Abdulhalim
Platinum Member
- Jul 20, 2007
- 17,193
- 3,011
Nijuavyo ardhi ni mali ya serikali. Au??
Nijuavyo ardhi ni mali ya serikali. Au??
Hivi wote hamuoni hizi picha au baadhi ya watu tu?
Naamini kwa sasa picha zinaonekana...
hommie,Yeeeh nazipta vizuri kweli....very clear hakuna chenga kabisa aiseee!
Hivi what should be done to stop this? je, ni kupiga kelele na how? na je, who approved this? na kwa manufaa ya nani?
Picha zinaonekana, ila Mzee Mwanakijiji umeziacha kwenye file kubwa, hivyo internate zenye speed ndogo kama nyingi ya cafe zetu, then haifungui, ila picha zipo.
Ukanda wote wa beach toka Toure drive inakoanzia mpaka Sea Cliff, imeuzwa, miti yote imeshakatwa, wenye viwanja vyao wameanza kufanya fencing, hadi Coco Beach, yule mmiliki Alphonse Buhatwa, amepiga kelele sana, sijua kama kilio chake kimesikika na kubakizwa miongoni mwa wamiliki..
Tayari Zainudeen Adamjee amewaorganize wakazi, wamepinga mahakamani, ujenzi umeshasimamishwa. Nalo Baraza la Usimamizi wa Mazingira limewashikia kidedea wakitaka EIA kwanza.
Kwa mliosoma ile Ripoti yas Warioba, ilisema wazi kuwa Rais Mwinyi, ilisaini badiliko la matumizi ya ardhi ile kwa kutegua ile sheria ya mkoloni iliokataza ujenzi wa kando ya bahari.
Viwanja 18 wilipimwa kwa presidential discretion na alipewa yeye, familia yake na marafiki zake.
Miongoni mwa viwanja hivyo 18, ni 2 tuu ndio vimeendelezwa ambavyo vilitolewa kwa rafiki zake. Hivi ni kile kilichojengwa Sea Cliff na Golden Tulip, hivyo 16 vilivyobaki havijaendelezwa, sasa wamiliki waliogaiwa ndia wameamuas kuviendeleza, kelele za nini?
Baada ya rais kutengua lili zuio la mkoloni na baada ya kuwagawia hao nduguze na rafikize, ndipo rekebisho lilipelekwa bungeni kuwa endorsed. Mzindakaya alipiga kelele sana, iweje jambo lifanyike kwanza, kinyume cha sheria, halafu bunge lilitewe kuubariki uchafu huo!
Bunge likakaa kama kamati ya chama, Mzindakaya akatulizwa, nadhani kwa chochote kitu, ukiwemo mgao wake kwenye vitalu vya uwindaji, akatulia. Bynge likarejea, na wakabariki, sasa cha kushangaza ni kipi hapa?
Nchi ilishauzwa siku nyingi, wenye nacho, wanaongezewa, wasio nacho, wananyang'anwa kidogo walichonacho, hivyo tutafikia mahali, watoto wetu na watoto wa watoto wetu, waishia kuwa wapangaji ndani ya nchi yao for the rest ofb their life, by that time, waliofanya hayo, na tulioshuhudia yakifanyika na tukaa kimya, we will have been long gone!.
I don't think so.Serikali inshika dhamana tu....mmiliki ni mwananchi
wenzangu mnatumia mitandao gani? Mbona miye naziona vizuri tu?
Pasco,
Umenipa mwanga mkubwa sana leo hapa! Umeandika vizuri sana, umeweka ALFA na OMEGA ya hili sakata.....sikuwahi kusikia wala kusoma pahala popote hii mambo aisee....very painful!
Ni baadhi yetu ndio hawaoni lakini zipo clear or wengine huziona lakini washakula ten percent yao thats y wana act like hawazioni!!Hivi wote hamuoni hizi picha au baadhi ya watu tu?
itafikia kipindi kila kipande cha nchi hii kitauzwa na tutaambiwa tuhame sasa shughuri itakuja wapi pa kwenda; ni hatari sana