba, Kubenea, Mjengwa na Jenerali Ulimwengu, nyinyi kama wakosoaji wa jamiiyetu hii hili hamkuliona???????

Kweli kabisa mtu ukijitwisha kofia hizi zote tatu na kujizivalia umaridi kabisa wewe mtu mmoja tu, Dr Hosea, kweli bado kunakosekana hali ya MGONGANO WA KIMASLAHI ambao hivi sasa inasababisha Watanzania tuliowengi kuwa WALAZWAHOI.

Hapana, Hapana na Hapana; hatutaki tena wala hutusikii cha mtu hapa - ulaghai na ufisadi sasa basi mwishoooo!!!! Mpaka hapa wala mtu huitaji kuwa na elimu ya hata sekondari kugundua kwa nini mambo kila siku hayaendi kwa njia nyoofu huko serikalini badala yake watu kuzunguka tu mbuyu; kumbe kuna Joka kuu katamalaki na kuenea kila kona!!!

Watanzania wenzangu, ni kati ya Kikwete yupi kati ya hao watatu atakayeweza kupata kweli ujasiri na uhalali wa kumdhibiti yule Kikwete mwingine?????

Mbona tunachezewa shere siku zote hivi nchini na bado tu watu hatuoni haya yote????????????? Je baada ya kusoma na kutafakari haya niliyoyaandika hapo juu:

1) Je, bado unayo imani na Hoja ya Dharura ya Januari Makamba kule bungeni Dodoma??

2) Je, bado unategemea kusikia kutolewa kwa agizo lolote na serikali yetu na ikazingatiwa???

3) Je, mpaka hapo bado unaamini kuwa EWURA ni chombo cha kulinda maslahi yetu Umma wa Tanzania????

4) Je, kwa hiyo hali hapo juu na ukipiga picha na kwingineko kama eneo la matatizo sugu ya maji, maliasili na umeme nchini bado tu utakua unaamini kweli kwamba Dr Hosea bado anayo meno ya kuweza kutafuna mtu au kampuni yoyote hapa nchi kwa madai ya UFISADI???????????????????

Tafakari zaidi na zaidi na mwisho ujishauri mwenyewe jinsi UTAKAVYOTUMIA HAKI YAKO YA KUPIGA KURA siku za usoni!!!!!!!!!!
 
KUMBE MAGAMBA YOTE YALIOKIOTA CCM MWILI MZIMA NI KULE KUJIINGIZA KATIKA BIASHARA????

Madudu ya CCM sasa hadharani kila kona mtaani!!!!!!!!!!

Nawachukia kuliko kwa kukigeuza hiki chama kisafi cha Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, kuwa pango la wanyang'anyi kiasi hiki.

Nasema NAKICHUKIA KUFA hiki CCM FOTOKOPI kwa jinsi kilivyosaliti DHAMIRAyetu kama taifa. Wasaliti wakubwa nyinyi; mmewasaliti WADAU WA MSINGI WA CCM (Wakulima na Wafanyakazi) na sasa chama kujiingiza moja kwa moja katika kufanya biashara hadi ikulu na kutuacha solemba!!!!!!!

Mzee Warioba, Salim, Salmi Komandoo, Lyatonga Mrema na wengine wengi wa aina yenu tunaowaheshimu sana; tunasema hii CCM si ile ya Mwalimu hivyo hatuambiliki tena wala hatusikilizi na nyuma haturudi.


CCM wametumaliza! I hate them from the bottom of my heart!
 
haya tuliyataka wenyewe kwa kutojifunza baada ya kuona kipindi cha usanii wa maisha bora kwa kila mtangagiza
 
Wakati wa kampeni Dr. Slaa alitumia mara nyingi kauli tata iliposema kuwa kumchagua kikwete ni sawa na janga la kitaifa. Wengi wetu tulijua kuwa ni maneno ya kisiasa tu. Tukambeza! Sasa taratibu nimeanza kuamini kile alichosema Dr. Slaa kwa kuangalia sakata linaloendelea hivi sasa la ukosefu wa nishati muhimu ya mafuta. Hivi sasa, wananchi mitaani wanahangaika na kuteseka kwa sababu tu ya kuwa na serikali legelege inayoweza kupewa masaa 24 na mfanyabiashara mmoja tu. Hicho ni kituko cha mwaka na nadhani kimetokea kwa mara ya kwanza nchini Tanzania. Watanzania tujiandae kwa majanga mengine zaidi maana wafanyabiashara wakubwa "wameishika" serikali eneo kubwa siyo kwenye sekta ya nishati tu.
 
  • Thanks
Reactions: DSN
Back
Top Bottom